Thursday, October 31, 2013

SIRI



HII NI SIRI
By Apostle Eliya


YALIYOMO

1. UTANGULIZI

2. SIRI

3. HITIMISHO



LENGO LA SOMO

- Kufunua Siri iliyofichika

-Kuonyesha umuhimu wa kubadili vipaumbele vyetu





ANDIKO KUU ;- KOLOSAI 1:26 “Siri ile iliyofichwa tangu zamani zote na tangu vizazi vyote,bali sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake”



1.UTANGULIZI


-Ninapoangalia mimea, wanyama, sayari, mazingira na ulimwengu kwaujumla ninagundua kwa hakika kuna kitu kinapungua, kuna siri imejificha.



-Hapa ninapoandika haya mafundisho kuna siri nyingi zimenizunguka, hata hapo unaposoma haya mafundisho ya Apostle Eliya, kuna siri nyingi zimekuzunguka. Hapo ulipo unaweza kuingia katika Bustani ya Edeni ambayo Adam na Hawa walifukuzwa miaka 6000 iliyopita. Sasa twende wote tukagundue hii siri……..



2. SIRI


- Najua watu wengi hawajui kilichotokea katika bustani ya Edeni wakati wa Adam na Hawa, wana Theolojia wamejaribu kutengenezea somo ailimradi watengeneze mtaala, lakini wameshindwa kufunua siri iliyokuwa imejificha. Hata hivyo Theolojia sii ya Muhimu sana. Asili ya Biblia ni Rohoni, ukiingia rohoni utaigundua, kwahiyo hatuwategemei wana theolojia kutuchambulia kila kitu, Hapana.—2 Petro 1:21



a).Bustani ya Edeni – NWANZO 2:8-9


- Bustani ya Edeni ni bustani ambayo ndani yake kulikuwa na bustani nyingine ndogo.



- Kinachofanya wapendwa wengi wasielewe hizi sura za mwanzo kwasababu hizi sura za mwanzo zinachanganya matukio ya kimwili na kiroho. Mungu aliumba Dunia na vitu vyote kwa siku sita, siku ya saba akapumzika, cha ajabu siku hii ya pumnziko ndo aliamua apande bustani. Hii bustani ilikuwa niya kiroho na vyote vilivyochipushwa vilikuwa ni alama za rohoni.



- Kitu cha muhimu katika hadithi ya Bustani ya Edeni ni miti iliyokuwa imepandwa, kulikuwa na miti mitatu ; 1. Mti unaotamanika kwa macho na unaofaa kuliwa, 2. Mti wa uzima na 3.Mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Miti hii mitatu pamoja na matunda yake yote niya kiroho. Mungu aliwaambie matunda ya mti wa kwanza na wapili wanaruhusiwa kula ila matunda ya mti wa tatu hawakuruhusiwa kula.



-Mti wa Kwanza ni Roho Mtakatifu, na mti wa pili ni Yesu na mti wa tatu Shetani. Hii bustani ambayo ni mbingu ya pili tulipewa wanadamu kuimiliki, kwahiyo Dunia pamoja na mbingu ya pili(ulimwengu wa kiroho) ilikuwa ni mali ya Adam na Hawa, kwa kule kuasi kwao wakapoteza haki ya kumiliki ulimwengu wa kiroho pamoja na huu ulimwengu, vyote vikawa chini ya Shetani, lakini ile bustani ndogo ndani ya Edeni haikuwa chini ya Shetani kwasababu ilifungwa, ingawa ipo ndani ya Edeni.



b).Adam na Hawa


- Waliumbwa katika ulimwengu huu wa mwili – Mwanzo 2:7

Pumnzi aliwapulizia ilikuwa ni Uhai(uwepo wa Mungu), namaanisha Roho Mt,hii Roho ilitoka baada ya uasi na ilirudi rasmi wakati wa Yesu—Yohana 20:22, ndio maana waliweza kuwekwa katika ulimwengu wa kiroho(Edeni), shetani alimuingia nyoka akamdanganya Hawa na hatimaye Adam akashawishika. Matokeo walifukuzwa nnje toka Bustani ya ndani ya Edeni, na pia walifukuzwa ndani ya Edeni, yale makalipio aliyoyatoa Mungu yalikuwa katika ulimwengu wa kimwili. Mwanzo 3:16-19



-Kwanini walifukuzwa ?

Tayari walishafanya Dhambi kilichotakiwa kufuata ni kutubu na mwisho kula matunda ya ile miti miwili, lakini hiyo toba haikutakiwa ifanyike kwa mdomo, hapana, lilitakiwa jambo lifanyike katika ulimwengu wa kimwili, lazima damu imwagike. Sasa mwanadamu hakujua kuwa amefanya kosa ambalo lina GHARAMA NYINGI na KUBWA za kulipa. Unadhani walikula vipi tunda ?



c).Kurudi Tena katika Bustani ya Edeni.


- Kikwazo cha Adam na Hawa cha kutokuruhusiwa kuingia tena katika Bustani ya Edeni ni Dhambi ambayo malipo yake hakuna mwanadamu ambaye angeweza kulipa, sasa Yesu ameshalipa, nini kilichobaki ? Kumbe hapo ulipo unaweza kuingia tena katika Bustani ya Edeni, najua huwezi kuamini lakini kile kikwazo kimeondolewa. Kuingia tena katika ulimwengu wa kiroho ni haki yako, hapo ulipo upo karibu sana na Bustani ya Edeni, tatizo ni nini ? umefumbwa macho – Efeso 1:18



d).Umuhimu wa Kuingia Bustani ya Edeni.


- Siri za kila mwanadamu unaweza ukazigundua kama utaingia bustani ya Edeni, manabii wote Mungu aliwapa neema ya kuingia katika ulimwengu wa kiroho bila wale Malaika walinzi kuwasumbua – Ezekieli 37:1-2. Henoki alitumia Muda wake mwingi kuwa katika Bustani ya Edeni ndio maana Mungu akamwambia baki hukuhuku—Mwa 5:24, vipi kuhusu Nabii Eliya Mtishibi ?—2 Wafalme 2:11, wote hawa wapo katika Edeni wanakula good-time. Mtume Paulo aliweza kuperuzi ulimwengu wa kiroho, Stefano wakati wanampiga mawe aliweza kuperuzi ulimwengu wa kiroho – Mdo 7:55, Yesu aliwaambia wananfunzi wake nilimuona shetani akianguka toka juu, wewe unadhani Yesu alimuonaje shetani pasipokuwa alikuwa katika ulimwengu wa kiroho ? Watu wengi unaowasoma katika Biblia waliweza kuingia katika ulimwengu wa kiroho na kurudi katika ulimwengu wa kimwili, nikama vile kufumba na kufumbua macho.—Marko 9:4



-  Huu ulimwengu tunaouishi, haukutengenezwa ilitujifunze mambo yaliyomo, HAPANA, tulipaswa kuwa tunajua mambo yote bila kufundishwa kwasababu siri zote zimefichwa katika Edeni. Ndiyo maana mimi nasema huu mpango wa shule sio kwa ajili yakukuelimisha, bali kukupotezea muda ili usijue unapotakiwa kuwepo. Huu ulimwengu na mambo yote yaliyomo ni rahisi kuyafahamu ukiwa rohoni, lakini ukiwa mwilini itakughalimu sana, kwasababu haukutengenezwa kwa mtu wa mwilini, ndio maana uchunguzi mmoja wa kisayansi unaweza ukachukua muda mwingi na mapesa mengi. Ngoja nikuulize, mfalme dawa ya kumtibu mfalme Hezekia, nabii Isaya aliisomea wapi ?



-Ngoja nikushitue kidogo ; Wanasayansi wanasema kipenyo cha Ulimwengu ni Maili 93 bilioni, ukipita katikati ya hiki kipenyo kwa mwendo kasi wa mwanga itakuchukua miaka 28 Bilioni kumaliza kipenyo cha ulimwengu, unajifunza nini hapa? Kama umefunguka kimawazo utagundua mambo yanayoendelea ulimwenguni ni juu ya akili za asili za mwanadamu wa kawaida. Kila mbegu unayoiona imetengenezwa kwa namna ya ajabu na huwezi kugundua kwa macho yako viwango wa kabohaidreti, protini, fati na nguvu iliyomo ndani ya kila mbegu, na kuichunguza mbegu moja inaweza ikakugharimu muda na gharama,sasa kuna mbegu mabilioni. Vipepeo unaowaona wapo aina chungu nzima, hujaingia kwenye miti na matunda pamoja na elimu ya unajimu. Ngoja nikwambie, kuna Galaksi Mabilioni katika huu ulimwengu wetu, kila galaksi ina nyota karibia Bilioni 100. Hii Dunia yetu ikiingizwa ndani ya jua, zitatakiwa Dunia karibia Milioni moja ili upate ukubwa wa Jua, umbali wa kutoka hapo ulipokaa mpaka kwenye  Jua ni mabilioni ya maili. Kwavipimo hivi, nani aliumbiwa huu ulimwengu ? hata akili zetu haziwezi kufikiri ? ndomaana nikasema kuna siri imefichika.



