Tuesday, July 11, 2017

SOMO #2. ADAMU NA HAWA

SOMO #2. ADAMU NA HAWA

Andiko Kuu- Mwanzo sura ya 3 yote.
  1.       ANGUKO (Kabla ya Yesu)
1.       Kila kilichoumbwa kilikuwa kikamilifu-Mwanzo 1:3
·         Anga - Jua, mwezi, nyota, sayari, mawingu nk
·         Dunia – Mimea, wanyama,miamba, madini nk
·         Bahari – Samaki wakubwa kwa Wadogo nk
2.       Mungu akaumba Mtu (Adam na Hawa)-Mwanzo 1:26
·         Walimuumba kwa MFANO wao na SURA yao
·         Ili Mtu awe - Mwenye HAKI, MTAKATIFU na MTUKUFU
3.       Dhumuni Kuu la Mungu kumuumba Mtu
·         Wawe na MAHUSIANO
·         Kwamba “Mungu awe Mungu wao na Watu wawe Watu wake”
4.       Adam na Hawa
·         Wanafanya DHAMBI kwani WALIMUAMINI na KUMTII Shetani kuliko Mungu
·         Matokeo ya Dhambi ni :- Kuvunjika kwa Mahusiano, Mtu alipoteza (Haki, Utakatifu na Utukufu), mwishowe AKAFUKUZWA-Mwanzo 3:24
·         Mtu akawa MTUMWA wa Dhambi, akawa (Anaona AIBU, UCHI, ANAJIFICHA)
5.       Njia ya Adam ya KUJISITIRI NA KUJIPATANISHA
·         Walidhani wangejisitiri kwenye vichaka
·         Walidhani wangeendeleza Mahusiano kwa upatanisho wa majani (Eproni)
·         Mungu anawakataa wao na njia zao zote walizobuni kwa laana-Mwanzo 3:1-3,16-19
6.       Njia ya Mungu ya KUSITIRI NA KUPATANA
·         Kondoo asiye na Hatia ANAUAWA – Ili Damu yake ifanye UPATANISHO na ngozi yake IWASITIRI na achukue adhabu ya Mtu. Alikuwa kama MWOKOZI- Mwanzo 3:20
·         Kwa kufa kwa Kondoo, Dhambi ILIFUNIKWA na HAIKUFUTWA, hivyo UREJESHO haukuwa kamili na Mahusiano yaliendelea NJE ya Bustani ya EDENI (MASKANI ya Mungu na Mtu)
7.       Mungu anatoa AHADI
·         Mungu alimpenda sana Adam ingawa alikuwa ameshaingiwa na dosari, sasa alikuwa na asili mbili (Asili ya Mungu na Shetani), na Mungu alijua Kondoo hawezi KUFUTA dhambi, na hizi Asili mbili zimeingia kwenye vizazi vyote vya Adam-50% kwa 50%
·         Mungu akatoa AHADI kwamba angelikuja MKOMBOZI afe badala yao ili Dhambi zao ZIFUTWE-Isaya 7:14,9:6-7, Imanueli maana yake ni Mungu pamoja nasi.
·         Lakini Kabla hajaja KRISTO ilitakiwa KAFARA iendelee kutolewa kila mwaka ili Dhambi ziendelee KUFUNIKWA na sio KUFUTWA mpaka itakapotolewa Kafara KAMILIFU, isiyo na WAA, wala ILA, au KUNYANZI – Kutoka 30:10


   2.       AGANO JIPYA (Wakati wa Yesu)
1.       Yesu KONDOO wa Mungu amekuja-Yohana 1:29,36
·         Kama Mungu alivyotoa Kondoo wakati wa Adam, ndivyo alivyotoa tena kwa ajili y a vizazi vyote vya Adam, tofauti ya kondoo huyu ni KUFUTA Dhambi zote.
·         Yesu ni Kondoo mkamilifu aliyeahidiwa. Fidia yake INATOSHEREZA malipo yote kwani UHAI wake unathamani kuliko chochote-Marko 14:24
·         Yesu ni Mwokozi HALISI sio kama Kondoo aliyefunika Dhambi- Luka 2:11
2.       Mungu Anamkataa Yesu
·         Kama Mungu alivyo MFUKUZA Adamu-Mwanzo 3:24, ndivyo alivyo MUACHA Yesu kwa sababu alikuja afe Badala ya Uzao wa Adam-Marko 15:34, Yohana 19:28.
·         Hivyo Yesu alikataliwa, na akaenda kuzimu ambapo angetakiwa kwenda Mwanadamu aliyeasi, lakini akaenda badala yake.

   3.       NYAKATI ZETU-mwaka 2017 (Baada ya Yesu )
1.       ASILI ya Adam na Yesu-1Wakorintho 15:21-22
·         Tunachukua Asili, sura na Chapa za Adam kwasababu tulizaliwa toka viunoni mwake, Adamu ni wa Chini na sisi ni wa Chini, Adam wa Udongo na sisi ni wa Udongo.
·         Habari njema ni kwamba Tukimwamini Mungu alichokifanya kwa ajili yetu kupitia Yesu, tunapokea ASILI mpya ya Yesu. Yesu alitoka juu, Yesu ni Roho inayohuisha, ndivyo tutakavyokuwa – 1 Wakorintho 15:45-49
2.       DAMU ya Yesu
·         Inasitiri (Covering), hivyo hutaona Aibu wala hutajificha tena-Warumi 4:7-8
·         Inatufanyia UPATANISHO kati ya Sisi na Mungu- Efeso 2:16
·         Kama hujui Damu ya Yesu inachofanya mpaka usamehewe, ndio inaitwa Imani. Unaamini vidonge vitakusaidia ingawa hujui vinafanyaje, ndio inaitwa Imani. Muamini Mungu kuwa anasamehe watu kupitiaa Damu ya Mtoto wake Yesu.


      4    HITIMISHO
CHUKUA HATUA-Warumi 10:9-10
LEO HII, MUDA HUU - 2Wakorintho 2:2-Ukimwamini Mungu alichokifanya kwa ajili yetu kupitia Yesu;- utasamehewa Dhambi, Utarejeshwa,Utasitiriwa, utapatanishwa, utarudishiwa (Haki, utakatifu na Utukufu), hutakuwa mtumwa tena wa Dhambi,na utakuwa na MAHUSIANO na Mungu tena.



By
 APOSTLE  ELIYA SIMON
THE EPANGELIA CHURCH
MAKULU-DODOMA MJINI
0753 011 774


No comments:

Post a Comment