Friday, November 29, 2013

PETER NYAGA, MIAKA 7 YA UREJESHO


POPO WAIBUKA TANGA


Muda mfupi baada ya Mch Gwajima kuanza kuhubiri jana kukaibuka kundi kubwa la popo sijawahi ona mpaka uwanja ukawa na kimvuli hivi mapopo makubwa kama kungulu mchana kweupe,wachawi wa Tanga wanamambo kweli,wachawi wa Tanga jana walianguka kila mmoja kwa wakati wake wa3 live wananchi fujo wanataka wawapige watu wamechachamaa.WOTE WAMESHINDWA KWA JINA LA YESU.
BY FLORA MBASHA

Thursday, November 28, 2013

WATU ZAIDI YA KUMI WATOA USHUHUDA WA KUOKOLEWA KUTOKA MSUKULENI




Katika siku ya pili ya Mkutano Mkubwa wa kutokea katika mkoa wa Tanga kumekuwa na matendo makuu na maajbu ambayo Mungu ameyatenda kupitia kwa Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima, wa Kanisa la Glory of Christ (T)  Church- Ufufuo na Uzima.










Mchungaji Gwajima akiwabariki na kuwawekea ulinzi maelfu ya watu ili wasichukuliwe au kudhuriwa tena na shetani kwa Jina la Yesu
HALIMA ALLY
Anatoa ushuhuda wake na kuelezea kuwa alikuwa amechukuliwa msukule na Bibi mmoja aitwaye  Nyatanga ambaye ni mchawi, na alikuwa amemuweka kwenye shimo kubwa jeusi.
Halima aliendelea kuelezea akiwa na machungu sana huku akilia kutokana na mateso makali na mambo ya kikatili aliyoyaona huko msukuleni, aliuelezea uamti kuwa chakula alichokuwa anakula ni Pumba za mahindi na za mtama...na shughuli yake kubwa ilikuwa ni kutumikishwa mambo ya kichawi na kuwadhuru wanadamu.

Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima akiwa na HALIMA ALLY akiwa anatoa ushuhuda wake kwa machungu sana huku akibubujikwa na machozi ya kwikwi.

Mama yake mzazi aliweza kuitwa na kujitokeza na akaelezea kuwa mtoto wake alikuwa hana maendeleo mazuri shuleni wala nyumbani na alikuwa hajui hasa chanzo ni nini.

Mama yake Halima alitoa kauli nzito za kulaani vitendo vya kichawi na akamshukuru sana Mungu kwa kumuokoa mtoto wake kutoka utumwani mwa shetani, na wote wawili walimpokea Yesu na wameahidi kummpa Yesu maisha yao milele yote.

HUSSEIN OMARY
Ni kijana ambaye anaishi Tanga mjini alifika siku ya Pili ya mkutano, maisha yake yalikuwa na mikosi isiyoisha.
Lakini baada ya maombezi ya Mchungaji Josephat Gwajima ikaja kugundulika kuwa nafsi ya  Hussein ilikuwa imechukuliwa msukule kwa njia za kichawi na alikuwa anatumikishwa kulima mashambani huko Bumbuli. 


Mchungaji Josephat Gwajima akiwa na Hussein Omari mbele ya maelfu ya watu akiwa anatoa ushuhuda wake.

Mama yake Hussein akilia kwa uchungu huku akielezea furaha yake moyoni kwa kummpata tena mwanae wa mwisho Hussein,Pia Hussein akiwa analia kwa furaha kwa kuweza tena kumuona mama yake Mzazi
Hussein akimshukuru Mungu na kuahidi kumkabidhi bwana Yesu maisha yake milele.

Mama yake mzazi Hussein (mwenye nyekundu) na Mama mdogo katikati wakimlaki mtoto wao baada ya kurudishwa kutoka msukuleni.

MWANAIDI JULIASI

Dada huyu alipokea uponyaji wake baada ya kuombewa na mchungaji Josephat Gwajima kwa Jina la Yesu, ni msichana ambaye kwa muda mwingi ameishi na mama yake wa kambo.

Lakini ikafikia wakati akachukuliwa msukule na huyo huyo mama wa kambo na kuplekwa kutumikishwa katika mashamba, ambapo, yeye mwenyewe anaelezea huku akiwa analia sana kiasi cha kuishiwa nguvu, kuwa alikuwa analimishwa sana kwa njia za kichawi mashamba ambayo ni makubwa sana..

