Tuesday, January 21, 2014

USIJIFUNZE KWA WALIOFANIKIWA ??????


NAMNA YA KUWA TAJIRI MKUBWA

YALIYOMO
1. UTANGULIZI    2. JIFUNZE KWA WALIOFANIKIWA
3. USIJIFUNZE KWA WALIOFANIKIWA   4. HITIMISHO

ANDIKO KUU: Ezekieli 28:1-7,11-13

1.UTANGULIZI
- Andiko kuu linazungumzia watawala wawili, kuna mkuu wa Tiro-Ezek 28:1-7, huyu ni mwanadamu, na Mfalme wa Tiro-Ezek 28:11-13, huyu ni mkuu wa anga(shetani). Hawa wawili walikuwa na mahusiano, mwanadamu akiwa kama kawaida yake KIBARAKA, hakuna mtu atakaye kuambia mahusiano yake na mapepo, mpaka siri zifichuliwe.

-Kila tajiri mkubwa hapa Duniani, anayo siri moyoni mwake ya huo utajiri, na ukishasikia SIRI, ujue ni Siri kweli. Kwakifupi hakuna aliyezaliwa masikini, kila mmoja wetu amezaliwa kuwa tajiri mkubwa, tatizo ni namna ya kufanya huo utajiri uwe halisi..

-Mafanikio na utajiri ni AIDIA, ni WAZO. Wewe msomaji unahitaji kitu kimoja tu uwe tajiri wa kutupwa, otea nini !! AIDIA. Swali linakuja, nitapata wapi Aidia ili niisimamie hiyo Aidia niwe tajiri?. Apostle Eliya atakusaidia kufichua hii SIRI ya AIDIA ya matajiri na waliofanikiwa. Twende pamoja……………..


2. JIFUNZE KWA WALIOFANIKIWA

-Mafanikio ni hali ya kutokuwa muhitaji, utajiri ni hali ya kuwa huru ki-fedha. Kwa hizi maana za mafanikio na utajiri utagundua kuwa mafanikio ni muhimu kuliko utajiri kwasababu utajiri ni sehemu mojawapo ya mafanikio. Vyote viwili vinahitaji AIDIA.

- Huu msemo umekuwa maarufu, na wengi wameunukuu kwa nyimbo au misemo,kwamba “jifunze kwa waliofanikiwa, usijifunze kwa walioshindwa”. Sijajua kama wanajua huu msemo umebuniwa na nani, mimi ninashauri usijifunze kwa waliofanikiwa.

-Njia rahisi ya kujifunza kuhusu Mafanikio na utajiri ni;
(a) kuwatambua waliofanikiwa (b) kujifunza kwao na (c) Kufanya maamuzi.

-Kabla sijaelezea hivyo vipengele vitatu, naomba utambue kuwa Mwanadamu ana asili mbili, yakwanza ambayo ina nguvu ni asili ya rohoni, na yapili ni asili ya mwilini. Roho ya mtu ndio inayochukua mambo ya rohoni na kuipatia nafsi, na nafsi inaungoza mwili. Ninapokwenda kueleza vipengele vitatu utambue kuwa yanayooneka mwilini ni matokeo.

  1. WATAMBUE WALIOFANIKIWA
-Ili kuwatambua waliofanikiwa, nitatumia uzoefu wa mwanadamu wa kujifanikisha, historia huwa inajirudia, Aidia za mafanikio za watu wa zamani ni sawa kabisa na Aidia za ulimwengu huu isipokuwa tofauti ni namna ya kuendesha na kusimamia hizo Aidia.

-Nitataja watu 5 ambao walifanikiwa sana, na mafanikio yao yaliweza kubadirii tamaduni na maisha ya ulimwengu wote. Kwa kupitia hawa matajiri 5, utagundua asili ya mwanadamu na vyanzo vya Aidia ya mafanikio yao.

