Thursday, January 15, 2015

KAKOBE: UCHAGUZI USIFANYIKE JUMAPILI


  1.  
    Juzi Jumapili 11.1.2015, maelfu ya waumini wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) linaloongozwa na Askofu Mkuu Zachary Kakobe, walivaa TShirt zenye maandishi “UCHAGUZI USIFANYIKE JUMAPILI”, katika ibada maalum ya maombi kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Katika maombi hayo maalum yaliyofanyika katika Kanisa hilo lililoko barabara ya Sam Nujoma, Mwenge, Dar-Es-Salaam; Askofu Kakobe aliwaongoza waumini hao kumshukuru Mungu kwa ajili ya roho ya usikivu iliyomwingia Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliyetangaza katika hotuba yake ya Mwaka Mpya kwamba Kura ya Maoni kuhusu Katiba pendekezwa itafanyika ALHAMISI 30.4.2015.

    Katika maombi hayo, Askofu Kakobe alisema kwamba kwa miaka mingi, kilio cha Wakristo wengi kimekuwa kwamba siku ya kupiga kura isiwe siku ya Jumapili inayoingilia haki ya Kikatiba ya kupiga kura na uhuru wa kuabudu kwa Wakristo usiotakiwa kuingiliwa na mamlaka ya nchi, kama inavyoainishwa katika Katiba, Ibara ya 5 (1) na Ibara ya 19 (2); hivyo hawana budi kumshukuru Mungu kwa jinsi ambavyo Serikali ilivyosikia kilio chao, kwa kutangaza kwamba Kura ya maoni itafanyika Siku ya Alhamisi, badala ya siku iliyozoeleka ya Jumapili.


    Kwa msingi huohuo, waumini hao walimwomba Mungu katika maombi hayo kwamba, Serikali izidi kuwa na usikivu na hivyo kutangaza siku ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ambayo haitakuwa Jumapili, wala Jumamosi wala Ijumaa; ambazo ni siku za kuabudu kwa waumini wa madhehebu yote ya Wakristo, Wasabato na Waislamu; ili Wakristo na Watanzania wote kwa ujumla wapate kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura. Askofu Kakobe alisema kwamba imekuwa kawaida kwa wanasiasa kujiuliza kwa nini watu wengi hawajitokezi siku ya kupiga kura, bila kuwaza juu ya kujenga mazingira ya kuwawezesha watu wote kupiga kura, kwa kuifanya siku ya kura kutokuwa siku ya Ibada.


    Askofu Kakobe alitoa mifano ya nchi zinazotuzunguka ambazo hufanya Uchaguzi wao Mkuu kuwa siku ambayo siyo siku ya Ijumaa, Jumamosi au Jumapili; ili watu wengi wajitokeze kupiga kura, kwa mfano Zambia ambayo itakuwa na Uchaguzi siku ya JUMANNE 20.1.2015, baada ya Rais wao aliyechaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wa JUMANNE 20.9.2011, kufariki. Vilevile alitaja siku za Uchaguzi Mkuu uliopita wa nchi nyingine kama ifuatavyo: Malawi (JUMANNE 20.5.2014); Zimbabwe (JUMATANO 31.7.2013); Kenya (JUMATATU 4.3.2013); Uganda (JUMATATU 18.2.2011); Rwanda (JUMATATU 9.8.2010); Burundi (JUMATATU 28.6.2010); na Afrika Kusini (JUMATANO 7.5.2014); na baada ya kutaja mifano hiyo, aliwaongoza waumini kumwomba Mungu ili kwamba Serikali iwe na usikivu katika jambo hili pia, na kutangaza Siku ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu wa 2015 katika nchi yetu Tanzania, kuwa siku yoyote ambayo siyo Jumapili, Jumamosi, wala Ijumaa; na kuifanya siku hiyo kuwa siku ya mapumziko maalum yenye kazi moja tu kuu, ya kupiga kura.





























    Attached Thumbnails Attached ThumbnailsClick image for larger version. 

Name: 3C9A0956.jpg 
Views: 0 
Size: 201.9 KB 
ID: 218234   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0898.jpg 
Views: 0 
Size: 315.5 KB 
ID: 218235   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0899.jpg 
Views: 0 
Size: 288.7 KB 
ID: 218236  Click image for larger version. 

Name: 4B7A0900.jpg 
Views: 0 
Size: 334.1 KB 
ID: 218237   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0901.jpg 
Views: 0 
Size: 297.8 KB 
ID: 218238   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0908.jpg 
Views: 0 
Size: 351.1 KB 
ID: 218239  Click image for larger version. 

Name: 4B7A0909.jpg 
Views: 0 
Size: 339.3 KB 
ID: 218240   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0910.jpg 
Views: 0 
Size: 355.7 KB 
ID: 218241   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0944.jpg 
Views: 0 
Size: 332.8 KB 
ID: 218242  Click image for larger version. 

