Tuesday, November 19, 2013

SABATO KWA WALOKOLE ? NDIYO

By Apostle Eliya -0759 166 934


SABATO KWA WALOKOLE ? NDIYO

YALIYOMO;- 1.UTANGULIZI  2.SABATO NI LAZIMA  3.HITIMISHO

LENGO LA FUNDISHO
- Kuonyesha ulazima wa sabato kwa kila mtu anayemwamini Yesu.

ANDIKO KUU:- Waebrania 4:1 Basi ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha, na tuogope mmoja wenu asije akaonekana ameikosa

1.UTANGULIZI

- Sabato ni siku ya saba, ambayo ni Jumamosi.ni siku ya raha.
- Mungu anataka kila mwanadamu aishi sabato, ni lazima na milele.
- Makuhani, manabii, wafalme, mitume 12 na Waizraeli wote walishika sabato kwa uaminifu mpaka leo

- Kumekuwa na dini nyingi sana miaka hii, makanisa mengi, huduma nyingi, Imani mbalimbali, wana-theolojia wengi,shule za Biblia zimekuwa nyingi, makongamano, mikutano na semina nyingi sana. Lakini makundi yote haya yanatakiwa yaingie Sabatoni, ni MUHIMU.

2.SABATO NI LAZIMA
Sabato ni zaidi ya siku, ni zaidi ya kupumzika nyumbani, ni zaidi ya kwenda kanisani. Sabato inamaana nyingine ya muhimu zaidi kuliko zote. ISAYA 58:13

A) NANI MWANZILISHI WA SABATO ?

- Mungu ndiye muanzilishi wa Sabato, sio Waisraeli wala Wasabato, Mungu anajali sabato kuliko zaka, au matoleo yoyote unayoyajua, sabato ni sehemu 1 kati ya 7 lakini zaka ni sehemu 1 kati ya 10. Sabato ni amri ya 4 lakini zaka na sadaka hazimo kwenye amri. KUMB TORATI 5:12

- Mambo mawili ambayo Mungu aliyafanya siku ya 7 a) Kupumzika kuumba mambo yanayoonekana(ulimwengu wa mwili) MWANZO 2:1 na b) Kuanza kufanya kazi ya kuumba mambo ya rohoni(ulimwengu wa kiroho) au Edeni MWANZO 2:8. Yote haya yalitokea katika siku moja,ya sabato, kupumzika na kufanya kazi tena.Iliitwa sabato ya Bwana TORATI 5:14, lawi 25:4

- Nakubaliana na sayansi inayosema Dunia ina umri wa miaka bilioni 13.7, kila siku moja katika uumbaji iliwakilisha jumla ya miaka kadhaa ZABURI 90:4, kwa mujibu wangu, mpaka mwaka huu 2013 upo ndani ya ile siku ya 7 ya uumbaji MWANZO 2:2-3. Huu ni mtazamo wangu tu.

B) SABATO ILIMAANISHA NINI KABLA YA YESU ?

- Wana wa Israeli ndio warithi hasa wa kushika sabato ambayo Mungu aliianzisha kisha akamfundisha Adamu na Eva,ingawa sabato kabla ya Dhambi(anguko)na baada ya Dhambi kuingia Duniani ni tofauti lakini Mungu alitaka ishikwe KUTOKA 20:8. Kuingia sabato na kushika sabato ni tofauti, wao walishika.

Sabato ya Adam na Eva kabla ya anguko ---- Adamu hakushika sabato, aliishi sabato, Siku zote ilikuwa ni sabato,hakuna ibada wala siku ya ibada, hakuna hekalu, hakuna makuhani, hakuna sheria wala torati, Mungu akaona kila kitu ni chema MWANZO 1:31. Adam alichotakiwa ni kuitunza tu bustani MWANZO 2:15.

Sabato baada ya Dhambi kuingia(anguko) ---- Sabato ikawa na dosari, badala ya kuishi kisabato wakatakiwa kuishika sabato TORAT 5:15e. Dhumuni likageuka badala ya kufurahia Edeni na uumbaji wote ikawa kufanya Upatanisho WALAWI 16:31, ikamlazimu Mungu asipumzike tena, Mungu akaweka makuhani, sheria, hekalu, torati na kafara ambayo hayakuwa na umuhimu wowote.- WAEBRANI 8:5, 10:1, KUTOKA 25:40.