- Waulimwengu


Waulimwengu ni watumishi wa shetani wanaofanyakazi kwa jina la serikali, makampuni, viwanda, taasisi, mashirika. Amini au usiamini shetani anajua ule uwezo ambao Mungu alituumbia na tukaaupoteza na kisha akaturudishia tena, hataki tutambue haya mambo ndiomaana anajaribu kutupotezea muda kwa mtindo wa AJIRA, ajira ni kifungo kimojawapo kizuri sana, Mchakato wa elimu pamoja na mitaala yake pia ni kifungo. Daktari mmoja alisema alichukua miaka 40 kumchunguza nyani,hebu ona !! huku sinikupoteza muda !!, haya ndio madhara tunayoyapata kwa ile dhambi ya asili na kukataa kuingia katika bustani ya Edeni. Fanya urudi Bustanini. Ndio maana ukisoma Biblia vizuri hukuti hata sehemu moja Mungu akiwaambie Waizraeli sumbukieni maisha, anajua nini tulichokipoteza na hakirudi kwa kufanya majaribio mengi ya kisayansi, siku zote aliwaambia mkitii mtakuwa watu bora Duniani. Tatizo liko rohoni.—TORAT 7:14



e).Mapepo katika ulimwengu wa kiroho.


-Malaika walioasi wote walitupwa kuzimu, lakini muhura wao bado haujafika wa kufungwa kwahiyo wanatumia muda mwingi kuwa katika ulimwengu wetu na ule tulioupoteza wa kiroho, mipango mingi hupangwa huko, wala hatuoni ndio maana wanatutesa. Kama tungekuwa na uwezo wa kurudi Bustanini, tungeweza kufukuzana nao na kuwakamata na kuwapiga kwasababu mwendokasi wao sio mkali ukilinganisha na mwendokasi wetu wa mawazo, kama roho zetu zingeweza kuingia ulimwengu wa kiroho tungeweza kutoka sayari moja na kwenda nyingine kwa sekunde, kama Pepo limejificha nyuma ya sayari ya Pluto ningeweza kwenda mara moja na kumkamata na kumtupa kuzimu tena. Kumbuka Edeni alipewa Mwanadamu sio Shetani.



-Kwakweli tulipoteza kitu cha muhimu sana, macho yetu ya kiroho yalifungwa. Mpaka muda huu ninaoongea wanadamu hawajui umuhimu wa kurudi tena katika Bustani ya Edeni, tumeshazoelea shida, ndio maana hatuogopi kufanya dhambi, kumbe kila dhambi tunayoifanya inatufumba macho ya kiroho, watoto wadogo wanahuo uwezo kuingia katika Bustani nzuri ya Edeni lakini anapokuwa na kuanza kufanya dhambi macho yake yanafumbwa, maana yake anafukuzwa katika bustani,sasa kurudi tena nikasheshe.



3.HITIMISHO


-Kama hujakubaliana na mimi, fanya uchunguzi wa kila kitu duniani, kama utashindwa haimaanishi wewe huna akili au muda wako wa maisha ni mafupi, HAPANA, badala yak e nikwamba ulimwengu huu wa mwili uliumbwa kwa ajili ya mtu wa kiroho. Ugumu upo kwasababu tunataka tuugundue kwa namna ya kimwili.



-Vitabu vya siri za huu ulimwengu viliachwa katika bustani ya Edeni, tafadhari turudi tukasome tufurahie maisha. Lakini, tutaingiaje Bustanini wakati kuna Malaika walinzi ?—Mwanzo 3:24.





……………….….THE BEST HAS COME…………………

Wednesday, October 30, 2013

AMANI



Kuna makundi mawili ya Amani: nayo ni

(A) Amani itokanayo na ulimwengu

(B) Amani itokanayo na Yesu Kristo.(Amani ya Kristo)

YOHANA 14:27 > Amani nawaachieni, Amani yangu nawapa, niwapavyo mimi sivyo ulimwengu utoavyo.

Ukiangalia kwa Makini katika Mstari huu utagundua kwamba Yesu anatoa Amani, na ulimwengu nao unatoa Amani, lakini Amani hizi ni tofauti kabisa.

Atupavyo Yesu, sivyo Ulimwengu utoavyo.

Maanayake ni kwamba : Amani aitoayo Yesu siyo kama Amani itolewayo na ulimwengu huu.

Ifuatayo ni tofautu baina ya makundi haya mawili ya Aman

(A)= Amani itokanayo na Ulimwengu.

Kuna aina mbili za Amani zitokanazo na Ulimwengu

1, Amani ya binaadamu iliyo sawa na njia za ulimwengu

2, Amani ya shetani mkuu wa ulimwengu

1- AMANANI YA KIBINAADAMU ILIYO SAWA NA NJIA ZA ULIMWENGU

Biblia inatuambia kwamba hatupaswi kuifuata Amani ya namna hii ya kibinaadamu

TORATI 23:6 = usifuate Amani yao, wala heri ya siku zako zote, milele

Amani ya kibinaadamu ni Amani anayokuwanayo mtu kutokana na kupenda kitu anacho chagua kukifanya au kukitenda kutokana na njia za kawaida za ulimwengu

Mtu yeyote anaweza kuwanayo Amani hii hata kama haja okoka

Mfano -:
Mtu amekaa muda mlefu bila kazi, na akaletewa taharifa ya nafasi ya kazi mahari furani , mtu yeyote katika mazingira hayo ni lazima atakuwa mwenye Amani, na atakwenda haraka kwenye kazi hiyo. Hii ni amani ya kawaida kwa kila mtu wa ulimwengu huu

=Mtu aliyekosa kitu furani kwa muda mlefu, akija kupata kitu hicho ni lazima atakuwa mwenye Amani

=Mtu akipata mchumba anaye mpenda, ni lazima atakuwa ni mwenye Amani

=Wanandoa waliotafuta mtoto kwa muda mrefu , siku wakipata mtoto ni lazima watakuwa wenye Amani

=Mlevi mwenye kiu, au hamu ya Pombe, akipata pombe ni lazima atakuwa mwenye Amani, kadharika na mtu wa sigara naye vivyn hivyo.

Hizi zote ni amani za kawaida zitokanazo na ulimwengu huu.

2= Aman ya shetani mkuu wa ulimwengu.

Hii ni Amani anayokuwa nayo mtu anayeishi katika dhambi, anafanya dhambi na kuenenda kinyume na Neno la Mungu lakini yeye anaitetea dhambi hiyo na kusema yeye ana Amani katika kuifanya dhambi hiyo, na hii sio Amani ya Kristo

2WAFALME 9:22 = ikawa Yoramu alipomuona Yehu, akasema, Je, ni Amani yehu? Akajibu, Amani gani maadamu uzinzi wa mama yako Yezeberi na Uchawi wake ni mwingi?

TORATI 29:19-21 = ikiwa msikiapo maneno ya laana hii, ajibarikiye mtu huyo moyoni mwake na kusema nitakuwa katika Amani nijapotenda katika upote wa moyo wangu kwa kuziangamiza mbichi na kavu, Bwana hata msamehe mtu huyo, lakini wakati hasira ya Bwana na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itakuwa juu yake, na Bwana atalifuta jina lake chini ya mbingu......

MITHALI 23:20 = Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo

mtu mlevi huwa na amani moyoni mwake, na Amani hiyo ni amani itokanayo na mkuu wa pepo (ibilisi) kwamaana maandiko yanasema ,, Walevi hawataurithi ufalme wa mbinguni =1wakoritho 6:9-10,

Amani ya shetani ni kuona mtu anaishi maisha ya dhambi siku zote za maisha yake hapa duniani,

(B) AMANI ITOKANAYO NA KRISTO (Amani ya Kristo)

=Amani ya Kristo inayoamua mioyoni mwetu hupatikana ndani ya Kristo, Maana yake ni kwamba, Amani ya Kristo hupatikana katika Utakatifu wa Kristo
=Katika mapenzi yake,
=katika Neno lake,
=katika mpango wa Mungu

YOHANA 16:33a =Hayo nimewaambia mpate kuwa na Amani ndani yangu.

