Friday, June 27, 2014

Mahakama nchini Sudan yamuachia huru Mwanamke aliyetakiwa Kunyongwa kwa kosa la Kubadili Dini.


Wakili wake Elshareef Ali, ameambia BBC kuwa mwanamke huyo aliyekiuka dini kwa kuolewa na mwanamume mkristo aliachiliwa huru Jumatatu.
Meriam na mumewe Daniel siku ya harusi yao.
Meriam ameolewa na mwanamume mkristo na alihukumiwa kifo na mahakama ya kiisilamu kwa kosa la kuasi dini, baada ya kukata kukana kuwa yeye ni mkristo.

Hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya Meriam Ibrahim,ilibatilishwa na mahakama ya rufaa, kwa mujibu wa shirika la habari la Sudan Suna.

Hukumu dhidi yake ilichochea viongozi wa kimataifa walioilaani wakisema inakiuka haki za binadamu.

'Hamu kumuona mkewe'
Mumewe Meriam Daniel Wani, alisema kuwa ana hamu sana kumuona mkewe kwani taarifa hiyo ilitolewa bila yeye mwenyewe kuitarajia.

Ameambia BBC kuwa anataka familia yake kuondoka nchini Sudan haraka iwezekanavyo.
Mume wa Meriam Daniel Wani akiwa amewapakata watoto wake, mdogo kushoto alizaliwa gerezani hivi karibuni.
Wanandoa hao walioana kanisani baada ya kukutana mwaka 2011.
Hukumu ya kifo dhidi ya Meriam Yahia Ibrahim Ishag, ambaye alijifungulia gerezani, ilisababisha gadhabu sana hadi katika ulingo wa kimataifa.

"Tuna furaha sana kuhusu hatua hii ya serikalli na tunaelekea sasa kumchukua,'' alisema wakili wa Bi Meriam Elshareef Ali.
Bwana Ali alisema kuwa Bi Meriam alionyesha ujasiri mkubwa sana wakati huu wa masaibu yaliyomkumba.

''Ni ushindi kwa uhuru wa dini na imani, tunaamini kuwa katika siku za usoni hakuna mtu atakayelazimika kupitia masaibu kama yaliyomkumba Meriam,'' alisema wakili wake.

Babake Meriam alikuwa muisilamu ingawa mamake alikuwa mkristo na Meriam akaamua kuolewa na mwanamume mkristo.
Amekuwa gerezani tangu mwezi Februari pamoja na mwanawe mdogo.

Hata hivyo bwana Ali alisema kuwa hajaona hukumu ya mahakama ya rufaa na kwamba alipokea taarifa hizo kupitia kwa vyombo vya habari. BBC Swahili imeripoti.

ROSE MUHANDO KUZINDUA ALBAMU YAKE YA FACEBOOK AUGUST 3/2014 JIJINI DAR.


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiLVwiVzZK8sRYGobNzbXyWGg6qeZLT3nNvG287nVZXxh-2bPyrrskMamzOYMmTT1oc2j1hjtlNdEY5DWspmYtCG0Vc_Wvg5r4prmtRhcJyoQ0CgDSHayypBxfpIey9Mu1jCRxorSpoYXo/s640/ROSE.jpg
Rose Muhando ndani ya Wololo ambao pia ni wimbo mpya.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari kwenye viwanja vya Karimjee leo wakati alipokua akitangaza Uzinduzi mkubwa wa Albam ya Shikilia Pindo maarufu ka FACEBOOK ya mwimbaji wa muziki wa injili anayevuma, Rose Muhando utakaofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Agosti 3 /2014 jijini Dar es salaam, ambapo amesema baadhi ya mapato yatakwenda kuviwezesha mitaji zaidi ya vituo 10 vya watoto yatima jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua zaidi kwa Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi huo unaoatarajiwa kuwa mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki kwa waimbaji wa muziki wa injili.

Monday, June 23, 2014

SONG: Mateso Sita


TAMASHA LA UIMBAJI NDANI YA FPCT MOROGORO LA FANA

Ilikuwa ni jumapili ya Tarehe 22 mwez wa 6 katika ukumbi wa kanisa la FPCT Morogoro ambapo tamasha kubwa la uimbaji lilifanyika likishirikisha kwaya na vikundi binafsi vya uimbaji.

