Thursday, January 4, 2018

SIRI YA DAMU YA YESU(THE JESUS BLOOD MYSTERY)

Na Asafu Robert Maziku


Shalom
Kwa mtu mwenye akili timamu naelewa alishawahi kujiuliza kwanini ukitamka jina la YESU kunatokea mrejesho usio wa kawaida.

Hapo kuna mambo mawili kwa pamoja.
A) Jina
B) Damu

Kila jina ulijualo huwa lina nguvu nyuma yake. Nguvu hio inabebwa na asili ya jina, mfano jina Asafu/ Emmanuel, Shida, Eliya au lolote huwa lina nguvu kutokana na asili. Ninapo sema asili namaanisha NANI AMELIITA na KWANINI AMEKUITA. Hii ndipo inaweza kutofautisha nguvu ya jina la watu wawili tofauti lakini jina Moja. Mfano kuna mtu anaweza kuitwa Emmanuel na Babu yake kwasababu kuna Rafiki yake anayempenda sana anaitwa hivyo, Pia mwingine anaweza kumuita Emmanuel sababu ya Kufunuliwa na Roho mtakatifu. Watu hao wataitwa wote Emmanuel lakini kilamtu na Nguvu yake.

DAMU
Damu yoyote uijuavyo huwa imebeba uhai, Pia hunena. Damu ya YESU ni tofauti kidogo na damu uzijuazo kwa sababu zifiatazo, kwanza ni Damu ya Mungu mwenyewe.

Ili binadamu au mnyama yeyote awe anaishi ni lazima awe anaishi na mchanganyiko wa damu kutoka kwa mama na Baba. Ili damu hizo zimkamilishe binadamu ni lazima liwepo tendo la ndoa.

Damu ya Yesu haina mchanganyiko kati ya Baba na Mama kwani hakuna uwepo wa Tendo la ndoa Bali Uwepo kwa Uwezo wa Mungu mwenyewe.

IKIWA KILA DAMU UIJUAVYO INA UHAI NA INANENA VIPI DAMU YA MUNGU MWENYEWE. Kwakupitia damu ya Yesu inenayo mema kwa mwanadamu mapepo yanatetemeka.

HIVYO BASI,
JINA + DAMU YA YESU inapatikana nguvu ya ajabu iwezayo kutikisa ufalme wa giza......

MWAKA 2018 TUTASHINDA KWA DAMU YA YESU                                               0653340950

No comments:

Post a Comment