AMANI yeyote ambayo siyo Amani ndani ya Yesu, hiyo ni Amani ya Ulimwengu.
Amani ndani ya Yesu ni Amani ndani ya Neno la Mungu, Yesu Kristo ndiye Neno (YOHANA 1:1-)

Amani yeyote iliyo nje ya Neno la Mungu hiyo ni Amani ya shetani mkuu wa ulimwengu.

Amani ya Kristo ni ile inayopatikana baada ya kumuomba Mungu juu ya jambo furani na kupokea kile ulichotarajia kupokea.

MUNGU AKUBARIKI

 .. .usikose SOMO lijalo, litakuwa na kichwa cha habari kiitwacho ,,IMANI,, ahsante.

Monday, October 28, 2013

WITO NA UTUMISHI




WITO NA UTUMISHI
By Apostle Eliya

YALIYOMO;
  1. Utangulizi, 2. Wito, 3. Utumishi, 4. Hitimisho

DHUMUNI
-         Kuonyesha njia sahihi ya kuwa Mtumishi
-         Kusaidia mtu ajue Wito wake

ANDIKO KUU;- MATENDO 13:2-3 “…..nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia

1. UTANGULIZI
- Maisha ya Binadamu hayatakuwa na matokeo makamilifu mpaka siku atayogundua Wito wake. Kwanini Mungu alikuumba ? Kwanini upo Duniani ?.

-Kuna aina nyingi za wito, lakini nataka nizungumzie Wito wa Utumishi. Wito hautegemei elimu, fedha, muonekano ,umasikini. Wito ni wewe.

2. WITO
Maana Ya Wito
-Wito ni kitendo cha KUMSIKIA Mungu akitoa majukumu ya utumishi wako.
YEREMIA 1:5, ISAYA 42:6-7
Dhumuni la Wito
- Dhumuni la kuitwa ni Mungu anataka jambo litendeke kwa kupitia wewe, kwahiyo wewe unakuwa ni chombo, kazi yako ni kutii na kutenda.
YEREMIA 51:20-23
a) Naanzanje safari yangu ?
- Mambo mawili ya msingi katika mwanzo wa mchakato;-
     (1) Amini injili (2) Pokea zawadi( Roho Mt)
INJILI- Ni habari njema za Yesu kuhusu msamaha kamili wa dhambi zote, injili ina habari nne kuu;- Maji, Damu, Mwili na Msalaba.-RUMI 1:16, Unaiamini Injili kwa kuliamini JINA LA YESUMdo 4:12, 16:31

ROHO MTAKATIFU Ni zawadi pekee, ni ahadi pekee ya Mungu kwa anaeiamini injili. Huwa anatoa hii zawadi kwa kupitia watumishi aliowatia muhuri. Hakikisha unakuwa na Roho Mt, sio hisia-hisia.
MATENDO 2:38-39,5:32, YOEL 2:32, ISAYA 44:3, YEREMIA 36:27.

b) Mungu anamuitaje mtu ?
- Ingawa Mungu huwa anaita watu kwa namna tofauti lakini anatumia njia moja ya mawasiliano kwa kila muitwaji. Mungu huwasiliana na mwanadamu kwa njia ya sita ya ufahamu ya mtu(fourth dimension), namaanisha Mungu hutumia MAONO, NDOTO, MASIKIO YA NDANI, MACHO YA NDANI.

- Mungu ni Roho, huwa anapenda kuongea na roho aliyompa mwanadamu kwa njia ya Yesu na kupita Roho Mt.WAEBRANIA 1:1-2, YOHANA 10:4,16,27. Naomba nikwambie kwamba Mungu anataka kila mtu aweze kumsikia.

c) Utajuaje Wito wako ?
- Wito wako ni lazima uanzie ndani, Mungu atakuambia wito wako kwa kupitia MAONO(MDO 18:9), NDOTO(1Falme 3:5), KUSIKIA(1 Falme 19:13) NA KUONA KWA UTU WA NDANI(Ufu 1:12), hizi njia nne za mawasilia ninaziita kwa jina moja KUSIKIA au KUWA ROHONI(Ufu 1:10). Kwahiyo ili ujue wito wako utatakiwa USIKIE KWA BIDII. TORATI 28:1, YEREMIA 1:7,9-10. 

- Baada ya kuwa UMESIKIA KWA BIDII wito wako, usikulupuke, subiri uthibitisho, Mungu atamtumia Mtumishi wake ( aliyeamini injili na kupokea Roho Mt)aje akuthibitishie huo wito wako, au ataongea na wewe kwa mara ya pili, mpaka mara ya tatu. MATENDO 9:17-18, 1 SAM 3:8-9

d) Nianze Utumishi?
- Kutokana na ulivyosikia, Mungu atatimiza kile alichokwambia, huwa analiangalia Neno lake, we anza huduma usiogope. ISAYA 55:11.Mungu atatuma watumishi kwa ajili yako, -- Mdo 18:26.

e) Sina Pesa,nitaanzaje huduma ? WALAWI 10:13
- Makuhani walikula matoleo yaliyosongezwa kwa moto, Moto ni Roho Mt, kwahiyo utakapoanza kufanya huduma kwa Moto(Roho Mt), Mungu atakupa matunzo kwa huo moto, Roho Mt. hutatumia nguvu kupata pesa, yeye Mungu atawaamulu watu walete - MITHALI 8:18-21,sababu ni moja --- umefanya kazi kwa Roho Mt MDO 28:8-10, wala hukutumia Moto wa kigeni     WALAWI 10:1

3. UTUMISHI

Wito ni tofauti kwa watumishi lakini misingi ya utumishi ni sawa.
a)Misingi Miwili ya Utumishi sahihi;-- MDO 2:38
- Misingi hii ni (1) Injili na (2) Kutoa vipawa.WAEBRANIA 8:3
Kila mtumishi wa kweli lazima awe nahii misingi, hii misingi ndiyo itakayokupa uelekeo wa wito wako ambao ni tofauti na mwingine.

b) Makuhani na misingi yao.
-Makuhani Agano la kale walikuwa na kazi kuu mbili, kufanya upatanisho na kutoa vipawa WAEBRANIA 8:3. Mtumishi wa Agano jipya anatakiwa kuhubiri ondoleo la dhambi kwa njia ya Yesu(Injili) MARKO 16:15, na kuwezesha watu kupokea Roho Mt YOHANA 20:22

c) Tofauti za Utumishi 

-  Kama uliamini Injili kwa usahihi, ukapokea zawadi kwa usahihi, Mungu hana ujanja, lazima akwambie kwa kupitia Simu yake Roho Mt eneo alilokuitia. Hapa sitaweza kueleza sana kwasababu hii ni siri kati yako na Roho wa Mungu. 1 KORINTHO 12:4-6, WAKOLOSAI 1:26-27

d) Kipi Cha Kuzingatia

- Kama utumishi wako ulianza kwa KUSIKIA Roho Mt, utatakiwa kuendelea kusikia na kutii 100% unachoelekezwa na Roho Mt, hii ndio inaitwa Sabato. Mungu hataki wanaojitolea kumtumikia 1 SAMWEL 16:1, TORATI 18:5, anataka wanaoisikia sauti yake siku zote YEREMIA 18:1-2, Kama Baba yako alikuteua au Jopo la maaskofu waliona unafaa badili mtazamo.

e) Nitamjuaje Mtumishi wa Kweli na Mshirika wa kweli? ,Rahisi sana;

 MTUMISHI --- (1) Anahubiri Injili (2) Anatoa vipawa
MSHIRIKA --- (1)Anaamini Injili  (2) Anapokea Vipawa

Kigezo cha INJILI kinasaidia kuvumbua wanaotumia nguvu za giza na Mawakala wa shetani,ukweli ni kwamba hakuna shetani hata mmoja anaeweza kuhubiri injili, hakuna. -- WAGALATIA 1:8, 2 KORINTHO 11:4,Mdo 4:18

Kigezo cha VIPAWA kinasaidia kuvumbua wale waliojiita, wanaosema watatumia elimu zao, kuna walioona maisha magumu wakaona utumishi unalipa. Mtu ambaye Mungu hajamuita hata afanyaje hawezi kuwapa watu zawadi au vipawa ( Roho Mt). -- MATENDO 19:6, 10:44,

f) Kuna Watumishi feki ?
- Ndiyo. 
Ufeki wa watumishi upo wa aina mbili;
(1) Mawakala wa shetani siku zote wanaipinga Injili wanapinga maji ya Yesu,damu ya Yesu,mwili wa Yesu na msalaba wa Yesu.
(2) Watafuta pesa Wanaikubali injili na wanaiamini, tatizo hawajaitwa, matokeo yake wanashindwa kutoa vipawa, mafundisho yao ni pesa, zaka ni amri, wanataka sana heshima, waitwe majina makubwa- baba askofu, watafanya juu chini waonekane njema, wao huwa hawatoi vipawa ni kupokea tu zaka na sadaka.- MATENDO 19:1-3, watumishi hawa mara nyingi wanatumia moto wa kigeni sijui siku ya hukumu itakuwaje !!!!