-Watambue Waliofanikiwa kupitiliza:
1. NEBUKADREZA, 2. DARIO NA KORESHI
3. SULEMANI, 4. ALEKZANDA, 5. AGASTUS

  1. JIFUNZE KWA WALIOFANIKIWA
- Hebu tuone hawa watu 5 walivyofanikiwa, naomba utambue kwamba mwanadamu hajabadirika, asili ya hawa 5 ndio uliyonayo wewe na kila unayemjua kuwa kafanikiwa.

1. NEBUKADREZA
-Alikuwa Mfalme wa Babeli, utajiri na mafanikio yake kila mtu Duniani aliyatambua, aliweza kuishi anavyotaka, kila aliyempinga aliweza kumuangamiza kwa uweza wa nguvu za mafanikio yake.

-Chanzo cha Mafanikio yake – Soma DANIELI 3:1-7. Kama mafanikio ya Nebukadreza yangekuwa ya kawaida asingetengeneza sanamu, hapa utagundua kwamba Mfalme alikuwa na mahusiano na ulimwengu wa kiroho wa shetani. Baadae akatawala mtoto wa Mfalme, tazama nayeye alichokifanya,DANIELI 5:3-4. Hii ndio asili ya Mwanadamu na haijabadirika .

2. DARIO NA KORESHI
- Dario alikuwa mfalme wa Umedi. Koreshi alikuwa mfalme wa Uajemi, Hawa wafalme walifanya ushirika Kung’oa mafanikio ya Babeli, mafanikio yao yalitambulika kila kona ya Duniani .

-Chanzo cha Mafanikio yao- (Dario) DANIELI 6:7- Alikuwa na miungu yake ambayo ilimdanganya kuwa yeye mfalme angeweza kuwa mungu, (Koreshi) DANIELI 10:13 huyu jamaa alikuwa na mahusiano na mkuu wa anga lake, yeye alikuwa ni kibaraka tu.

3. SULEMANI
-Alikuwa Mfalme wa Israeli, kama kawaida, mafanikio yake yalipita viambaza vya Dunia yote.

-Chanzo cha Mafanikio yake- 2 NYAKATI 1:7-12, Umejifunza nini? Umeona chanzo cha AIDIA ya mafanikio ya Sulemani?. Hapa tumeona chanzo kingine cha mafanikio,ni JEHOVA

4. ALEKZANDA
-Alikuwa Mfalme wa Ugiriki, mafanikio yake yalitawala Dunia yote

-Chanzo cha mafanikio yake- Gaya ndiye mungu wa wagiriki, wanaamini kuwa ndiye aliyeumba na ndiye mwenye milki ya kila kitu. Aidia za mafanikio zilitoka kwa huyu mungu Gaya wa wagiriki.

5. AGASTUS
-Alikuwa Mfalme wa Rumi, Mafanikio yake yalienea Duniani kote, mpaka leo tunaweza tukaona mabaki ya mafanikio ya Rumi(ROMA).

- Chanzo cha Mafanikio yake; alikuwa na miungu mingi, lakini mungu aliyekuwa maarufu ni MALIKIA WA ULIMWENGU, ambaye miaka hii wanamuita MAMA WA MUNGU(mama maria), lakini huyu mungu siyo yule Mungu wa Sulemani.

  1. FANYA MAAMUZI
- Wataalamu walisema usifanye maamuzi kama huna habari(informations) kamili, nimejaribu kukuonyesha hapo juu vyanzo vikuu vya waliofanikiwa, kumbuka asili ya mwanadamu ya kutafuta msaada wa mafanikio haijabadirika.

- Hebu nivigawe vyanzo vya mafanikio kabla hujafanya maamuzi, nimevigawa vyanzo katika makundi matatu;
   1. Mtu Binafsi  2.Shetani na 3.Mungu(Yesu)

-Kama tukiwakusanya waliofanikiwa na kuwagawanya katika makundi, bila shaka tunapata makundi matatu, mgawanyo huu ni kutegemea vyanzo vya mafanikio yao:

1. Mtu Binafsi
-Chanzo cha mafanikio hapa mtu BINAFSI. Hapa mtu anatumia Elimu,uzoefu,mipango kabambe,juhudi,kuwekeza,mikopo, nk. Watu wanaotumia hii njia ki-ukweli huwa hawana mafanikio sana, wakijitahidi sana wataweza kula vizuri na kupata ka-usafiri na ki-nyumba cha kuishi.Hawana uwezo wa kuikopesha serikali,siku zote wao hukopa.

