Tuesday, July 11, 2017

SOMO #1. HAPO MWANZO

SOMO #1. HAPO MWANZO
Andiko Kuu:- Mwanzo Sura ya 1 yote


1.      MAHUSIANO
Neno “Mungu” katika kitabu cha Mwanzo 1:1 ni ELOHIM, ni neno lenye uwingi katika umoja. Neno ELOHIM linabeba nafsi tatu katika umoja, hizi nafsi tatu bila shaka ni – Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu au Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu, kuwapanga huku hakumaanishi mmoja ni mkubwa kuliko mwingine ila kwa namna walivyo jitokeza kwetu.

·         UUMBAJI-           Mungu alitaka awe na MAHUSIANO NA MWANADAMU, ila asingeweza kuendesha mahusiano bila kuwa na MASKANI,kwahiyo andiko linaanza na kutuonyesha Mungu anavyoshughulika na maandalizi ya Maskani. Kuanzia  Mwanzo 1:1 mpaka Mwanzo 1:25-Mungu alikua akiandaa maskani ili aanze mahusiano na mwanadamu.

·         MWANADAMU             Kilele cha uumbaji wa Mungu ni mwanadamu, baada ya Mungu kua amemaliza kuandaa maskani  na siku ya kukutania (SABATO), ndipo alipomuumba na Mtu ili aanze Mahusiano nae. Kama tunavyojua mwanadamu ana asili mbili – Utu wa Ndani-Mwanzo 1:26-31 na Utu wa Nje-Mwanzo 2:7,15. Baada ya haya yote Mungu alikua akimtembelea Adamu muda wa Jua kupunga ili awe na mahusiano nae  “awe Mungu wake na Mtu awe Mtu wake”.

2.      DHAMBI
·         Mungu alimuumba Mwanadamu akiwa na Asili ya Mungu, alikua Mwenye Haki, Mtakatifu amejaa Utukufu na HIYARI.Mungu alimpa mwanadamu uhuru wa hiyari kwasababu alimuumba kwa mfano wake.Mwanadamu sio roboti au mwanasesele, haendeshwi na mitambo bali ni lazima achague kwa hiyari yake. Kwasababu mwanadamu ana uhuru ni lazima achague kutii na kuamini atakacho.

·         JARIBIO LA UTII –     Mungu alipenda kujua kama Adamu atamtii na Kumuamini anachosema au laa, wakati huo Shetani ambaye ni Baba wa Uongo nae yupo kazini kuhakikisha Mwanadamu hamtii Mungu na hivyo kuvunja  mahusiano. Mungu alitoa katazo-Mwanzo 2:17, Adamu alitii hii kauli siku zote mpaka siku Shetani aliyofanikiwa kumuingia Mwanamke-  Mwanzo 3:1-9. Hivyo Mwanadamu alifanya Dhambi kwa kumtii na kumuamini Shetani kuliko Mungu, matokeo yake ni KUFUKUZWA-Mwanzo 3:24, mahusiano YAKAVUNJIKA, mpaka Dhambi na urejesho wa utukufu vishughulikiwe kwanza, ndio maana Mungu akatoa Ahadi ya kuondoa Dhambi na kumrejeshea mwanadamu utukufu.

3.      UREJESHO

a.       MASIHI:-      Mungu alimpenda sana Mwanadamu, hivyo akawa na wivu nae lakini gharama ya kumrejesha ili mahusiano yaendelee ni kubwa mno, ikabidi Mungu awaahidi kwamba angalikuja mtu mwenye thamani atakae wafanyia UREJESHO,mtu huyo angeliitwa MASIHI- Mwanzo 3:15. Mungu alionyesha namna huyo masihi atavyowarejesha, kwa kuchinjwa – Mwanzo 3:21.

Kabla ya huyo masihi kuja, mwanadamu itatakiwa atoe sadaka ya mnyama aliye safi ili Dhambi yake iendelee kufunikwa kila mwaka, na kila asiyeua mnyama alionyesha kumtii na kumuamini Shetani kuliko Mungu kwani njia pekee ya kumkaribia Mungu ni kumwaga Damu isiyo na Hatia.