4. HITIMISHO

- Kuna watu wengi walioanza utumishi bila kujua hizi kanuni, usijali, anza upya kwa kufuata utaratibu hapa chini ;

          a) Tamani/omba Mungu akupe NENO-Isa 44:3, Math 7:11
     b) Tarajia KUSIKIA —Danieli 2:17-19, Habakuki 2:1-2
     c) Amini(believe) utakayo YASIKIA —Mwanzo 15:6
     d) Fanya(Faith)uliyo YASIKIA —Yohana 14:12
     e) Kiri/tamka Imani yako —Warumi 10:10b
     f) Mungu atakutumia —Yeremia 1:12, Isaya 55:11

…………….THE BEST HAS COME…………………

TOFAUTI KATI YA SERIKALI YA MBINGUNI NA DUNIANI (sehemu ya 2)


TOFAUTI KATI YA SERIKALI YA MBINGUNI NA DUNIANI (sehemu ya 2)

 Na Mwinjilisti Gerald Robert



JE SERIKALI ZA DUNIANI ZITAWEZA KUWA NA AMANI YA KUDUMU ?
Serikali za Duniani zinaoneka wazi wazi kwamba zimeshindwa kupata Amani ya Moja kwa moja (Amani ya kudumu)  japokuwa zimekuwa zikiitafuta Amani hiyo kwa gharama kubwa ya pesa  kwaajili ya kuunda vikosi vya kijeshi vya kutafuta Amani, au kuilinda Amani  lakini bila yakuwa na mafanikio yoyote

Upatikanaji wa Amani  kwa serikali za kidunia unakwamishwa na mambo mengi sana, zifutazo ni baadhi ya sababu

1= Viongozi wa Serikali za kidunia  hawapendi kuondoka madarakani kwasababu wao hupenda sana kutumikiwa  na sio kutumika kwaajili ya Raia au watu wanao watawala katika utawala wao

Yesu Kristo alipokuja Duniani alileta mfano mzuri sana  ambao kama viongozi hawa wa kidunia wangeukubali mfano wa Uongozi wake, leo hii Dunia ingekuwa ni sehemu ya Amani na Salama

MARKO 10:45 = kwamaana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa bali kutumika  na kutoa nafsi iwe faida kwa wengine.

2= Utawala wa nchi, Imani za wananchi juu ya mafundisho ya Mungu,

kuna baadhi ya nchi, au Watawala  wamekuwa wakitawala kwa kufuata sheria za Dini,  na ikumbukwe kwamba sheria za Dini huwekwa na wanadamu ambao ni washika Dini   na kuna wakati sheria hizo za Kidini hupingana na sheria za Mungu, mwanadamu anapoenenda kinyume na sheria za Mungu  hapo ndipo matatizo yanapoanzia  (Kumbukumbu la Torati 28:15-64-)


Sasa tuangalie mfano  namna Mungu anavyo penda tuishi kwa kumtii yeye

Mfano ;--

 WARUMI 12:17-21, (Hii ni sura kutoka Kitabu cha Biblia Takatifu) inasema hivi.
,, Msimlipe mtu Ovu kwa Ovu, angalieni yaliyo mema machoni  pa watu wote, kama ya mkini, kwa upande wenu, Mkae katika Amani na watu wote,

Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa, kisasi ni juu yangu mimi, mimi nitalipa, anena Bwana,

Lakini Adui yako akiwa na njaa, mlishe,  akiwa na kiuu, mnyweshe,  maaana ufanyapa hivyo unampalia makaa ya moto kichwani pake,

Usishindwe na Ubaya,  bali Uushinde ubaya kwa wema. (mwisho wa kunukuu)

Hapo tumejionea jinsi mifano hiyo miwili inavyopingana katika katika kupata Amani ya kudumu kwa serikali za duniani

AMANI ITOKAYO JUU MBINGUNI

Dunia nzima ingeweza kuwa na Amani kama watu wote tungekuwa na Upendo wa kweli bila ya kulipizana visasi, na kung'ang'ania Madaraka

YOHANA 14:27
Amani nawaachieni,  amani yangu nawapa, niwapavyo mimi sivyo ulimwengu utoavyo. . . .

Hapa tunaona kwamba, Yesu Kristo kabla ya kuondoka duniani alituachia Amani, na Amani hiyo siyo kama Amani ile ambayo inatolowa na ulimwengu huu kwa kupitia Watawala wa serikali za kidunia.

Kwenye upendo hapo ndipo Amani inapo patikana

YOHANA 13:34
Amri mpya nawapa, Mpendane, kama nilivyo wapenda ninyi, nanyi Mpendane vivyo hivyo.

Kwakuwa Mungu alifahamu kwamba wanadamu tu dhaifu kwa asili yetu. Akatuwekea Amri

YOHANA 15:17
Haya, nawaamuru ninyi mpate kupendana  (rejea Yohana 14:34)

Neno ,,Amuru,, maana yake ni Lazima, sio Ombi,
kwahiyo Upendo sio jambo la hiyari, bali ni Amri kutoka kwa Mungu, ukiidharau Amri ya Mungu, yapo madhara yakayokupata kwa kudharau kwako.

WARUMI 13:10
Pendo halimfanyi jirani Neno baya, basi, pendo ndilo utimilifu wa sheria (ya Mungu)

kwahiyo kutokuwa na upendo baina ya mtu na mtu, au nchi na nchi,  hapo ndipo Amani hutoweka,  kwamaana Upendo hauhesabu mabaya. ( 1wakorinto 13:4-8)

AMANI ITABAKI KWA WATAKATIFU WA MUNGU

ZABURI 16:3
Watakatifu waliopo Duniani ndio walio bora, hao ndio niliopendezwa nao.

Mungu akipendezwa na wewe hawezi mabya yaje kwako, (hata kama ukifikwa na mabaya ni lazima utayashinda) hivyo sikuzote wewe utakuwa ni mwenye Amani, kwakuwa uwepo wa utakuwa pamoja nawe daima  ni kwakuwa Mungu hapendezwi na waovu.

Hata kama nchi itafikwa na mabaya  lakini watu wa Mungu (watakatifu) wao wataendelea kuishi na kuwa na Amani  hiyo ni kwakuwa Watakatifu wa Mungu  hawaishi kwa kuitegemea sana Amani ya ulimwengu huu  bali huishi kwa kulitegemea Neno lake Mungu ambalo li hai, tena ni kweli.

HESABU 23:19
Mungu si mtu,  aseme uongo.

Mungu ni Mungu Mwenyezi, yeye anaweza mambo yote  isipokuwa kusema uongo, naye asema hivi
MARKO 11:24= kwasababu hiyo nawaambia, yo yote myaombayo mkisali aminini yakwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.

. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

Katika somo litakalofuata nitafundisha kuhusu Amani, 

MUNGU AKUBARIKI

Saturday, October 26, 2013

UKWELI KUHUSU ZAKA

ZAKA AGANO JIPYA?

By Apostle Eliya-0756 166 934

YALIYOMO
1.Utangulizi
2.Nani ni Nani
3.Zaka Agano Jipya ?
4.Zaidi Ya Zaka
5.Hitimisho

LENGO LA SOMO
- Kuonyesha nani anayestahili kupokea Zaka
- Kuonyesha uhalali wa Zaka nyakati zetu

ANDIKO KUU ;- MWANZO 14:18-20

1. UTANGULIZI
- Utakumbuka Zaka imezungumziwa sana Agano la Kale,kwahiyo nitakuchukua nikupeleke kwa makuhani na walawi na wana wa Israeli. Ukweli utakaougundua utakushtua, huwezi kuamini.

2. NANI NI NANI
- Nani ni nani maana yake ni nani anapaswa atoe zaka, na nani anapaswa apokee zaka. Kwamujibu wa Mungu, mtu ambaye hana dhambi ndiye aliyestahili kupokea zaka, na mtu yeyote mwenye dhambi alitakiwa atoe zaka, kwa lazima ili uwepo wa Mungu uwe juu yake.