Lakini Baada ya maombezi alianza kusikia sauti ya Mungu inamuita njoo..na ndipo alipoambiwa na huyo mchawi aliyekuwa anamtumikisha kuwa hafai na aondoke mara moja na hatimaye akajishtukia yuko uwanja wa Tangamano.
Mwanaidi Julias akimshukuru Mungu kwa kumuokoa kutoka katika kifungo cha shetani.
KHADIJA KASSIAN
Binti huyu anaitwa Khadija Kassian ni mkazi wa Tanga mjini ametoa ushuhuda wake kuwa alikuwa juu ya mti na kazi yake ilikuwa kumfanyia ushirikina mme wake.

Baada ya maombezi Khadija alikiri kuchukizwa sana na mambo ya kutumikishwa na shetani na alikiri kumkabidhi Yesu Kristo maisha yake.

Alimshukuru sana Mungu kwa kumuokoa.
Khadija Kassian akihojiwa na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima na akikiri mbele za watu kazi alizokuwa anaifanya ya kumufanyia ushirikina mme wake, ila amekiri kuacha na kumpokea Yesu.
Jojina Leonada, ndio jina la huyu dada, alikuwa anamuelezea Mchungaji Josephat Gwajima alipokuwa anamuhoji mbele ya Maelfu ya umati wa watu.Alitoa ushuhuda wake kuwa alikuwa amechukuliwa na Bibi mmoja wa kimakonde, na alikuwa amemuweka nyuma ya mlango chumbani kwa huyo Bibi, ambaye ananyumba yake huko malamba sehemu moja mjini Tanga, aliendelea kutoa shuhuda kuwa alikuwa akifanywa kiti na kukaliwa pindi ambapo bibi huyo alikuwa anaenda kufanya mambo ya kichawi...yani alikuwa chombo cha usafiri kabisa...bibi anamkalia na yeye anaenda, mfano wa punda.


Jojina akiwa anamshukuru Mchungaji Kiongozi kwa kumuombea kwa Jina la Yesu na amerudishwa kutoka msukuleni.


HILDA JOHN
 Ni mwanamke aliyekuwa anaishi mjini Tanga lakini kumbe alikuwa amechukuliwa msukule na bibi yake huko barabara ya 19 ambako alikuwa anatumikishwa mabo mengi ya kichawi 
Hilda akiombewa na Mchungaji Kiongozi Josphat Gwajiama.

SIKUZANI MSIAKA
Huyu ni mtoto wa kike mwenye umri wa Miaka 19 anaishi Tanga Barabara ya 16, baada ya kuombewa na Mchungaji Josephat Gwajima katika uwanja wa Tangamano, alianza kutoa ushuhuda wake.
Alisema alikuwa anaishi chini ya Bahari ya Hindi, na huko alikuwa analishwa nyama za watu, alianza kuelezea ilikuwaje hadi akawa huko chini ya bahari na ndipo akasema katika siku ambayo haifahamu vizuri mwaka 2009 alianza kuota ndoto mbaya mbaya sana, na zikaendelea kwa kipindi kirefu sana hadi siku moja akawa anaota ameshikiwa upanga na mkuki akiongozwa aelekee baharini na ndipo alipokuwa hadi anarudishwa uwanjani hapo.
Msichana aitwaye Sikuzani akimuelezea Mchungaji Josphat Gwajima kuhusu maisha yake ya kulishwa nyama za watu chini ya bahari ambako amekuwa huko Tangu mwaka 2009.

Sikuzani alimshukuru Mungu kwa Kumukomboa kutoka katika vifungo vya shetani na aliahidi kumpokea Yesu kuwa Bwana na Muokozi wa Maisha yake.

 Fadhili ni kijana anayeishi Chimbageni katika mkoa wa Tanga, na yeye aliweza kuokolewa baada ya maombezi na mchungaji Josephat Gwajima.

Yeye mwenyewe alishuhudia akisema kuwa alikuwa analimishwa mashamba makubwa sana, na anamfahamu aliyekuwa amamchukua kwa njia za kichawi na kumtumikisha , na akadai kuwa na Mama wa nyumba ya Jirani..