Name: 4B7A0945.jpg 
Views: 0 
Size: 290.5 KB 
ID: 218243   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0947.jpg 
Views: 0 
Size: 296.9 KB 
ID: 218244   Click image for larger version. 

Name: 4B7A0948.jpg 
Views: 0 
Size: 331.9 KB 
ID: 218245  Click image for larger version. 

Name: 4B7A0999.jpg 
Views: 0 
Size: 300.3 KB 
ID: 218246   Click image for larger version. 

Name: 3C9A0971.jpg 
Views: 0 
Size: 259.4 KB 
ID: 218247   Click image for larger version. 

Name: 3C9A1004.jpg 
Views: 0 
Size: 214.6 KB 
ID: 218248SOURCE: JAMII FORUM  

Wednesday, January 14, 2015

NILIMPENDA MSICHANA KUMBE NI JINI NA AMENITESA SANA

     


                Naitwa Patrick Bundala niko mailimoja Kibaha ni mwajiriwa wa serikali ni Askari ila nyumbani ni Tabora na huku niko kikazi tu, nina mke na watoto 4. Kuna kitu kibaya kilinitokea nikiwa kozi ya uongozi huko Zanzibar mwaka 2009, tukiwa kozi tulikua tunapata mapumziko siku za weekend hivyo kutumia nafasi hiyo kwenda kutembea beach na siku hiyo ya tukio baya  ilikua jumamosi ambapo tuliondoka tukiwa wengi tu kama 50 na kwenda maeneo ya kilimani karibu na migombani ambako kuna beach nzuri sana na siku ya jumamosi jioni beach huwa inajaa watu wa kila aina na siku hiyo haikua mara ya kwanza mimi kwenda huko beach kwani kila weekend lazima niende huko beach ili kuburudisha macho na kuangalia mazingira na watu maana mimi kwa Zanzibar ilikua mara ya kwanza kwenda hivyo kwa umaarufu wa Zanzibar nilitaka hadi natoka huko niwe na cha kuwasimulia huku nyumbani kumbe ilikua bahati mbaya sana kwangu siku hiyo, wakati siku hiyo tumefika beach tulitawanyika kila mtu eneo analotaka na wengine walienda kuogelea na mimi licha ya kufahamu kuogelea lakini siku hiyo sikutaka kuogelea lakini nilitaka kutafuta binti mzuri ili nimtongoze na tuwe wapenzi na nilienda pembeni kidogo eneo ambalo watu walikua wachache na kukaa mkao wa kuangalia watu na baada kama ya dakika 40 alipita dada mmoja aliyevaa ninja akiwa ni nusu mwaarabu na nusu mwafrika na nikajikuta namtamani sana alinipita kidogo na kugeuka na kuniangalia na mimi nikaona hiyo ndio nafasi ya kumwogelesha na kikamwita akaja na ajabu sikumwambia chochote lakini sijui aligundua kuwa natafuta mwanamke maana alisogea na kunisalimia na akakaa pembeni yangu na kunichangamkia sana, na kwa sababu nilitaka mpenzi nilidhani kuwa huyo ni changudoa ambaye huwa anaenda kutafuta wanaume beach, Baada ya kukaa tuliendelea na story na ajabu yule dada akaniambia mwenyewe kuwa amenipenda sana maana nimemjali na mimi nikaona kuwa  hiyo nafasi ya kumpata mrembo yule siwezi kuipoteza na muda huo huo nikaanza kumwambia mambo ya mapenzi maana nilidhani ni kahaba na nilipomwambia hivyo alicheka na kusema amekubali ila anataka ajue kwanza jina langu, kwa sababu ya kuepusha maswali ya kuulizwa zaidi na ili asije akakataa kwa sababu ya majina yangu ya kikristo japokua hata kanisani sijawahi kwenda nilimwambia kuwa mimi naitwa Saleh Juma na yeye akasema anaitwa Munira, akafurahi sana na kusema kuwa nafaa sana na amefurahi sana kukutana na mimi. Sikutaka kuopoteza nafasi hiyo nilimwambia kuwa tunaweza kuwa wote usiku ule? akasema mbona mapema sana nikasema kwa sababu amenivutia sana, akaongea kwa madaha na kusema amekubali na kwa sababu ya binti yule nilisahau yote na kumwambia tuondoke twende tukaongelee guest house akakubali na tukaondoka saa ile ilie na kupanda gari za airport na tukashukia mkunazini na kutafuta gest tulipata na nikaalipia na tukaingia chumbani na lengo langu japokua nililipia chumba hadi asubuhi lakini nilitaka tu tufanye mapenzi na niondoke kuwahi foleni ya usiku kule kozi, tukiwa chumbani tulianza michezo ya kimapenzi na akanivulisha nguo zote na mimi nikamvulisha nguo zote isipokua nguo ya