Thursday, April 17, 2014

UNABII JUU YA TANZANIA KUHUSU MAMBO YA KATIBA NA MUUNGANO:



Mwana wa Nabii Mchungaji Mtalemwa Dionis wa kanisa la Enlightened Christian Gathering ( ECG ) CHURCH ARUSHA BRANCH TANZANIA amekuwa akitoa unabii mbalimbali kwa watu binafsi na jamii kwa nyakati mbalimbali, Mungu amekuwa akimtumia kutoa unabii wa mabomu Arusha kabla hayajotokea kwa kutaja siku na tarehe na maeneo, majanga ya moto Arusha, mafuriko Dar es salaam na maeneo mengine.Mara zote huwataka watu kuomba na kuchukua tahadhari mapema ili kuepuka madhara, katika mojawapo ya mafundisho yake katika ibada alisema madhara yanayotabiriwa yanatokea kwasababu watu hawaombi kikamilifu baada ya kupewa unabii, wengine wanaomba ila hawachukui tahadhari, wengine wanadharau unabii na kukejeri lakini kundi jingine haliamini kabisa, kwasababu hiyo madhara huwapata watu, akifafanua alisema lengo la Mungu kutujulisha mapema ni ili tuchukue hatua ili madhara yasitupate kama walivyochukua hatua watu wa Ninawi (Yona 3:4-10).Jumapili tarehe 13/04/2014 Mwana wa Nabii akiwa anaongoza ibada ya kinabii kanisani kwake ECG eneo la Sanawari Manchester Arusha aliwahimiza waumini kuomba juu ya malumbano yanayoendelea Bungeni juu ya katiba na Muungano na haya ndiyo yalikuwa maneno yake "Mungu anatutaka tuombe zaidi maana naona kuanzia sasa hadi tarehe 26 Aprili kundi la wanasiasa watakaodai kuchoshwa na mambo ya mjadala wa katiba juu ya Muungano wataamua kupinga kwa vitendo na kuendelea kuwashawishi wengine ili wasiikubali hata siku ya kitaifa ya muungano yaani tarehe 26 april" Aliendelea kusema kwamba tarehe 26 kuna watu wamepanga kwenda barabarani na mabango wakidai pawepo na serikali tatu" Siku zote Mwana wa Nabii huwa anasisitiza kwamba hayuko upande wowote wa chama cha siasa ila huwa anaeleza lile Mungu analosema juu ya watu na kuwaelekeza la kufanya, aliendelea kutoa unabii akisema "watakaokusanyana na kupinga naona wakisambazwa na polisi na wengine kuumizwa vibaya" Tunawashauri watu kuomba ili Mungu atuongoze la kufanya juu ya muundo wa serikali na siyo kurumbana. Kwa waombaji wote andika "Mungu tupe suluhisho la katiba"
BreakingNews:
UKAWA waondoka Bungeni! Lipumba adai wao wanawaachia Intarahamwe ukumbi waendelee watakavyo!
Fuatilia yaliyojiri Bungeni hapa - http://bit.ly/1ipbVBc

No comments:

Post a Comment