2. Shetani
-Chanzo cha mafanikio hapa ni SHETANI, Hili kundi wanapata muongozo na mipango kutoka kwa Shetani, juhudi binafsi zinakuwa ni za pili. Kundi hili limefanikiwa sana kuliko la kwanza kwasababu wanaye msaidizi wa kuwapa ramani.

3. YESU
- Chanzo cha Mafanikio hapa ni Mungu(Yesu), Mipango na aidia inatoka kwa Yesu, nikimaanisha Yesu ndiye anayempa wazo mtu afanye nini, lakini usimamizi wote anakuwanao mwanadamu. Kundi hili ndio lilipaswa lifanikiwe kuliko makundi yote mawili ya hapo juu, kwasababu Yesu ananguvu kuliko Shetani.


►Kwa ujumla tumejifunza kuwa AIDIA za utajiri mkubwa upo ulimwengu wa roho, na ulimwengu wa roho ni Mungu au Shetani tu,hakuna katikati, naomba niseme kwamba mwanadamu ni dhaifu mno, hana lolote wala si chochote, tumezuiliwa na MUDA(time) na NAFASI(space).

- Pamoja na kwamba Mungu ana nguvu kuliko Shetani lakini watu wanaomwamini Yesu ndio walio masikini wazuri,tatizo ni nini? Hili swali linamajibu mawili, labda tatizo lipo kwa hawa wanaomwamini au mtazamo wa Mungu kuhusu mafanikio upo tofauti.

►Kati ya hao waliofanikiwa watano, tumeona mmoja kati yao ndiye aliyekuwa na chanzo sahihi cha Aidia, kwahiyo kama ukienda kujifunza kwa hao wane maana yake watakuingiaza chaka. Usijifunze kwa waliofanikiwa tu kwasababu watakupoteza.

3. USIJIFUNZE KWA WALIOFANIKIWA

Kwanini watoto wa Mungu wengi ni masikini???????

- Nimesema hapo juu kuwa kuna majibu mawili:
(a)Tatizo la watoto wa Mungu, au (b) Mtazamo wa Mungu wa Mafanikio ni tofauti na tunavyodhani.

A.WATOTO WA MUNGU
-Nimegundua wakristo wengi tumeshindwa kuifichua hii siri ya kupata Aidia ya mafanikio. Baada ya kufanya utafiti wa mafanikio, nimegundua kitu nyeti sana, kwamba AIDIA ya mafanikio anayo Mungu ambayo yupo rohoni, na mwanadamu anaihitaji hiyo AIDIA lakini yupo mwilini, kwahiyo mwanadamu anahitaji MAWASIRIANO kati yake na Mungu.

-Mawasiriano ni KUSIKIA, KUONA. Kusikia nini? Sauti ya Mungu. Kuona nini? Maono na kuota ndoto. Hapa tu ndio tatizo. Wakristo wengi hawajui kuwa Mungu anaongea mpaka sasa na hivyo hawakotayari kusikia Mungu anachowaambia, hawataki kuingia rohoni, wanapenda mambo ya mwilini na kujitahidi.

- 2 NYAKATI 1:7-12. Hapa utagundua Mungu anaongea na Sulemani katika ndoto/maono na Sulemani ANAMSIKIA Mungu, kisha ANATII alichokisikia. Baada ya kupata AIDIA toka kwa Mungu kwa kusikia ndipo unapoweza kuanza juhudi binafsi.