ndani na baadae kidogo akashuka kitandani na kusimama huku akinitazama kwa macho makali sana nikaanza kushtuka na ghafla kibanio chake cha nywele kikaachia ghafla na tukio la ajabu sana likatokea nywele zake zikalefuka na kuongezeka zikajaa chumba chote, nikiwa nimejilaza kitandani nilikaa ghafla na baada ya muda kidogo zile nywele zilisinyaa na kuwa za kawaida na kile kibanio kijiweka mahali pake na kubana nywele, Munira akasema kuwa yeye ni jini na anataka tu damu yangu kwani ana njaa sana nilikimbilia mlangoni ghafla huku nikiwa uchi na kujaribu kufungua mlango lakini haukufunguka japokua hatukufunga, akasema siwezi kumtoroka hata siku moja na kwa sababu mimi nimempenda na yeye amependa nyama yangu na damu yangu, nilijikaza lakini nilikua hoi karibu na kuzimia na nikaona njia iliyobaki ni kupiga kele ili watu waje kunisaidia na nilipopiga kele sauti haikwenda kokote maana nilipanua mdogo kwa nguvu zangu zote lakini sauti iliyotoka ni kama namng'ong'eza mtu kiukweli nikikua kama nimechanganyikiwa na niliposhidwa zoezi hilo niliwaza kuwa njia iliyobaki ni kulibembeleza tu lile jini na nilipoliangalia nilikuta linakwato miguuni na miguu ina manyoya kama mbuzi na meno limetoa na kuwa marefu zaidi ya rula ya kupigia mistari, Hakuwa tena yule msichana mrembo munira ambaye nilimpenda sana kwa muda mfupi, Nilimwambia yule jini anibadilishie adhabu akakataa na nilijikuta naomba maombi kwa MUNGU anihurumie na ajabu kama dakika 5 zilizofuata mlango uligogwa na ghafla lile jini likawa Munira yule wa beach na kwa sababu ya mlango kuendelea kugongwa yule jini alienda kufungua na mimi muda huo nikaanza kuvaa nguo kiaskari yaani nusu dakika nimeshavaa zote, Alikua ni dada wa mapokezi akileta chakula chipsi mayai na  na soda na munira kwa ujanja akasimama katikati ya mlango na kuanza kusema sisi hatukuagiza chochote na muda huo huo nikwamwambia yule dada aingie ndani maana kuna kitu nataka kumtuma akaja na alipokaribia tu nikatoka ghafla na kumwaga kile chakula chote huku nikisema kuwa yule dada sio mtu ni jini yule dada mhudumu naye akaakimbia na sikujua kilichoendelea ila nadhani yule jini alipotea muda huohuo maana nilipofika tu nje nilimkuta akinisubiri na kuniambia sina ujanja wa kumtoroka na kwasababu ilikua ni barabarani na watu wengi wanapita nilipiga kelele na kusema jamani niokoeni na vijana fulani waliokua wanapita mmoja wao akasema wewe umekua chizi yaani unaongea peke yako niliondoka kwa kukimbia kama mita 100  na kupanda gari ambayo ilinipekeka hado kambini na nilipofika tu kambini nilimwona tena yule jini na akaniambia kuwa kuniua lazima anaiue tu tena usiku uleule nilipiga tena kele na askari wenzangu wakaanza kucheka sana wakisema nimepandisha mashetani na nikawaelezea kuwa sijapandisha chochote ila ni hali halisi na nikawasimulia mwanzo wa tukio hadi mwisho na usiku huo sikulala maana usiku wa saa 7 nilimwona tena yule munira jini na nikapiga kelele na wenzangu kwa hasira wakasema nisiwasumbue lakini mmoja wao ambaye ameokoka akaniambia namhitaji YESU ili niwe huru. Kwa sababu ya shida nilimwambia niko tayari kuokoka kuanzia sekunde ile, akasema kuwa wao wana kundi lao la maombi hapo kozi ambalo ni kundi la waliookoka kutoka makanisa mbalimbali na huwa wana ratiba ya maombi hivyo muda ukifika atanijurisha ili twende wote na muda huo akaniombea ulinzi wa MUNGU. Muda wa maombi ulipofika tulikwenda na niliombewa na wakati wa maombezi ikasikika sauti kuwa ipo siku watanipata tu. lakini namshukuru MUNGU sana maana nilipona tangu saa ile na nimeendelea na wokovu hadi leo na hakuna chochote walichofanya. Nampenda YESU na namshukuru sana kwa kuniponya na kuniokoka pia kuniepusha na mabaya yale. MUNGU akubariki sana ndugu mtumishi wa MUNGU.

SOURCE: Miasha ya Ushindi