Pia akasema kuna vipindi anapelekwa kishirikina katika msitu mkubwa sana kufanya mambo ya uchawi pia.
Fadhili Chamshama akilia kwa uchungu akiwa anaelezea mateso makalia aliyokuwa anatendewa huko msukuleni

RODGERS FREDERICK
Ni kijana mdogo ambaye na yeye alifanikiwa kuachiwa shetani baada ya maombezi na Mchungaji Josephat Gwajima, Rodgers alipoulizwa aelezee alikuwa wapi akasema alikuwa msikitini alipokuwa amekewa jini maimuna.
Na aliyekuwa amemmpeleka msikitini ni shekh aliyemtambulisha kwa Jina moja la Hassan ambaye ni sheikh kwenye msikiti uliopo mjini Tanga katika barabara ya 15
Rodgers anaelezea jinsi sheikh Hassan alipokuwa anamtumia kupandisha mashetani na kuongea kiarabu, na kumtumia kwenye mambo ya kishirikina

Kijana Rodgers Frederick alimshukuru Mungu kwa Kumuokoa na akaahidi kummpokea Yesu kuwa Bwana na muokozi binafsi wa Maisha yake.


ZAWADI
Anaelezea kuwa alikuwa amechukuliwa msukule na Bibi upande wa Baba yake mzazi, anaendlea kusema kuwa bibi huyo alikuwa anamtuma usiku wa manane akawamwagie watu madawa ambayo yeye anaelezea kuwa zile dawa ni kwa ajili ya kuwapumbaza watu akili, na kuwavurugia maisha.
 Zawadi alipoulizwa kuwa ametoka wapi kwa sasa akasema alikuwa chini ya meza kwenye nyumba ya huyo bibi, ghafla akaanza kusikia sauti inamwita na bibi yakee akaiskia pia akshtuka sana, bibi yake akaanza kumfukuza kwa kumpigia kelele "ondoka! ondoka! usiniletee balaa""!! na yeye akaanza kusikia kwa jina la Yesu Njooo"" na ndipo akazidi kukimbia na akajishtukia yuko katika uwanja wa Tangamano
Zawadi anamshukuru sana Mungu kwa kumkomboa aliahidi kummpokea Yesu na kuanza kumtumikia Mungu.

ANNA RAPHAELI
Kisa cha Anna kinasikitisha na kinafanya kila mtu mwenye akili amlaani shetani, Anna alirudishwa baada ya kuombewa na Mchungaji Josephat Gwajima, Aisema huku akiwa analia kwa uchungu sana na kudai kuwa alikuwa amewekwa kwenye chupa, ambako alikuwa amewekwa kwa ajili ya kuwalea watoto, kwenye hiyo hiyo chupa.
Aliendelea kusema kuwa kwenye chupa kulikuwa na watoto wadogo sana ambao yeye lalifungiwa nao ili awalee, Baada ya maombezi siku hii alianza kuhisi chupa inawaka moto na anahamishwa na sauti ya Mungu iliyokuwa inamuita, huku wale watoto nao wakimuomba aende nao..lakini baada ya kitambo kidogo akajikuta yuko katika uwanja wa Tangamano.

Anna Raphaeli alimshukuru Mungu kwa kumkomboa kutoka kwenye kifungo cha shetani na ameahidi kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Muokozi wa Maisha yake.
Ni siku ambayo iliambatana na watu kurudishwa na pia kurudishiwa vyote ambavyo shetani amekuwa akiwadhulumu, kwa jina la Yesu watu wengi wamerudi na kuponywa kabisa.

Mungu amembariki sana Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima kwa kumfikisha katika mikoa ya Arusha, Moshi na sasa ni Tanga na kote huko kumekuwa na miujiza na matendo makuu ya Mungu ambayo yamewafanya watu waokolewe kutoka katika mikono ya shetani.

Wednesday, November 27, 2013

KUMBUKUMBU YA KUSHEHEREKEA MIAKA 20 YA NDOA YA MTUME NA NABII JOSEPHAT E. MWINGIRA


 ''Baba na Mama Watumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat na Mchungaji Eliakunda Elias Mwingira wakiwa ndani Hemani mwa BWANA wakiingia...''