Habari njema katika tamasha hilo ilikuwa taarifa rasmi ya uwepo wa tamasha kubwa mwezi wa nane litakalo ongozwa na waimbaji wakubwa Afrika Mashariki akiwemo Sarah K na Solomon Mkubwa.

Baadhi ya picha za Tamasha ni hizi zifuatazo,




 Mtumishi wa Mungu Mwita akitawala jukwaa
 Kwaya ya KKKT Majengo (Kihonda)
Chotlda Mathias akimuimbia Mungu ndani ya ukumbi wa FPCT Morogoro

BEN PAUL AKILI YESU NDIO MPENZI WAKE WA KARIBU WAKIFANYA USHIRIKIANO PACHA NA PAUL CLEMENT


Hii ilikuwa katika tamasha kubwa la LIVE RECORDING iliyo fanywa katika kanisa la VCCT. Kama hukuhudhulia na ulishawahi kuzisikia sauti za hawa watu katika kazi tofauti tofauti basi utakuwa umepata picha japo kidogo. NANI AJUAE PENGINE HII NI MBEGU SAFI ILIYO PANDWA NA PAUL CLEMENT KWA BEN PAUL,



MUNGU YU MWEMA, HONGERA PAUL CLEMENT

Saturday, June 21, 2014

KUPANDISHA MAPEPO KWA MFANYA HAFSA KAZINJA KUBADILI DINI.

Hafsa Kazinja anayetamba na Wimbo wa Mlala Nje huku video yake ikiwa tayari, ameamua kuikacha dini yake ya Kiislam na kuhamia kwenye Ukristo.Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Hafsa alisema alifikia uamuzi huo baada ya kusumbuliwa na maruhani ambayo yalimfanya arukwe na akili.


Mwanamuziki Hafsa Kazinja.

“Niliumwa sana hadi ikaonekana nimerukwa na akili, maruhani ndiyo yaliyokuwa yananisumbua. Kuna kipindi yalikuwa yakiniambia nisile samaki wala dagaa, mara yakaniambia natakiwa kuwa mganga.

“Njia zote ziligonga mwamba, nikaambiwa nisali na nimuachie Mungu, nikawa nikisali sauti zinanijia nimtukane Mungu tena matusi makubwa, nimeenda hadi kwa waganga, mashehe na walokole wakaniombea na nikapoteza pesa nyingi hadi nikauza nyumba yangu na magari lakini wapi. Nimekwenda Kanisa la Zoe ndiyo nimepona, namshukuru Mungu.
“Sasa nimeamua kuwa Mkristo, yaani nimebadili dini kwa kumaanisha, nampenda Mungu katika roho na kweli. Sijabatizwa hivyo bado sijabadili jina ila nasali Kanisa la Zoe lililopo Segerea jijini Dar.”

Wednesday, June 18, 2014

ASKOFU KAKOBE

SOMO : JINSI YA KUOMBA MWENYEWE NA KUPATA JIBU

Askofu Zachary Kakobe.

NENO LA MSINGI

YOHANA 16:24

“Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu: OMBENI, NANYI MTAPATA; furaha yenu iwe timilifu”.

Maneno haya aliyasema Yesu Kristo mwenyewe akiwaambia Wanafunzi wake. Tunaona katika maneno haya kwamba, kila mwanafunzi wa Yesu au mtu aliyeokoka, ana haki ya kumwomba Baba yetu aliye mbinguni kwa Jina la Yesu Kristo na akapokea jibu. Yesu hasemi kwamba mtu fulani tu aliyeokoka akiomba, ndiye atakayepata jibu, bali YEYOTE.

MARKO 11:23

“Amin, nawaambia, YEYOTE atakayeuambia mlima huu, ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.”

Maandiko mengi yanadhihirisha jinsi ambavyo kila mtu aliyeokoka alivyo na haki ya kuomba na kupokea jibu na wala siyo mtu fulani pekee. [Angalia mifano katika YOHANA 14:12-14; MATHAYO 7:8-11].

ANGALIA TENA LUKA 11:10; “ Kwa kuwa KILA AOMBAYE HUPOKEA…….”.