- Mchakato wa zaka ulianza rasmi wakati wa ukuhani, kulikwa na makabila 12, makabila 11 yalipaswa yatoe kwa kabila moja la walawi, na katika kabila la walawi kulikuwa na kundi la makuhani, na katika kundi la makuhani kulikuwa na familia ya kuhani mkuu, na mwisho kuhani mkuu ambaye alikuwa Haruni.TORATI 18:5

►Huduma ya Ondoleo la Dhambi ;- Watu au mtu anayefanya huduma ya Ondoleo la Dhambi ndiye aliyestahili kupokea zaka. Ndiyo maana nikasema asiyekuwa na dhambi ndiye aliyestahili ili awafanyie upatanisho wengine, hivyo ilim’bidi Haruni atoe Ng’ombe peke yake ili angalau awe mtakatifu na wapatanishe wengine. – Walawi 16:11

b) Majukumu ya kuhani
Haya ndio yaliyokuwa majukumu ya kuhani,- Waebrania 8:3
1)kutoa dhabihu (2)kutoa vipawa (zawadi)
-Utagundua utoaji wa zaka unahusiana moja kwa moja na ondoleo la dhambi na kupokea vipawa, mtu mwenye dhambi hakuluhusiwa kupokea zaka wala kutoa vipawa (zawadi). Ni laana kumpa zaka mwenye dhambi.

►Kutoa Dhabihu – Kuhani alikuwa akichukua matoleo kutoka kwa wana wa Israeli na kuyagawanya katika taratibu zake, matoleo mengine yalikuwa yakichomwa, mengine yakitikiswa,mengine yakichinjwa. Lakini kati ya matoleo yote haya, matoleo mengi yalikuwa yakichomwa na yaliyobaki yalikuwa mali ya makuhani, hii desturi ilikuwa ni kila siku asubuhi na jioni, lakini sadaka zilikuwa zikichomwa usiku kucha, moto ulikuwa hauzimiki kwa ajili ya sadaka ya dhambi.WALAWI 6:13

► Kutoa Vipawa – Hii huduma ni muitikio wa Mungu kwa wana wa Israeli,Mungu alikuwa anawapa zawadi kwa kuwa wamejitakasa na wameondolewa dhambi kwa yale matoleo waliyoyatoa.Ndio maana akawaahidi kuwabariki na kuwalinda na alae. MALAKI 3:11

d) Majukumu ya wana wa Israeli
(1) Kutoa zaka zote na kamili sehemu sahihi. MALAKI 3:10
►Sababu za kutoa zaka (1) Wasamehewe dhambi (2) Wapate vipawa (baraka)

-Katika sababu zote mbili utagundua zaka za Israeli ilikuwa ni kwa ajili yao wenyewe. Makuhani wale, washibe ili wawahudumie katik ondoleo la dhambi. Kwakufanya hivyo Mungu akasamehe dhambi na kuwalinda.

3. ZAKA AGANO JIPYA ?
-► Kuhani mkuu Agano jipya ni Yesu, na wana wa Israeli ni kanisa.

a) Majukumu ya kuhani Yesu
1. Kufanya upatanisho na (2. Kutoa Vipawa(zawadi)- Yohan 14:16-17
Majukumu makuu ya ukuhani yesu alishayatimiza yote, alifanya upatanisho—Ebrania 9:12, alishatoa vipawa,zawadi,karama na huduma – Efeso 4:11, katika Agano Jipya, Roho Mt ni zawadi pekee ambayo kuhani anapaswa atoe kwa watu wanaomtolea zaka,— Mathayo 20:22

b) Majukumu ya Kanisa (ktk zaka) ---
(1) Kutoa nafsi kamili – Mathayo 16:26 – Mungu anaithamini nafsi sana.
(2)Kutoa matoleo sehemu sahihi – LUKA 5:14

►Sababu za kutoa zaka
(1) Kupeleka injili. RUMI 10:15
(2) Kumuwezesha Mtumishi aliyepigwa muhuri na Roho Mt.FILP 4:15

Yesu hahitaji kuwezeshwa na zaka zetu na pia Yesu hahitaji zaka zetu ili akampatie Mungu, au ili aendelee kutupatanisha kila mwaka.

4. ZAIDI YA ZAKA
-► Kuhani mkuu Yesu, ametutolea zaka bora kwa Mungu akapaa kwenda mbinguni, majukumu ya kikuhani ambayo Yesu ameliachia kanisa ni mawili; - (1) Kusambaza injili na (2) kuwawezesha watu kupata Roho Mt.
Mtumishi sahihi lazima ajilengesha katika haya majukumu mawili.

a)Kwanini Utoe Zaka ?. Kwaupatanisho alioufanya Yesu unatubidiisha zaidi ya kutoa, Mungu haitaji zaka, anatuhitaji sisi kama tulivyo, anahitaji toleo zaidi ya zaka, ndio maana Mitume walitoa vitu vyote shirika, walijua Mungu anataka miili yao, nafsi,roho na mali zao zote – MATENDO 2:44-47
-Unatakiwa utoe zaka kwasababu umeshindwa kutoa mali zako zote na moyo wako, kwasababu Mungu hataki zaka, anataka kila kitu chako. Kwahiyo Agano Jipya tunatoa zaka kwasababu tumeshindwa kutoa mali zetu zote ukilinganisha na kazi ya upatanisho ya Yesu na kipawa alichotupa cha Roho Mt.

- Kama kutoa zaka ni muhimu, Swali linalokuja, zaka apewe nani ? kwasababu mpokea zaka angestahili kuwa Yesu sasa hayupo !! Wengi wamejifanya watumishi ili wapokee zaka. Toa zaka kwa mtumishi aliye sahihi, utamjuaje mtumishi sahihi ?

b) Wapi utoe zaka ? – mimi nakushauri toa zaka sehemu ambayo wanafanya kazi ya kikuhani aliyoiacha Yesu --- kutoa vipawa (zawadi), ninamaanisha hivi, katoe zaka ulipo pokea Roho Mtakatifu. Dalili ya kujua mtumishi anastahili kupokea zaka ni kuwezesha watu wapokee Roho Mt, hapa haijalishi wito wa mtumishi. Kila mtumishi wa kweli nilazime awe amepigwa muhuri na Roho Mt ili awawezeshe wengine kupokea Roho Mt.

- Wewe kama ni mtumishi usiniambie kwamba huna wito wa kuwa na Roho Mt, anayetofautisha wito ni Roho Mt, hivyo kila mpokea zaka anatakiwa awe na Roho Mt na awezeshe wengine kupokea, yaani huu ndio msingi wa mpokea zaka halali.

► Naomba watu wafundishwe hivi;- Badala ya kuwafundisha kutoa zaka ni Amri, waambiwe kile Yesu alichofanya kuondoa dhambi ili watu watoe zaka kwa moyo wa kuelewa, kwamba wanachokitoa hakiendani na walichofanyiwa.Kwahiyo zaka iwe pale pale ila mtazamo na msukumo ubadirike, wajue bila Yesu, chochote wanachokitoa kisingewakomboa.GALATIA 5:18

5. HITIMISHO
- Tafadhali Wachungaji – kama hujawawezesha washirika wako kupokea ahadi kuu ya Mungu, Roho Mt, hiyo zaka haupokei kihalali, hebu uwe na huruma, wamekuwezesha wewe tu lakini wewe hujawawezesha.

-Tafadhali Waumini – Zaka unayotoa, kama ungempa anayewezesha watu kupokea ahadi kuu ya Mungu, Roho Mt, usingeibiwa, na Mungu angekulinda na alae.

- Soma KUMB TORATI 18:1-5, Kama Mungu amemuita kweli mtumishi, Mungu atakutoshereza, usiwatishie washirika kuwa wasipotoa zaka watakufa, au Mungu atawalaani, sio kweli.

...................................................................THE BEST HAS COM................................................

SOMO LA LAANA ZA FAMILIA




MKUTANO MKUBWA WA INJILI UNAOENDELEA MJINI MOSHI.
TAREHE: 25/10/2013.
SOMO: LAANA ZA FAMILIA
Na Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima

Mch.Kiongozi Josephat Gwajima.


Kuna familia zinaandamwa na matatizo mbalimbali, mfano. matatizo ya kutokuolewa,umasikini au matatizo mengine yanayotokana na laana za familia. Mchungaji Kiongozi alihaidi kuvunja matatizo yote ya kifamilia yanayoletwa na familia,na kusema kuwa leo kuna mambo ambayo anataka kuusemea ukweli.
kuna familia ambazo zinakuwa zipo chini ya laana fulani na hata mtu akipenya anapenya kwa taabu sana.
Sasa tutaangalia siri iliyopo nyuma yake halafu utafunguliwa katika Jina la yesu.

