Saturday, January 18, 2014

HUYO NDIYE MUIGIZAJI BRIAN DEACON ALIYEIGIZA KAMA "YESU" NA ANACHOKIFANYA KWA SASA KATIKA MAISHA..!!




                                                                John Honore's photo.  John Honore's photo.
                                     

Brian Deacon ndio jina lake mwigizaji 


huyo ambaye ni



 mwingereza aliyezaliwa mnamo tarehe 13/02/1949 huko 


Oxford nchini Uingereza akiwa ni mtoto wa pili katika familia 


yao baba yake akiwa fundi makenika na mama yake akiwa ni


 nesi. Ndoa yake ya kwanza na Rula Lenska ilivunjika ambapo


 alizaa na mkewe huyo binti yao aitwaye Lara Deacon,ndoa


 yake ya pili alioana na mwanamama Natalie Bloch mnamo


 mwaka 1998 mpaka sasa wapo kwenye ndoa hiyo.



Brian Deacon ndani ya filamu ya ''JESUS'' Aliigiza filamu ya


 Yesu ambayo pia ilimfanya aokoke mara baada ya kuitazama


 akiwa na miaka 30,baada ya kupita kwenye mchujo mkali wa


 waigizaji zaidi ya elfu moja ambao walifanyiwa mahojiano


 huku 260 wakijaribishwa kuigiza(screen test)kuona kwamba 


wanafaa akiwa ni mwingereza pekee kati ya waigizaji Waisrael


 walioingia kwenye usaili huo akiwa chini ya kampuni iitwayo 


New shakespears ambako alikuwa akifanya sanaa za 


majukwaani na uigizaji. Brian Deacon miaka iliyofuatia baada 


ya kuigiza kama Yesu.Amesema kabla ya kuchaguliwa mtihani


 wake wa kwanza ulikuwa kutoka kwa wakala wake 


aliyemvunja moyo kwakumweleza hadhani kama 


yeye(Brian)atafaa kwenye kumwigiza Yesu,lakini anasema


 alifanikiwa,baada ya hapo akawa na wakati mgumu kutoka 


kwa watu ambao kila mmoja alikuwa anajaribu kumweleza 


jinsi anavyotakiwa kuigiza,sauti yake na mambo


 mengine,ingawa yeye alisema nitatumia sauti yangu na 


maelezo kutoka kwa muongozaji.Amesema wiki tatu kabla 


hawajaanza kurekodi filamu hiyo alisoma kitabu cha Luka 


mtakatifu zaidi ya mara 20 kwakuwa filamu hiyo imenukuliwa


 kutoka kitabu hicho ambapo Brian amesema kusoma kwake 


kulimpa nguvu sana na moyo wa kuigiza filamu hiyo na


 kuweza kumfahamu vyema Yesu kuwa ni mtu wa aina


 gani.watu wakiangalia filamu ya Yesu ambayo bwana Brian 


Deacon ni mwigizaji mkuu.Katika miezi saba waliyochukua 


kuigiza filamu hiyo Brian amesema,walikuwa wanaigiza kwa 


masaa mengi kuanzia saa kumi za alfajiri mpaka mwisho wa


 siku kiasi kwamba wakati mwingine aliwaambia wenzake 


kwamba wamsaidie kwani amechoka sana hajui kwamba


 angeweza kuigiza kwa siku hiyo lakini anasema alikuwa 


anashangazwa na nguvu za ajabu alizokuwa akizipata na


 kuendelea kuigiza ingawa wakati huo nasema alikuwa


 mkristo jina wa kanisa katoliki,alikuwa anauwalakini kuhusu 


mafundisho na huduma ya Yesu kwa ujumla,siku moja wakati


 anaigiza alikuwa anawaombea watu mara mwanamke mmoja


 alishika mkono wake kumbe alikuwa na mapepo alimuombea


 na mapepo yalimtoka mwanamama huyo. Siku nyingine


waliokuwa wakiigiza kama wanafunzi wa Yesu wapatao 12


 wakiwa ndani ya basi walikuwa wamepanga kugoma


 kutokana na malipo waliyokuwa wakipata cha ajabu Brian


 anasema director alikuja kumuomba yeye(Brian)azungumze 


nao warejee kazini akashangaa akamwambia mimi sio Yesu ni


 Brian Deacon,akaamua kuzungumza nao,baada ya masaa 36


 walikubali kurudi kuendelea na kaziAmesema mtihani 


mwingine ni siku alipokuwa hotelini Tel Aviv ghorofa ya 18 


usiku mara kukawa na moto hotelini hapo baada ya


 mwingereza mmoja aliyekuwa akivuta sigara kusahau 


kuizima hivyo kusababisha moto,lakini anasema bahati nzuri


 hakuna aliyejeruhiwa ila walifanya kazi siku inayofuatia muda


 mrefu bila muongozaji kujali kwamba hawakulala vyema 


usiku.Amesema siku hiyo mmoja wa waigizaji anayeitwa Tom


 Panella alianzisha mada kwa kusema moto uliokuwa


 umetokea ni hila za shetani,na kusababisha mjadala wa


 muda mrefu ni vipi shetani anahusishwa kwenye swala hilo


 lakini jibu likawa,shetani hataki filamu hiyo irekodiwe ndio


 maana analeta hila zake.haikuwa kazi rahisi kurekodi filamu


 hiyo na pia si ujuzi wa kufurahia,baada ya 


kumaliza kurekodi kwa takribani miezi 18 ilianza kuonyeshwa


 kwa baadhi ya watu na ndipo hata yeye kwa mara ya 


kwanza akaona ni 


kwa jinsi filamu hiyo ilivyonanguvu,ukweli na kugusa mioyo


 ya watu. Baada ya filamu hiyo Briana anasema alirudi kuigiza


 majukwaani na kwenye runinga, ambapo kwa miaka zaidi ya 


30 sasa tangu kutoka filamu ya Yesu tayari imetazamwa na 


watu zaidi ya bilioni tatu katika nchi 233(kwa takwimu za


 mwaka 2001),zaidi ya watu milioni 117 waliamua kubadilisha


 maisha yao na kumpokea Yesu,filamu hiyo ambayo


 ilitengenezwa chini ya Campus Crusade for crusade ambao


 kwasasa wanaitwa Life Ministry pia nchini Tanzania wapo


 chini ya mkurugenzi Dismas Shekhalage.ambapo tayari 


imetafsiriwa katika lugha zaidi 500 huku nyingine zaidi ya 200


 zikiwa njiani kutafsiriwa. Brian anawaambia watu kwamba


 yeye ni mwigizaji tu na sio Yesu kama watu wengine na


 kuwataka watu hao kujua hivyo ambapo anasema


 ameendelea kupata barua mbalimbali za kumpongeza na


 kumshukuru kwa kazi nzuri aliyofanya kwenye filamu


 hiyo,ambapo kwa upande wake anasema anayo nakala ya 


filamu hiyo kwenye maktaba yake nyumbani kwao


 Uingereza,ambapo kwa takribani miaka 20 filamu hiyo 


imekuwa ikitazamwa duniani kote na kubadilisha maisha ya


 watu. kati ya filamu alizowahi kushiriki ni pamoja na A zed &


 Two Noughts ya mwaka 1985,The Feathered Serpent ya 


mwaka 1976-1978 na Tamthilia ya iitwayo Lillie iliyoigizwa


 mwaka 1978.

No comments:

Post a Comment