Unaona! Kila mtoto wa Mungu, yaani kila mtu aliyeokoka, akiomba, hupokea. Huu ni UHONDO maalum kwa watoto wa Mungu tu. Mtu ambaye hajaokoka, ametenganishwa kabisa na Mungu kutokana na maovu yake. Kutokana na dhambi za mtu ambaye hajaokoka kumfarikisha au kumtenganisha na Mungu, sala zake ni machukizo mbele za Mungu na hazisikilizwi kabisa. [SOMA ISAYA 59:2; MITHALI 28:9; MITHALI 15:29; YOHANA 9:31]. Sala pekee ambayo inasikilizwa na Mungu inapotoka kwa mtu ambaye hajaokoka, ni pale anapotubu dhambi zake na kuwa tayari kuziacha na kuomba damu ya Yesu imsafishe uovu wake; ili aokolewe kutoka katika mauti ya milele [1 YOHANA 1:7-9]. Mtu ambaye hajaokoka, akimpokea Yesu Kristo kuwa Bwana au Mtawala wake na mwokozi wake ndipo anapofanyika MTOTO WA MUNGU na kuanza kufaidi uhondo wa kujibiwa maombi na Baba yetu aliye mbinguni [YOHANA 1:12]. Kabla ya kuokoka, mtu anakuwa ni mtoto wa Ibilisi, na siyo mtoto wa Mungu [YOHANA 8:44]. Kwa sababu hiyo ili uingie katika mpango wa Mungu wa kukupa majibu ya maombi, kwanza ni lazima ukubali kuokolewa na kuwa mtoto wake.

KUTEGEMEA KUOMBEWA NA MWINGINE WAKATI WOTE

Ni huzuni kwamba, wako watoto wa Mungu ambao wanafikiria kwamba wao hawawezi kusikilizwa na Mungu na kujibiwa; mpaka waombewe na mtoto wa Mungu mwingine. Huku ni kukosa ufahamu. Hakuna upendeleo kwa Mungu. Mtoto yeyote katika familia ya Mungu anakubaliwa na Baba aliye Mbinguni. Hakuna mtoto anayekubaliwa na Mungu zaidi anapoomba kuliko mwingine [SOMA MATENDO 10:34-35; WARUMI 2:10-11; KUMB.10:17]. Biblia inasema Mungu hapokei uso wa mwanadamu, yaani hamuoni mtoto wake mmoja kuwa ni bora kuliko wengine kiasi ya kwamba wengine asiwajali [WAGALATIA 2:6]. Eliya alipoomba mvua isinye kwa miaka 31/2; halafu akaomba tena mbingu zikatoa mvua; alikuwa katika hali ya mtoto wa Mungu kama yeyote yule. Alikuwa mwenye tabia moja na sisi, na Mungu hakufanya hayo kwa sababu aliomba Eliya! [YAKOBO 5:17-18].

Watu wengi waliookoka, wanatembea huko na huko katika mikutano wakihitaji kuombewa na watu wengine. Miongoni mwao, wako wanaofikiri sala ya mzungu fulani kutoka Marekani au Uingereza ndiyo ataisikia Mungu zaidi kuliko sala yake. Huku ni kukosa ufahamu. Mungu hapokei uso wa mwanadamu wala hana upendeleo. Kila aaminiye, akiomba hupokea. Ukifanya utafiti, utagundua kwamba, mara nyingi watu ambao wanapokea miujiza wanapoombewa na wengine; ni wale ambao hawajaokoka kabisa, au wale waliookoka lakini wakiwa na muda mfupi sana katika wokovu. Sababu ni kwamba, baada ya mtu kuwa na muda mrefu katika wokovu; unatazamiwa na Mungu kuchukua mwenyewe chakula na kukila bila kungoja kulishwa. Biblia inasema uponyaji ni chakula cha watoto wa Mungu [MATHAYO15:26]. Katika hali ya asili, mtoto anapozaliwa, katika uchanga hulishwa kwa kijiko na mtu mwingine, kwa sababu hawezi kujilisha mwenyewe. Mtoto huyo anapokua, anatazamiwa achukue kijiko na kula mwenyewe. Haitapendeza kumwona mtoto mwenye miaka kumi, akilishwa chakula na mtu mwingine. Vivyo hivyo katika maombi, kila mtu aliyeokoka anatazamiwa kuomba mwenyewe na kuchukua jibu lake. Kwa kukosa maarifa, watu wengi wa Mungu wameangamia [HOSEA 4:6]; na kukosa majibu ya maombi yao. Yafuatayo ni maarifa unayopaswa kuwa nayo ili upate majibu ya maombi yako kila mara.