Mungu alionyesha NJIA YA UPATANISHO kwa mfano kwa kumvika Adamu Koti la Ngozi, wakati huo Damu ya mnyama ilifanya upatanisho, huu mfano ulipaswa uigwe na Wanadamu.Tatizo linakuja – Damu za wanyama hazikufaa KUMFUTIA HATIA MWANADAMU kwani uthamani wa Mwanadamu ni mkubwa kuliko wa mnyama, hivyo Damu ya mnyama ILIFUNIKA TU DHAMBI, na ndio maana Mungu akaahidi MASIHI ili arejeshe Mahusiano kwa KUFUTA DHAMBI – Isaya 59:20.

b.      ROHO MTAKATIFU:- Mwanadamu alipoasi alipungukiwa na utukufu, hivyo Mtu akishasamehewa Dhambi hupewa zawadi ya Roho Mtakatigu (Utukufu).Kama Mungu alivyoahidi kuwapa wanadamu ZAWADI ya MASIHI ndivyo Mungu alivoahidi kuwapa wanadamu ROHO WAKE MTAKATIFU – Isaya 44:3,kwahiyo Masihi na Roho Mtakatifu ni ZAWADI – Luka 24:49 ambazo Mungu aliziahidi ili arejeshe MAHUSIANO yaliyokua yamevunjika kwasababu ya Dhambi – Isaya 59:2.

Mungu alimpulizia PUMZI mwanadamu akawa nafsi hai lakini baada ya Dhambi Mungu hakumuona tena Adamu (alishakufa kiroho), ile pumzi ilikua imetoka, ndio maana Mungu akaahidi- atatia Roho yake na Mtu ataishi tena – Ezekieli 37:14.

c.       MAHUSIANO:- Mungu alianzisha Mahusiano, baada ya Dhambi mahusiano yakavunjika mpaka Dhambi ishughurikiwe na baada ya Dhambi kushughurikiwa mwanadamu anapewa utukufu tena na hatimae MAHUSIANO YALIYOVUNJIKA yanarejeshwa.Mahusiano haya tunaonjeshwa tukiwa hapa Duniani lakini Mahusiano kamili yatakua Mbinguni – Ufunuo 21:3-7, iko hivyo kwasababu Mahusiano ya Mungu na Adamu yaliendeshewa kwenye MASKANI YA EDENI, hapa Duniani hakuna Edeni, ndio maana Yesu akasema anakwenda kuandaa mahali – Yohana 14:2-3.

Licha ya Mungu kuahidi zawadi ya MASIHI na ROHO MT, pia aliahidi MAHUSIANO kurejeshwa, sharti likiwa ni kusamehewa Dhambi kwanza(kwa Yesu) na kupewa nguvu (Kwa ROHO MT), baada ya hapo Mwanadamu anaanza kuonja Mahusiano ya Mbinguni akiwa hapa Duniani – Mathayo 6:10. Mungu aliahidi kurejesha Mahusiano kwa kufanya Maskani yake kuwa katikati ya Wanadamu – Walawi 26:12, Ezekieli 27:37 “Mungu anakua Mungu wao na Watu wanakua watu wake”.

4.       HITIMISHO
·         Kuanzia sura ya 4 ya kitabu cha mwanzo mpaka malaki, kumejaa ahadi za ujio wa Masihi,ujazo wa Roho MT na urejesho wa Mahusiano, vitabu vya Injili vinaonyesha utimilizo wa Ahadi zilivyoahidiwa na Mungu-Yohana 4:25-26, 11:27. Nyaraka za mitume zinathibitisha utimilizo wa Ahadi – Mdo2:39, 13:23 na Efeso 2:22.Hivyo LEO hii tunaweza kudai kile kilichoahidiwa na kutimizwa na Mungu.
·         Kwanini Mungu anafanya haya yote? – Kwasababu ANAMPENDA Mwanadamu sana.

·         Hizi Zawadi zilizoahidiwa ndio zinaitwa EPANGELIA  na ndio mpango mkuu wa Mungu.

by 0753 011 774

No comments:

Post a Comment