 Watumishi wa MUNGU wakipongezana baada ya Kuvishana pete katika Kusherekea Miaka 20 ya Ndoa Takatifu leo.
 Watumishi wa MUNGU toka nje ya Tanzania (Namibia na Uingereza) wakiwa Hemani mwa BWANA wakishuhudia sherehe ya Miaka ya 20 ya Ndoa ya Watumishi wa MUNGU Mtume na Nabii.
UTUKUFU kwa MUNGU Wetu MKUU




 Mtumishi wa MUNGU Mark Kariuki akihubiri katika Ibada hii,...

.
 Wazazi wa Mtumishi wa MUNGU na Watoto wa Mtume na Nabii wakifuatilia Ibada hemani mwa BWANA.
 Pete zikiwa ndani ya Mafuta Matakatifu toka Isreal ya Mizeituni yakiyokwisha Ombewa tayari kwa ajili ya Ibada hii ya Kumbukumbu ya Miaka 20 ya Ndoa ya Watumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat na Mchungaji Eliakunda Elias Mwingira , Efatha Mwenge Dar es Salaam, Tanzania.


 Baba Mzazi na Mama Mzazi wa Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii, wakiwashika mikono na kutoa Salamu za Pongezi kwa Watoto wao.


Monday, November 25, 2013

AGANO LA TATU LIMEGUNDULIWA

By Apostle Eliya 0759 166 934


AGANO KUU



YALIYOMO; 1).UTANGULIZI 2).AGANO KUU 3).HITIMISHO



DHUMUNI LA SOMO

- Kugundua Agano kuu kati ya sisi na Mungu



ANDIKO KUU; Ezekieli 37:27 Tena maskani yangu itakuwa pamoja nao,nami nitakuwa Mungu wao,nao watakuwa watu wangu.



1. UTANGULIZI

- Kila Mwanadamu asiyesikia au kusoma au kujua hili Agano kuu amelaaniwa, narudia tena A M E L A A N I W A --- YEREMIA 11:3-4. Mtu yeyote asiyejua hili Agano kuu ALAANIWE, ALAANIWE, TENA ALAANIWE kabisa

- Wengi wanajua kuna maagano mawili, la kale (AK) na Jipya (AJ), lakini sio kweli. Agano lipo moja tu, ndio nimeliita AGANO KUU. Kwamujibu wangu AK naliita MCHAKATO KIVULI na AJ naliita MCHAKATO HALISI.

- Ukweli ni kwamba Mungu ameweka agano na kila kilichoumbwa, kalini sitazungumzia haya maagano, mfano; agano la chumvi, Agano la walawi na Yuda, agano la viumbe, agano la marafiki na agano la Macho, badala yake nitazungumzia Agano moja tu --- Agano kuu.



2. AGANO KUU

- Nimemshangaa sana Mungu baada ya kusoma hili andiko TORATI 29:10-15 Mungu aliweka Agano moja(Horebu) na wanadamu wote, Kuanzia Ibrahimu mpaka Mtanzania wa mwisho, rudia kusoma huo mstari wa 15. Bado Yesu akarudia = YOHANA 17:20. Tofauti iliyopo ni MICHAKATO (Matengenezo) ya kufanya hilo Agano liwe halisi. EBRANIA 9:10



A).AGANO LIPO MOJA TU

- Kama Mungu ameweka Agano na kila kiumbe, itakuwa ni ajabu sana asipokuwa na Agano na Mwanadamu, pia itakuwa ni ajabu sana akiwa na Maagano tofauti-tofauti na wanadamu, ndio maana nasema kuna Agano moja.

- Yeremia 11:4. Ahadi Kkuu ya Agano kuu ni Uzima wa milele = 1YOH 2:25

  1. Agano Kuu Moja ni Lipi?  EZEKIELI 37:27

-        Agano kuu hili hapa, Mungu anasema; Maskani yangu itakuwa pamoja nao, Nitakuwa Mungu wao, watakuwa watu wangu. Hili ndilo Agano Kuu, lina sentesi tatu (3) tu.