Tukiangalia maandiko

Mwanzo 9:18-25..
18 Wana wa Nuhu waliotoka katika safina, ni Shemu, na Hamu, na Yafethi; na Hamu ndiye baba wa Kanaani.
19 Hawa watatu walikuwa wana wa Nuhu na kwa hao nchi yote ikaenea watu.
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema,Na alaaniwe Kaanani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.

Tukiangalia kitu hiki cha ajabu, Hamu ndiye aliyeona uchi wa babaye lakini anayelaniwa ni mwanaye Kanaani.Hapa tunaanza kujifunza jambo ya kuwa jambo linapotokea kwa wazazi linakwenda kwa watoto,wajukuu na watoto na watoto.

Lakini Kanaani alikuja kuwa na watoto baadae,hebu tuwaone watoto waliozaliwa na Kanaani aliyelaaniwa walikuwa kina nani na maisha yao walikuwaje;

Mwanzo 10:15-19.
15 Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi,
17 na Mhivi, na Mwarki, na Msini,
18 na Mwarvadi, na Msemari, na Mhamathi. Baadaye jamaa za Wakanaani walitawanyikana.
19 Na mpaka wa Wakanaani ulianza kutoka Sidoni kwa njia ya Gerari hata Gaza; tena kwa njia ya Sodoma, na Gomora, na Adma, na Seboimu, hata Lasha.

Ndio haohao watoto ambao wana wa Israeli wakati wanatoka katika nchi ya utumwa, Mungu alimwambia Musa waangamizwe njiani wauawe wote,hii inatupa picha ya ajabu ya kwamba wote waliozaliwa na Kanaani walikuwa na laana na ndio Mungu akamwambia Musa ili wauawe.

Tukiangalia tena maandiko matakaifu

Kitabu cha Kutoka 3:7-8.
7 Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.

Hapa tunaanza kuona kumbe laana zinaweza kutokea katika familia,hivyo inawezekana leo hii una matatizo siyo kwa sababu umetenda dhambi ila ni kwa sababu kuna mambo yalitendwa kwenye familia yenu yankuandama mchana na usiku, hivyo naomba leo unifatilie kwa makini ili tuvunje hizo laana na Baraka yako itakwenda kutokea katika jina la Yesu.

Kitabu cha Kutoka 3:17
“Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali”
Hapa Mungu alikuwa akiongea na wana wa Israeli.Kwa hiyo utaona mojawapo ya alama ya laana ni kunyang’anywa kile kitu ulichokimiliki kwa nguvu zote.

Kitabu cha Mithali 26:2
“Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpigi mtu.”

Kwa hiyo kumbe maana yake ni laana yenye sababu inampiga mtu.
Lakini utaona pia kuwa mambo ya imani nayo yanaweza kwenda familia hata familia.
2Timoteo 1:3-5.
3 Namshukuru Mungu, nimwabuduye kwa dhamiri safi tangu zamani za wazee wangu, kama vile nikukumbukavyo wewe daima, katika kuomba kwangu usiku na mchana.
4 Nami natamani sana kukuona, nikiyakumbuka machozi yako, ili nijae furaha;
5 nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo.

T.A.G KUREJESHA MAADILI




UKOSEFU wa maadili katika jamii madhara yake ni makubwa.

Watu wengi wamekuwa wakilizungumza hilo, lengo likiwa ni kuwashawishi wazazi na walezi wawalee vijana wao katika misingi mema.

Kwa kuliona hilo Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) chini ya Kiongozi Mkuu Mchungaji Dunstan Kanemba limezindua mkakati wa kugeuza mioyo ya watu kwa kueneza Neno la Mungu.

Mkakati huo umefanikiwa ambapo mateja, vibaka, majambazi na mashoga wameamua kubadili tabia zao na kuwa watu wema katika jamii.

Mchungaji Kanemba anasema Magomeni inajulikana ni miongoni mwa maeneo yenye vitendo vya ukosefu wa maadili ambapo biashara za dawa za kulevya, changudoa kuwaibia wanaume wasiowafahamu kwa kutumia mfumo wa kuwawekea dawa za kulevya kwenye vinywaji vyao na kuwaibia kila kitu vimashamiri.

Kwa kuliona hilo, Mchungaji Kanemba amezindua mkakati wa muda mfupi (miezi minne) ili aweze kuwafikia watu kwa injili ya upendo chini ya kaulimbiu ya “Ushuhudiaji wenye shabaha.”

Mkakati huo ulizinduliwa Agosti 4 mwaka huu.

Lengo ni kuwafikia Watanzania bila ubaguzi kwa kuwashirikishia habari njema za upendo wa Mungu.

Anasema kupitia mkakati huo rushwa haitakuwepo, magereza yatakosa wafungwa na uchumi utakua.

“Yanayotokea kama ufisadi, masuala ya rushwa ni matokeo ya jamii kukosa maadili na uzalendo kwa ujumla wake kwani ni aibu kwa Mtanzania yeyote kuomba rushwa kwani ni ukosefu wa maadili uliopitiliza.

“Ukienda nchi zilizoendelea kama Marekani huwezi ukakuta Mmarekani anamuomba rushwa Mmarekani mwenzake,” anasema.

Akieleza mkakati wa kurejesha maadili Mchungaji Kanemba anasema wameanzia katika Tarafa ya Magomeni yenye kata sita za Mzimuni, Magomeni, Ndugumbi, Kigogo, Mburahati na Makurumla.

Tangu mkakati kuzinduliwa, anasema tayari wameshafikia vitongoji vinne ambavyo ni Mzimuni, Magomeni, Ndugumbi na Kigogo.

Anasema njia ambazo wamekuwa wakizitumia ni ushuhudiaji wa mtu mmoja mmoja na mikutano midogo midogo ya mihadhara.

Njia nyingine ni kupitia matangazo kwa kutumia vyombo vya habari na mfumo wa kuonyesha filamu zenye ujumbe wa neno la Mungu.

Anasema mpango huo wa ushuhudiaji wenye shabaha utakuwa wa muda mrefu kwani hawana mpango wa kuishia Magomeni tu bali kufika maeneo mengine.

Akielezea matokeo ambayo wameyapata tangu kampeni hiyo izinduliwe, Mchungaji Kanemba anasema watu bila kujali utofauti wa imani zao wameupokea mkakati vizuri sana.

Kwa sasa anasema vibaka, mateja, mashoga, wachawi na watu waliokuwa wamekata tamaa wengi wamebadili tabia zao na kuamua kumfuata Mungu kiasi kwamba hata kanisa analoliongoza limekuwa dogo kutokana na mwitikio mkubwa.

“Nitumie fursa hii kuwashukuru wananchi wa Magomeni kwa kuupokea mkakati wa ushuhudiaji wenye shabaha, huku tukiunga mkono kampeni ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Said Mwema ya ‘Utii wa Sheria Bila Shuruti’, hivyo kampeni hii ina msaada mkubwa kwa polisi.

“Sisi kama kanisa kazi tunayoifanya ni kubadilisha mioyo ya watu ili waweze kuwa raia wema wanaotii sheria bila shuruti.

“Ndugu mwandishi, hata mimi sikutegemea kama mkakati huu unaweza kuwa na mafanikio kiasi hiki, maana watu ambao tumewafikia ni wale ambao kwa dhati walikuwa kero kwa jamii kutokana na tabia zao kuwa mbaya. Leo hii wamebadilika na wako kanisani wakiendelea kulelewa vyema kiroho.

“Leo hii kuna wanaume waliokuwa mashoga wamebadili tabia na kutangaza hadharani kuwa sasa wameokoka…kwa kweli hata mimi napenda kumshukuru Mungu sana. Kutokana na mwitikio huo imefikia hatua hata IGP kupitia kamanda wake wa Kinondoni ameweza kututia moyo na kuupongeza mkakati huu. Kwa dhati umeweza kuwafikia walengwa waliokuwa wameshindikana kwenye jamii,” anasema.

Anasema wana mpango wa kuwafikia hata vigogo kwa njia ya mikutano, magazeti, redio na runinga ili nao waweze kubadili tabia kwani suala la maadili mema ni la watu wote bila kujali hadhi ya mtu.

Akieleza changamoto zinazowakabili, Mchungaji Kanemba anasema kiukweli watu wameupokea mkakati wao, lakini tatizo linalowakabili ni namna ya kuwawezesha wale ambao wameamua kubadili tabia zao.

Mfano kuna watu walikuwa majambazi, changudoa na mashoga, hivyo anaiomba jamii, serikali na kampuni kuwasaidia fedha ili waweze kuwawezesha watu hao waliobadili tabia zao.

