Saturday, August 16, 2014

Apostle Eliya Simon 0717 267676

KUWA ROHONI?

Kuwa Rohoni ni kuwa na Daiolojia na Mungu. Daiolojia ni mazungumzo baina ya pande mbili, nikimaanisha Mungu na Mwanadamu. Tuangalie daiolojia Agano la Kale na Jipya.

A. AGANO LA KALE
Agano la Kale Mungu alizungumza na Wanadamu kwa njia mbalimbali, Mgawanyo wangu wa daiolojia na Mungu nimeugawanya kwa kuzingatia idadi ya wahusika.

1. Moja kwa moja na mtu binafsi (wachache)
a. Ndoto – Danieli 2:19
b. Maono – Ezekieli 1:1
c.Ana kwa ana – Kutoka 33:11, Hesabu 12:7-8

2. Kupitia Mtu mwingine(wengi)
a. Kuhani (Urim, Thumimu na Naivera) – Kutoka 28:30-31,1 Samweli 28:6
b. Unabii – Kumbu Torati 18:18

3. Kupitia Kitu(Kiumbe) kingine
a. Punda – Hesabu 22:28
b. Samaki – Yona 2:10
c.Kiganja – Danieli 5:5-6
d. Malaika – Kutoka 33:2a

B. AGANO JIPYA
Agano Jipya Mungu ameboresha Daiolojia, ni kinyume cha Agano la Kale. Lakini bahati mbay wahusika wa Agano Jipya hawapo makini ukilinganisha na wale wa Agano la Kale.

1. Moja kwa moja na Mtu binafsi (wengi)
a. Yesu – Ebrania 1:1-2
b. Roho Mtakatifu – Ufunuo 2:7, Matendo 13:2
c. Kuwa Rohoni – Ufunuo 1:10

2. Kupitia Mtu mwingine(wachache)
a. Nabii – Matendo 11:27-28
b. Malaika – Matendo 10:3-4

C. KIZAZI  KIPYA -- Zaburi 24:6
-Pamoja na njia zote nilizozitaja hapo juu,bado Mungu anaweza akazungumza na Mwanadamu kwa njia yoyoyte na kaktumia chochote. Mungu hana mipaka, vitu vyote ni watumishi wake.

Njia zote za Mwanadamu kuongea na Mungu au Mungu kuongea na Mwanadamu ni nzuri lakini iliyo bora kuliko zote ni kuongea kwa kupitia Yesu kwa njia ya Roho Mtakatifu, wewe utatakiwa kuwa rohoni ili uwe na Daiolojia.

Ungependa kuwa rohoni?

........HOSE.........................THE BEST HAS COME............

No comments:

Post a Comment