AU

-        Kwa Kiswahili kingine Mungu angesema; Nitakuwa na mahusiano nae, Nami nitakuwa Mume wake, naye atakuwa mke wangu =ISAY 54:5-6

AU

-        Ni sawa na Mungu kusema; Makao yangu pamoja nao, Nitakuwa Baba yao, Watakuwa wana wangu. = UFUNUO 21:7



-        Sasa ili hili Agano Kuu litimie, kulikuwa na vikwazo ambavyo vilitakiwa viondolewe kwa michakato maalum, hii michakato ndio watu wakaiita Agano la Kale na Agano Jipya. Hii ni michakato tu na sio maagano. YEREMIA 31:33-34



  1. Vikwazo Vikuu cha Agano Kuu.

- Kwazo la kwanza ni Dhambi

    • Dhambi ya ulimwengu YOHANA 1:29
    • Dhambi halisi YOHANA 5:14, 8:11, 1YOH 2:2



- Kwazo la pili ni Mungu na Agano lake kueleweka kwa wanadamu. Sio rahisi mtu amuelewe Mungu asiyeonekana na Agano lake lisiloonekana. Ndio maana Mungu amekuwa akitumia Ahadi, angalau tu aeleweke.   ISAYA 53:1



  1. Vichakatuo Vya Agano Kuu

- Vichatuo ni vitu ambavyo vilitakiwa vifanywe ili Agano kuu lifanyike kisha liwe endelevu;

·        Mungu anaanzisha Agano kwa kutamka NENO MWANZO 12:1

·        Mwanadamu anaitikia kwa kuamini kwa hiyari- TORATI 30:14

·        Mungu anafuta Dhambi za Mwanadamu -- kwa Damu WAEBR 9:12

·        Mungu anampongeza Mtu kwa kuamini anampa Roho - MDO 2:28

·        Mtu anatakiwa atunze Agano -- asimhuzunishe Roho - EFE 4:30



  1. Vielezi vya Agano Kuu

- Ili Mungu aeleweke kwa Mwanadamu, anaambatanisha Ahadi na viapo kwenye Agano kuu, kwasababu sentesi 3 za Agano hazimshawishi Mwanadamu kujibidiisha kwenye Agano kuu;

·        Nchi Mpya 17:7-8

·        Uzazi mwingi MWANZO 28:14

·        Baraka/utajiri/kutawala MWANZO 22:17-18



  1. Ishara(Viashiria) Vya Agano Kuu.

- Kama umegundua ni kwamba Agano ni NENO tu linalotamkwa, hivyo Agano huwa halionekani, kwasababu hiyo Mungu ameweka Ishara ili iwakumbushe wote wawili kuwa wapo kwenye Agano Kuu;

·        Damu --- ni kwa ajili ya Mungu KUTOKA 12:13

·        Kupigwa muhuri --- Nikwa ajili ya Mwanadamu MWANZO 17:11

    =►Malupu-lupu ya Agano Kuu ni Baraka utajiri na kumtawala Adui.



B) MCHAKATO KIVULI NA MCHAKATO HALISI



- Hili Agano la Kale lilitoka wapi ? Hili lilikuwa ni wazo zuri la watu(Baada ya Yesu) kuwafanya watu waelewe utofauti wa kabla na baada ya Yesu, hivyo wakaamua nyakati za kale waziite Agano la Kale na Nyakati za Yesu waziite Agano Jipya. Lakini kiuhalisia, sio maagano.



- Nimekwisha kueleza hapo juu kwamba Agano kuu ni moja lakini michakato ya kufanikisha hilo Agano Kuu ni tofauti kwa uhalisia wake, sasa angalia jedwali hapa chini uone tofauti ya mchakato kivuli na mchakato halisi. Kumbuka Agano Kuu ni Moja




MCHAKATO
KIVULI
HALISI
Nchi Tarajiwa----
Kanaani =LAW 25:38-------------
Mbingu Mpya=UFUN 21:1
 Makuhani---
Walawi = HESABU 17:8
Yesu = WAEBR 5:6
Wafalme-----
Yuda =
Yesu = UFUNUO 17:14
Kafara------
Wanyama = LAWI 23:19
Yesu = WAEBRANIA 10:10
Dhambi------
Kusitiriwa = ZABURI 85:2
Kufutwa = EFESO 1:7
Viongozi----
Torat/makuhani=
Roho Mt =RUMI 8:9
Msamaha-----
Kila sabato= EBR 10:11
Mara moja tu= EBRA 9:12
Sheria------
Zaidi ya 600
1 = EFESO 4:30
Amri
10 = KUTOKA 34:28
2 =MATHAYO 22:37-40
Dalili za Uwepo-------
Sanduku = KUTOK 29:43-46
Roho Mt = EFESO 1:13-14
Vita na adui
Mataifa = TORAT 20:17
Shetani/pepo =EFESO 6:16
Wahusika wakuu-------
Israeli tu =KUTOK 3:10
Mtu yeyote =MARKO 16:15
Tohara------
Zunga = MWANZO 17:11
Moyo =YEREMIA 4:4
Makutanio----
Sandukuni =KUTOK 25:22
Moyoni = KOLOSAI 1:27
Kuhesabiwa haki---------
Kwa Sheria =LUKA 1:6
Imani =RUMI 1:17
Ghafi za Hekalu-------
Jengo =1FALME 5:18
Mwili =1 KORINTHO 3:16
Makao ya Roho
Nnje,juu = ISAYA 61:1
Ndani = YOHANA 14:17
Thawabu------
Ya muda = EBRANIA 4:8
Uzima milele = MDO 13:48