SOURCE: TANZANIA DAIMA 26/10/2013

Friday, October 25, 2013

PICHA YA SIKU

TD JAKES


HII NDIO PICHA YETU YA LEO.

KAFARA YA DAMU










Na: Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima

Somo: Kafara ya Damu


Lengo la somo hili ni kuwatoa wale waliopo mapangoni,mashimoni,uvunguni au waliofichwa mahala popote pale kutokana na kafara ya damu.

Mara nyingi ukisema neno “kafara” watu wanajiuliza kwamba “kwani huyu ni mganga wa kienyeji?”hii inatokana na watu kutopata mafundisho kuhusu mambo haya.

Utaona Neno kafara limeandikwa zaidi ya mara 19 kwenye biblia,na ukisoma biblia utaona kuna watu walitoa kafara za damu kwa ajili ya mafanikio fulani fulani. mfano mfalme wa Moabu ambaye alimtoa mwanae (2wafalme 3:26-27)


Damu ni nini?


Kumbukumbu la torati 12:23

Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na uhai usile pamoja na nyama.

Mambo ya Walawi 17:11

Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.

Mambo ya Walawi 17:14

Kwa maana kuliko huo uhai wa mnyama, hiyo damu yake ni moja na uhai wake; kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Msile damu ya mnyama wa aina yo yote; kwa kuwa uhai wa wanyama wote ni katika hiyo damu yake; atakayeila awaye yote atakatiliwa mbali.

Kwa nini Mungu anazuia kunywa damu?

Mungu anazuia kunywa damu kwa sababu damu ina uhai.
Mwanzo 4:10

Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.


Katika andiko hili tunajifunza mambo yafuatayo;

1. Damu ina sauti

2. Damu inaweza kulia.

3. Mungu anaweza kusikia kilio cha damu


Pia damu inao uwezo wa kumfuata mtu mana kuna uhai katika damu,utaiona hii katika;


Mathayo 27:24

Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe.

Matendo ya Mitume 5:28

Akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu.


AINA ZA DAMU.

A. Damu inayonena mazuri(mema)

B. Damu inayonena mabaya.


A. Damu inayonena mazuri(mema).

Damu ya Yesu ndiyo unayonena mema,Damu ya Yesu inanena mafanikio,kuinuliwa,ushindi,uwezo na mambo yote mema.

Waebrania 12:24

Na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.

B. Damu inayonena mabaya.

Wachawi,waganga wa kienyeji,washirikina nao wana madhabahu zao. Mfano, wachawi wakitaka kuloga huwa wanakutana mahali, na kawaida yao huwa wanakutana kwa vikundi, mfano wachawi wa kibosho,wachawi wa Marangu huwa wanakutana mahali na kumwaga damu,na mahali hapo wanapokutana ndipo madhabahu yao ambapo kuhani wao wa madhabahu ni Shetani.

Kumbuka damu huwa inamwagwa kwa ajili ya madhabahu.

Madhabahu ni nini? Madhabahu ni daraja kutoka ulimwengu wa roho kwenda ulimwengu wa mwili na kutoka ulimwengu wa mwili kwenda ulimwengu war roho.

Madhabahu huwa inaundwa na vitu vifuatavyo;

1) Madhabahu yenyewe

2) Kuhani wa madhabahu

3) Mungu wa madhabahu

4) Nguvu za madhabahu

5) Watu wa madhabahu

Mwanzo 8:20

Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.

Mwanzo 12:7

Bwana akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu Bwana aliyemtokea.

Mwanzo 13:4

Napo ndipo palipokuwa na madhabahu aliyofanya hapo kwanza; naye Abramu akaliitia jina la Bwana hapo.

Thursday, October 24, 2013

ALIYEKUWA FREEMASON KWA MIAKA 14 AOKOKA MOSHI, AONESHA KIDOLE ALICHOKATWA



Aliyekuwa Freemason kwa miaka 14 afunguliwa katika mkutano wa Ufufuo na Uzima unaoendelea Moshi; alikatwa kidole akiwa mdogo kama udhihirisho wa alama yao (devil horns)
alieleza mwenyewe mbele ya waliokuwepo mkutanoni maelfu ya watu wa mkoa wa Kilimanjaro na vitongoji vyake wanaohudhuria mkutano huo katika viwanja vya mashujaa unaoongozwa na mchungaji Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima lenye makao makuu yake Kawe jijini Dar es salaam.


Binti wa kiislamu ambaye aliwekwa ndani ya bahari kwa miaka mingi; alipokea ukombozi wake mara baada ya maombezi. Kule baharini alikuwa ameolewa na jini ambaye alimweka awe malkia wa baharini kwa miaka mingi... Mungu akamrudisha baada ya maombezi na kumpokea Yesu Kristo.

Baadhi ya picha jinsi maelfu ya wakazi wa mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro wanavyohudhuria mkutano huo toka ulipoanza tarehe 20 mwezi huu, unatarajiwa kumalizika siku ya jumapili tarehe 27.


Njia ni moja tu nayo ni YESU, Askofu Gwajima akifundisha mkutanoni


Flora Mbasha na mumewe wapo sambamba na wana Ufufuo na uzima mkoani Kilimanjaro.

SOURCE: GOSPEL KITAA

DINI MPYA YA SHETANI IMEIBUKA MBEYA INAITWA DIMAYO



SHALOM:
 Dini inayoamini katika MUNGU lakini ikiruhusu yale ambayo dini zingine zinapinga imeanzishwa eneo la mji mdogo wa Makongolosi wilayani Chunya mkoani Mbeya,
 Dini hiyo haiamini katika kutoa sadaka bali inasema tunamtolea nani sadaka wakati Vitu vyote tulivyonavyo ni mali ya MUNGU,kwa nini tunampa MUNGU mali zake Mwnyewe.!
Dini hiyo inaruhusu ulevi,uchawi na uzinzi kwa sababu vimeumbwa na MUNGU,Vile vile inaamini hakuna dhambi duniani,Dini hiyo inaitwa DIMAYO, sasa imeanza kuenezwa Mbeya.


Habari hii mwanzo ilinishtua sana mwanzo nilipoipata kutoka katika mtandao wa kijamii ujulikanao kwa jina la Jamii Forum. Ila nikakumbuka kuwa kila sehemu penye neema kubwa ya wokovu pia ndipo shetani hupapigania sana. Kama unaelewa neema ya wokovu iliyopo Nigeria ambako kuna watumishi wakubwa wenye upako wa kila aina kama TB. JOSHUA na wengine ila usisahau Nigeria inasifika pia kwa uchawi.

Wakati Mbeya ikiwa na neema kubwa ya wokovu kwa kutoa wainjilisti, Waimbaji, Wachungaji wengi nchi hii pia ni Mkoa unaosifika kwa matukio ya ajabu ajabu ikiwemo mauaji. Ukiulizwa ni mkoa gani unamakanisa mengi Tanzania huwezi kuacha kuanza na Mbeya.

LENGO LANGU.

TUONAPO MAMBO YA KUMDHIHILISHA SHETANI WAZI WAZI KAMA DINI YA DIMAYO BASI UJUE NEEMA YA WOKOVU NAYO INAZIDI. Hakuna haja ya kushtuka zaidi sana ni kumshukuru Mungu maana anaenda kudhihilika. Tusisahau kuwa endapo Mungu angemlainisha Farao awaruhusu wana wa Israeli kirahisi rahisi basi Tusingejua nguvu zake na maajabu ikiwemo kuitenganisha Bahari kisha kuirudisha. Ni lazima dini kama hizi zije ili watu wazione nguvu na maajabu ya Mungu wa kweli ukitofautisha na DIMAYO.