A: MAMBO MANNE YA KUYAFAHAMU KABLA YA KUMWOMBA MUNGU LOLOTE
1. Mfahamu Vizuri Mungu Baba na Mungu Mwana

Kwa kuwa tunamwomba Mungu Baba kwa jina la Mungu Mwana-Yesu Kristo, ni vema sana kuwafahamu vizuri ili tuwe na hakika ya kujibiwa. Ufahamu ulio nao kuhusu mtu unayekwenda kumwomba hitaji lako, unaweza ukakupa imani ya kupokea kwake au ukakupunguzia imani hata ya kwenda kumweleza hitaji lako. Ukifahamu kwamba mtu fulani ni katili, ufahamu huo unatosha kuondoa ujasiri wa kumwomba lolote. Kwa kukosa kuwafahamu vizuri Mungu Baba na Mungu Mwana, watu wengi waliookoka wamekosa msingi mzuri wa kujibiwa maombi yao. Kinyume na inavyopasa, msingi wao wa kuomba unakuwa ni manung’uniko ambayo huleta maangamizo badala ya mafanikio [SOMA 1 WAKORINTHO 10:10]. Ukiwafahamu vizuri Mungu Baba na Mungu Mwana, ufahamu huo pekee, utakufanya uwe na hakika ya mambo unayotarajia kuyapata; ingawa hayajaonekana bado. Hii ndiyo inayoitwa IMANI ambayo ni msingi muhimu wa kupewa majibu yetu [WAEBRANIA 11:1,6]. Imani ni kuamini jinsi Neno la Mungu linavyoeleza kuhusu Mungu alivyo kwetu. Ukiwafahamu Mungu Baba na Mwana walivyo huwezi kunung’unika, kubabaika na kukata tamaa. Kunung’unika, Kubabaika na Kukata tamaa; ni kinyume kabisa na Imani. Watu wanaonung’unika, kubabaika na kukata tamaa, ni watu wasiomfahamu Mungu alivyo. Usiwe miongoni mwa watu wa jinsi hiyo, ambao hawawezi kupata majibu ya maombi yao.



Inakubidi basi, kuyafahamu yafuatayo na kuyaamini kabla ya kuomba; ili upate Majibu yaMaombi yako:

Mungu Baba hujishughulisha SANA na kila jambo tunalolihitaji, liwe dogo au kubwa. Wakati wote, fahamu kwamba hitaji ulilonalo anapenda kulishughulikia mno. Anataka tu, umtwike YEYE fadhaiko ulilo nalo. [SOMA 1 PETRO 5:6-7].

(b) Ni mapenzi ya Mungu Baba, kukupa haja za moyo wako na kukuona una furaha baada ya kujibiwa maombi [SOMA ZABURI 37:4; YOHANA 16:24].

(c) Mungu Baba anawahurumia watu waliookolewa kama vile Baba awahurumiavyo watoto wake [SOMA ZABURI 103:13]. Linalofurahisha zaidi ni kwamba, Mungu Baba; ni Baba mwenye uwezo wote, tofauti na baba wa duniani ambao wanaweza kuwa na huruma kwa watoto wao, lakini wakakosa uwezo wa kuwasaidia; wakabaki kusema “POLE”, bali huruma ya Mungu huambatana na UWEZO wa kutupa mahitaji yetu; hata yakiwa mazito kiasi gani. [ANGALIA MFANO LUKA 7:13-15].

Saturday, June 14, 2014

REUVIN RIVLIN: RAIS MPYA WA ISRAELI.