    

C) MCHAKATO KIVULI



- Agano Kuu lilianzia kabla ya ulimwengu kuumbwa = TITO 1:2, Adam na Eva, wakalivunja, Mungu akawafukuza. Toka hapo Mungu akaanza kutafuta mtu atakayekubali kufanya nae Agano tena, lakini huyo mtu shariti asiwe na dhambi, kwahiyo mahangaiko yoote ya watu wa kale ni kuondoa kikwazo cha Dhambi, lakini haikuwa rahisi kuondoa dhambi kama walivyodhani. MWANZO 3:24



- Mara zote Mungu amekuwa akimtaja Ibrahim, Isaka na Yakobo katika Agano kuu WAAMUZI 2:20, Kwasababu ya kutii kwao aliwapa na AhadiUzao, Nchi na Baraka = MWANZO 17:14. Pia akaweka Ishara ya Agano naoKutahiliwa, yote hayo hayakuwa Agano = JOSHUA 5:2. Ninashawishika kuona kwamba Mungu anajua vizuri sana namna ya kuuza wazo lake la Agano.



- Chunguza hizi sehemu tatu 1) Misri 2)Horebu(Jangwani) na 3) Kanaani. Mungu aliwakomboa Israeli Misri ili aweke nao Agano = KUTOKA 8:1, akaweka nao Agano Jangwani(Horebu)= TORAT 5:2, ili akaishi nao Kanaani=WALAWI 25:38. Zoezi hili halikuwa rahisi. Mungu kupata hisia zao aliamua atumie utumwa wao kuwatajia Nchi yenye Maziwa na Asali, jangwani ilikuwa ni shule ya kuishi kanaani= TORATI 4:10.



- Kama wewe ni msomaji mzuri wa Biblia utakubaliana na mimi kwamba kila kitu kilichokuwa kikitumika kwa ajili ya Mungu wakati wa kabla ya Yesu kiliitwa -- cha Agano. Ikumbukwe kuwa vyenyewe SIO Agano ila ni vitu vya Agano;

·        Sanduku la Agano = 2 NYAKATI 5:7

·        Torati ya Agano = 2 WAFALME 23:2-3

·        Damu ya Agano = KUTOKA 24:8, MATHAYO 26:27-28

·        Ukuhani wa Agano = MALAKI 2:4-5

·        Mbao za Agano = TORATI 9:9

·        Waisraeli-Taifa la Agano = 2 SAMWELI 7:23-24



Sina uhakika sana kama Israeli walikuwa wanajua wanachokifanya, ni kanakwamba Mungu alikuwa anawalazimisha ingawa ni kwafaida yao wenyewe. Nina uhakika, Zoezi la ibada, Sheria, Vita nk vilikuwa vinawakela sana = 2FALME 17:15, kwasababu walikuwa hawajui dhumuni, lakini wachache walitambua. Swali; Watu wangapi walitoka misri na wangapi walioingia Kanaani ?



-Ndivyo Mungu alivyofanya kwetu, ametutoa mikononi mwa 1)Shetani=KOLOSAI 1:13 ili tufanye nae Agano kwa 2) Yesu na Roho(Duniani)=ISAYA 53:11b ili tukaishi na Mungu 3) kwenye Ufalme wake = MATHAYO 8:11. Tupo hapa Duniani kujifunza namna ya kuishi mbinguni, pia wengi wetu hawajui dhumuni, hivyo wengi hawataingia kwenye Ufalme = MATHAYO 7:14. Lakini ashukuriwe Mungu kwani watu wengi miaka hii wameanza kuelewa.= UFUNUO 5:9



D) MCHAKATO HALISI YESU

- Utagundua mvunja Agano siku zote ni Mwanadamu, labda waisraeli hawakujua umuhimu au walifanya makusudi au walijua umuhimu lakini hawakuwezeshwa, vyovyote vile, Mungu aliamua atatue matatizo yote ya Agano Kuu kwa kumleta Mwanawe Yesu = KOL 1:20.Kipi kilimfanya Yesu aje?