B.MTAZAMO WA MUNGU
-Mtazamo wa Mungu kuhusu mafanikio ukoje? Ili kujibu swali hili utapaswa uangalie ni yupi ambaye Mungu alimfurahia. Tukishampata mtu ambaye Mungu anamfurahia ndipo tutakapoangalia maisha yake kisha tutajua mtazamo wa Mungu kuhusu mafanikio. Hapa nitachukua watu watatu :1. SULEMANI,  2.NEBUKADREZA, 3. YESU.

SULEMANI- 1FALME 11:9- Mungu anamghadhibikia Suleimani, aliyekuwa tajiri sana, na utajiri wake Mungu ndiye aliyempa, 2NYAKATI 9:22-24.

NEBUKADREZA- soma DANIELI 4:22, 25.Mafanikio ya Nebukadreza yangefutiliwa mbali na Mungu kwasababu alishindwa kumtambua Mungu.

YESU- Mathayo 17:5. Mungu anasema “ …NINAYEPENDEZWA NAYE…” Kwenye Biblia kuna watu wawili ambao Mungu alizungumza nao maneno kama haya, ni Musa-HESABU 12:6-8, na Daudi-1SAMWELI 13:14, lakini hawa wote hawafui dafu kwa Yesu.

►Umejifunza nini? Kumbe utajiri sio kipimo kizuri cha mafanikio, tulipochukua wale wafalme 5,tuliona sulemani ndiye aliyestahili lakini baada ya kumchukua Sulemani na kumlinganisha na Yesu tumeona hafai kabisa. Hivyo mtu ambaye tungepaswa kujifunza kwake ni…….YESU, kwanini? Kwasababu Mungu amependezwa naye.

YESU
-Msomaji, unataka kufanikiwa? Jifunze kwa Yesu, yeye alikuwa amefanikiwa, akapoteza mafanikio yote kisha akayapata yote. Ndio maana mwanzo nikasema usijifunze kwa waliofanikiwa bali jifunze kwa waliofanikiwa kwanza, harafu wakaishiwa kisha wakafanikiwa tena.

=Ngoja nikupe siri, Yesu hakuwa tajiri lakini hakuwa mhitaji, nahii ndiyo kanuni ya mkristo sahihi, kumbuka utajiri ni zawadi ya Mungu kwakuwa umempendeza, angalia hapa anavyomwambia Ibrahimu, baba wa Imani –MWANZO 15:1. Naomba uelewe kwamba kuna mtoa utajiri na utajiri, wakristo wengi wanahangaikia utajiri, lakini hawana haja ya mtoa utajiri- Mathayo 6:25

-Kilichomfanikisha Ibrahimu, Musa, Daudi na Yesu ni kuipenda sheria ya kwanza, unajua ni ipi?-MATHAYO 22:37. Usisahau kuwa Mungu ana wivu, hapendi kuona mtu anampenda kwasababu yeye ana mali au mtu anapenda mali kuliko mtoaji.


4.HITIMISHO

-Tafuta kitabu kilichoandikwa na tajiri yeyote kuhusu utajiri, kuna maneno yafuatayo hutayakosa: DESIRE, PLAN, PERSISTANCE, DECISION, INVEST, DETERMINATION, ACHIEVE, GOAL, MANAGE, COOPERATION, na maneno kibao watakupa, unajua siri ni nini? Hawakwambii, wengi wao wanamahusiano ya moja kwa moja na shetani, kama huamini fanya kila wanachoshauri uone, ukishashindwa fuata njia yangu, mimi ndo nimeshaanza, kwasababu nimegundua siri.

Maneno yote hapo juu ni juhudi binafsi, yanatakiwa yafuate ukishapata AIDIA toka ulimwengu wa roho yaani Mungu au shetani, nakushauri chagua Mungu, na ukishagua Mungu kubali kuendanan na mtazamo wa Mungu sio wako wewe.SIKIA sauti ya Mungu, pia ona Maono MWANZO 12:6, nnje ya hapo utaniwia radhi jamani.

…….Remembe…………THE BEST HAS COMES…0717 267676

No comments:

Post a Comment