Reuven Rivlin amechaguliwa na bunge la Israel 10.06.2014 kuwa rais mpya wa taifa hilo la kiyahudi akichukuwa mahala panapoachwa na Shimon Peres

Rais mteule wa Israel Reuven Rivlin
Rais mteule wa Israel Reuven Rivlin
Rivlin ambaye ni mwanachama wa chama tawala cha mrengo wa kulia cha Likud anakuwa ni rais wa 10 wa taifa hilo anayetwaa nafasi ya Shimon Peres anayeachia madaraka mwezi Julai.
Akitangaza ushindi huo wa Reuven Rivlin,spika wa bunge la Israel Yuli Edelstein amesema Rivlin amewashinda katika kinyang'anyiro hicho mpinzani wake wa mrengo wa kati Meir Sheetrit kwa kura 63 dhidi ya 53 katika zoezi la upigaji kura kwa siri katika bunge la nchi hiyo lenye viti 120.
Rais Schimon Peres na mwenzake wa Palestina Mahmoud Abbass
Rais Schimon Peres na mwenzake wa Palestina Mahmoud Abbass
Rivlin amewahi kuwa spika wa bunge mara mbili na ni mtu anayetajwa kuwa mwenye msimamo thabiti katika kupinga azma ya kuundwa kwa dola la wapalestina na vile vile amekuwa daima akiunga mkono ujenzi wa makaazi zaidi ya walowezi katika ardhi ya wapalestina iliyonyakuliwa kwa mabavu na Israel.Ni mwanasheria na mtu ambaye anafahamika sana katika juhudi zake za kutetea demokrasia na haki za kiraia ambazo zimempa heshima kubwa katika upande wa mrengo wa kushoto na hata miongoni jamii ya waarabu waliowachache katika taifa hilo la kiyahudi.
Hata hivyo rais huyo mteule wa Israel mwenye umri wa miaka 74 atakuwa na kibarua kigumu kufuata nyayo za rais anayeondoka madarakani Shimon Peres ambaye haiba yake na umaarufu ulimpa nafasi ya kutumia wadhifa wake wa urais ambao hauna mamlaka makubwa katika kuueneza au kuupa nguvu ujumbe wa amani katika ngazi ya kisiasa.Wengi wa wadadisi wa mambo wanaashiria kwamba baada ya kuondoka Peres madarakani mwezi Julai huenda mwelekeo wa siasa za Israel ukajikita kutoka kwenye mrengo wa Kimataifa na kuzingatia zaidi masuala ya ndani.
Katika Duru ya mwanzo wabunge walipiga kura kuamua juu ya wagombea watano waliojitokeza kugombea nafasi hiyo akiwemo Dalia Itzik mwanamke wa kwanza kuwahi kushikilia nafasi ya spika wa bunge la Israel,Knesset,jaji msatafu wa mahakama kuu Dali Dorner na mshindi wa tuzo ya Nobel ya Kemia Dan Shechtman.
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu akiwa bungeni
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu akiwa bungeni
Hata hivyo Ushindi wa Rivlin umekuja katika duru ya pili ambayo ni ya mwisho ya mpambano huo dhidi ya mgombea wa chama cha mrengo wa wastani cha Hatenua,Meir Shitrit.Pamoja na kuwa anapinga fikra ya kuwepo dola la wapalestina katika Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Gaza anawafiki ushirikiano zaidi na waarabu na hata hatua ya kuwapa uraia wa Israel wapalestina zaidi.
Shimon Peres rais anayestaafu
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu ameupongeza ushindi wa Rivlin akisema anataraji ushirikiaono wa karibu na rais huyo mteule ambaye mamlaka yake sio makubwa lakini anauwezo kiasi katika masuala muhimu,ikiwemo katika utoaji wa msahama kwa wafungwa pamoja na kumteua waziri mkuu mpya baada ya uchaguzi.Rais anayeondoka Shimon Peres ana umri wa miaka 90 na amekuwa rais wa Israel tangu mwaka 2007 baada ya kuondoka Moshe Katsav aliyeshtakiwa kwa tuhuma za ubakaji.Hata hivyo dalili zote zinaonyesha kwamba Peres ambaye ni mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel ataendelea kujihusisha na siasa ingawa inaonekana hatokuwa na wadhifa wowote wa kisiasa katika taifa hilo kwa mara yake ya kwanza katika kipindi cha miongo mingi.