1. Dhumuni la Ujio wa Yesu;

·        Kubadiri kivuli kuwa Halisi = WAEBRANIA 8:13

·        Kusajiri watakaoingia kwenye Agano Kuu = UFUN 5:9-10



2 Yesu na Tarajio Jipya.

- Yesu alikuja kutoka mbinguni, anapotaja ulimwengu ujao anauhakika.

·        Ufalme wa Mungu = YOHANA 14:2-3

·        Uzima wa milele = TITO 1:2

·        Kutawala milele = UFUNUO 22:5



3. Vikwazo vya Agano kuu kwa mujibu wa Yesu.

- Kikwazo hapa sio dhambi, kikwazo kimebadirika

·        Kutomwamini Yesu = YOHANA 8:24

·        Kumkufuru na kumhuzunisha Roho Mt = MATH 12:31, EFESO 4:30



4. Vichakatuo vya Agano Kuu kwa mujibu wa Yesu

- Mambo yanayowezesha kuwepo kwa Agano Kuu kwa mchakato Halisi

·        Yesu (Injili)= 1 KORINTHO 15:1-4

·        Roho Mt = RUMI 8:14

·        Mwamini = 1 WATHESALONIKE 5:10

Tunayapokea Yote haya kwa kuliamini jina la Yesu = WARUMIN 10:9



5.Ishara za Agano Kuu kwa mujibu wa Yesu

- Sifa ya Ishara au kiashiria ni lazima kionekane, sasa utamjuaje mtu aliye ndani ya Agano Kuu ?

·        Kumwamini Yesu = YOHANA 11:25

·        Uwepo wa Roho Mt- Karama na Matunda = 1 KORINTHO 12:4-6

·        Kuwa na Nguvu- Kutoa Mapepo = LUKA 11:20, 1 KORI 4:20

   =Ahadi kuu ya Agano kuu ni uzima wa milele = yuda 1:21



E) MUNGU KUTIMIZA AGANO LAKE KUU

- Baada ya Mambo yote, na michakato yote kutimizwa ndio sasa Mungu anasema nitalitimiza Agano langu Kuu. Mungu atafanya makazi na wanadamu,atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake. Itakuwaje ?



1.Kufanywa UpyaKila kitu kitafanywa upya, huwezi amini

·        Mbingu mpya = UFUNUO 21:1

·        Nchi mpya = UFUNUO 21:1

·        Mji mpya = UFUNUO 21:2

·        Utu mpya = KOLOSAI 3:10

Soma hapa uone Mungu anavyosema; UFUNUO 21:7



2. Hatimaye Agano Kuu kutimia

- Yote yakisha fanywa upya, sasa ndio Mungu atalitimiza Agano lake Kuu rasmi. Unakumbuka sentesi tatu(3) za Agano letu na Mungu ?

·        Maskani ya Mungu ni pamoja na Wanadamu = UFUNUO 21:3

·        Atakuwa Mungu wa Wanadamu na = YEREMIA 32:27

·        Wanadamu watakuwa watu wa Mungu = HOSEA 2:23



3. HITIMISHO

- Muda huu tunaoishi hapa Duniani ni sawa na Wana wa Israeli walipokuwa Jangwani, usitegemee Mungu kukufanikisha yote unayoyataka ukiwa hapa Duniani, sio kwamba hawezi au hujamuomba, la hasha, anataka utamani kwenda kwenu. Ukitakakuelewa soma hadithi ya Israeli jangwani. =EBR 13:14



- Agano Kuu lipo moja, hakuna Agano la Kale wala Agano Jipya, hivyo leo piga magoti umwambie Mungu kuwa unataka kuingia Agano naye;

Awe Mungu wako, Uwe mtu wake, na siku ya mwisho, Patakatifu pake pawe katikati yako na watakatifu wote.  



………..Remember……………THE BEST HAS COMES…………………..