IMEANDIKWA NA ROBERT MAZIKU 0653340950

Wednesday, October 23, 2013

YESU SI MBUZI -- 2



c) Kuzaliwa Kwa Maji na Roho Mtakatifu

Yohana 3:5, Tito 3:5, Ebrania 10:22, 1 Yohana 5:6,9, Mdo 10:44-48, Hapa ndipo penye siri yote, wengi wanasema tumeshabatizwa kwahiyo hakuna jipya, soma MDO 8:12-17 utawaona wenzako walivyopungukiwa na kitu cha muhimu-----ROHO MT………..….
………………………………..ENDELEA…………………………….
Hapa nitaelezea kwa umakini zaidi, naomba hiki kipengele nikiite MASHAHIDI WATATU, nikimaanisha ROHO MT, MAJI na DAMU --- 1 Yohana 5:6
- Hawa mashahidi watatu ndio wanaotengeneza AGANO JIPYA, labda tujiulize swali, Agano Jipya lilifanyika mto jordani au kalvali, najua wapendw wengi wangejibu kalvali (msalabani), sio kweli. Tunaposema Agano Jipya tunamaanisha Mungu ANACHUKUA DHAMBI(MAJI), kisha anatupa ROHO MT, hili ndilo Agano Jipya. Sasa Damu inakazi gain ? Damu ni USHAHIDI wa Agano lililofanya,kwahiyo Damu yenyewe sio Agano, bali ni KIASHIRIA cha Agano, ni kama vile PETE kwa wanandoa. Ndio maana ROHO MT na MAJI vimetajwa pamoja mara nyingi, na Biblia inapotaja Maji na Damu bila kutaja ROHO MT inajua kwamba ndani ya Maji kuna mgao wa ROHO MT.  ---kutoka 24:7-8, Waebrania 9:16-20
- Naomba niseme hivi, hata ukifunga,ukikesha,uki omba miaka 100 kwa ajili ya kupokea Roho Mt, HUTAPOKEA !!!,kinachofanya mtu apokee Roho Mt ni ile hali yakutokuwa na DHAMBI YA ULIMWENGU ndani ya Moyo wa mwanadamu, na ndio maana tukio la Ubatizo limekuwa likiendana na kupokea Roho Mt,sio Maombi. Haya matukio mawili siku zote yapo sambamba, Mfano;Yesu aliona udhihilisho wa Roho Mt alipomaliza kubatizwa –Mathayo 3:16, Mtume Paulo---ubatizo na kupokea Roho Mt vilienda pamoja—Mdo 9:17-18, soma hapa uone Petro anavyowashauri wanadamu –Mdo 2:38.Kitabu chote cha Matendo ya mitume kimejaa matukio haya mawili---KUMKABIDHI MUNGU DHAMBI na MUNGU KUTOA ROHO MT.
- Wachungaji wengi wamewaaminisha washirika wao kuwa wana Roho Mt, huo ni uongo,swala la kuwa na Roho Mt sio la Imani, ni uzoefu(you have to experience it), lazima kuwe na dalili, alama zinazoonyesha kuwa wewe una Roho ---ukisoma Efeso 1:13—utagundua Roho Mt ndiye anayempiga mtu MUHURI kuwa amesamehewa Dhambi kwa Maji. Dalili mojawapo rahisi ya kujua mtu amepigwa muhuri ni KUNENA KWA LUGHA---Mdo 10:45-46 – Mungu alimgonga Ibrahimu muhuri kwa namna gani ?--- Kutahiliwa, unaona, nilazima dalili zionekane. Unapojaribu kunena kwa Lugha bila kuongozwa na Roho Mt, utakuwa unafungua njia ya mapepo kukujia.
- Njia sahihi ya kumpokea Roho Mt; Tambua kuwa Mungu anataka aweke Agano na wewe, Agano hilo wewe unatakiwa umkabidhi dhambi zako zote, Mungu atazichukua zote na anakupa zawadi ya Roho Mt. Sasa amini kuwa makabidhiano ya dhambi zako yalifanyika kwa maji, na Yesu akakubali kuzichukua zote kwa kuwekewa mikono na Yohana na kuingia ndani ya maji, ukisha amini hivi nenda ukabatizwe, Mungu atakupa zawadi ya Roho Mt ambaye ndiye anawajibika kukutunza mpaka Yesu atakaporudi tena, baada ya hapo Mungu ataanza kukutazama wewe kwa miwani ya Damu ya Yesu, hatakuhesabia dhambi tena.
3. ONGEZA MTAZAMO
Mathayo 3:11 ‘..…atawabatiza kwa Roho Mt na kwa Moto ’.
a) Ubatizo wa Roho Mt
 Yohana anaongea vitu ambavyo kila mwanadamu angepaswa avitafute sana, kwasababu ndio Agano Jipya. Naomba niseme kwamba Mungu hana mpango na mtu yeyote aliye nnje ya Agano, ili ubatizo wa Roho Mt ufanikiwe inapaswa mtu aamini ondoleo la dhambi na pia awepo mtumishi aliyejaa Roho Mt, hautapokea Roho Mt mpaka yeye anayekuongoza kupokea Roho Mt awe ametiwa muhuri na Yesu,kwasababu jukumu la kubatiza kwa Roho Mt nila Yesu. Kwahiyo sio kila mchungaji anaweza kukufanyia mchakato wa kujazwa na Roho Mt. Soma Mdo 19:1-6 – utaona watu wa Efeso walikuwa wamebatizwa ubatizo wa Yohan lakini hawakuwa na Roho Mt, kwamba aliyewabatiza hakuweza kuwawezesha wapate Roho Mt. Soma pia Mdo 8:12-17 – Samaria walibatizwa lakini hawakupokea Roho Mt mpaka alipokwenda Petro na Yohana. Nataka niseme nini hapa !! imani yako lazima iendane na tendo la kuoshwa lakini ni lazima awepo mtumishi sahihi wakuyafanya hayo yote yawe na maana
b) Ubatizo wa Moto
-Kubatizwa kwa Moto ni kitendo cha Yesu kutufanya sisi tuwe harufu nzuri kwa Mungu, yaani atufurahie—2 korintho 2:14-15, sisi tuliozaliwa mara ya pili ni SADAKA ya kuteketezwa kwa moto, sasa Yesu akiwa kama kuhani anatuchukua sisi na kututeketeza kwa moto ili kumletea Mungu harufu nzuri. Soma Mwanzo 8:20-21, kutoka 29:18, Hesabu 15:3, Kwahiyo Yesu anatutoa kwa Mungu kama sadaka ya kuteketezwa, namaanisha Yesu anatuteketeza kwa Roho Mt. Hili ndilo Agano Jipya, yeyote ambaye hataelewa hapa atakuwa ameukosa ufalme wa Mungu (hataingia mbinguni). Yesu atakapokuja atawanyakuwa wale wenye Roho Mt tu !! Nakusihi sana msomaji wangu, fanya uwezavyo umpate Roho Mt kwasababu AHADI KUU ya Mungu kwa mwanadamu ni Roho Mt, nnje na hapo ni makida-makida
c) Watumishi Feki
- Hawa niwatumishi wanaoanza huduma bila ya luksa ya Yesu(Roho Mt)—Mdo 13:2, wamesababisha madhara makubwa sana kwasababu Mungu haitaji watu wakujitolea kumtumikia, na ndio maana mtembeo wa Roho Mt kwa watumishi wengi sio mzuri, mimi kama mtumishi mmojawapo naomba nikubali hili kosa. Utumishi ambao Roho Mt hajauanzisha, kamwe hatautimiza, samahani kwa kusema hivi;-mkristo ambaye hana Roho Mt, SIO MWANA WA MUNGU.
4. HITIMISHO
-Soma kwa umakini hapa, Agano la Mungu na Wanadamu toka mwanzo na mpaka mwisho wa ulimwengu ni hili, “MIMI NITAKUWA MUNGU WENU, NANYI MTAKUWA WATU WANGU---Ezekiel 36:25-29”, sasa basi, kikwazo kikubwa cha hili Agano kuwepo ni DHAMBI YA ULIMWENGU, sasa Mungu akawa anatafuta namna ya kuiondoa hii Dhambi moja kwa moja ili ATIE ROHO YAKE ndani yetu. Uwepo wa Roho Mt katika maisha ya mtu ndo yanaonyesha mafanikio ya Agano kwasababu Roho hakai sehemu chafu.
- Kwahiyo Yesu amefuta dhambi kwa Maji, Roho Mt akapata nafasi ya kuja Duniani, na Mungu akalinyunyizia hilo Agano kwa DAMU,pale msalabani. Kila wakati Mungu anapotaka amtazame mwanadamu,kwanza ni lazima avae MIWANI (aitazame damu msalabani) ndio amtazame, ndio maana hatatuhesabia hatia tena kwasababu HAIONI, anaona Damu-Damu tu.
-Agano la kale Mungu alishindwa kugawa Roho Mt kwa wote kwasababu dhambi za watu zilikuwa zinafunikwa tu bila kufutwa, lakini agano Jipya kila mtu anayo haki ya kupata Roho Mt kama vigezo na mashart yakizingatiwa
-Yesu sio Mbuzi ila amechukua uhusika wa Mbuzi wa Agano la kale, YESU NI MWANA WA MUNGU, YESU NI BWANA, YESU NI ALFA NA OMEGA,YESU NI MFALME ATATAWALA MILELE YOTE……………………………AMENI……………………………