- Ukisoma vizuri kuhusu sabato utagundua kuna mambo mawili kulwa na doto ambayo mara zote yalijitokeza wakati wa sabato, cha ajabu haya mambo mawili yapo kinyume kabisa WALAWI 23:32;
     1. Kujitesa nafsi  2. Kustarehe

Mungu alitaka Waisraeli wajifunze nini ?,
1.Kujitesa nafsi -=- kwamba wajitese nafsi zao kwasababu waliasi,wakapoteza haki zao za kumiliki bustani ya Edeni(ulimwengu wa kiroho). Kwahiyo Mungu na Mwanadamu wote walikuwa wakiiharifu sabato MATHAYO 12:5, ambapo sii sahihi. Hivi unajua kuwa kusamehe dhambi na kusamehewa dhambi ni kazi kubwa ?
2.Kustarehe -=-  Kwamba wajifurahishe, lakini furaha hii haikuwa halisi ilikuwa ni kwa ajili ya kuwakumbusha mambo mawili; kuwa kabla ya Dhambi maisha yalikuwa ya pumziko, na pia baada ya Yesu kutakuwa na pumziko MATHAYO 11:28

- Siku ya sabato waisraeli walitakiwa kutembea umbali wa mtupo wa jiwe, maana yake kazi wangefanya kidogo sana lakini matokeo yangekuwa makubwa sana, ni kama teknologia inavyofanya kazi wakati huu.

C) SABATO ILIKUWAJE WAKATI NA BAADA YA YESU ?

- Msomaji wangu naomba ujue kwamba KIPINDI cha BAADA ya anguko na KABLA ya Yesu mambo mengi sana hayakuwa halisi, Mungu aliichagua Israeli, makuhani,hekalu na Torati kutunza kumbukumbu, lakini hayakuwa na uhalisia(kivuli).EBRANIA 8:5

- Yesu hakuwa na tatizo na kushika sabato kwa waisraeli, wala makuhani,wala torati, wala hekalu. Bifu la Yesu na hawa jamaa ilikuwa ni UFAHAMU wao kuhusu sabato,ukuhani, hekalu na torati. Hawakujua kwanini Mungu aliamua achague siku moja(Jumamosi) iwe siku ya sabato.- MATHAYO 12:1-8, 23:16-22, LUKA 6:6-11

- Hata mitume nao hawakuwa na shida juu ya siku ya sabato, walishajua dhumuni la sabato. Ngoja nikupe huu mfano, chungu cha udongo kina almasi zimejaa ndani, kipi cha muhimu hapo, chungu au kilichopo ndani ya chungu ? Ndio utofauti wa Yesu na wayahudi.- MDO 13:42-44

- Yesu anapojiita Bwana wa sabato haimaanishi kuwa yeye ndiye anayejali sana kushika sabato, hapana, alimaanisha kuwa yeye ndiye anaeishi kisabato kwa usahihi. Kabla ya Yesu hakuna aliyeshika sabato 100% - YOHANA 5:30, LUKA 6:12

D) SABATO IWEJE NYAKATI ZETU ?

- Ili uelewe sabato nyakati zetu, turejee madhumuni mawili ya sabato ;-   1.Kujitesa;- Yesu ameshateswa, dhambi zote zimefutwa ISAYA 53:11a.
 2. Kustarehe tunatakiwa kuiishi sabato kama kabla ya anguko. Kwa kuishi kisabato tunautangazia ulimwengu kuwa kuna sabato tutakayoiishi milele inakuja. WAEBRANIA 4:11

- Sabato ni kutumia mambo ya kiroho kuendesha mambo ya mwilini       1 KORIN 2:14, sabato ni kuwa na vipawa na karama za Roho Mtakatifu RUMI 8:14. Sabato ni kupumzika kutumia mwili na kuanza kutumia Roho Mt. Sabato ni kusikiliza kila siku, kutii kila siku na kutenda kila siku- MATHAYO 7:24

E) JE, UPO TAYARI KUISHI KISABATO ?

- Sabato ni lazima hapa Duniani kwa mlokole na Mroma na Muislamu na Wanaojiita wasabato. Kama umechoka kuonewa na kuwa omba-omba, ingia kwenye sabato, kama unafurahia haya maisha sabato haina hajakwako MATHAYO 7:13

- Walokole wote ambao hawatembei katika mtembeo wa Roho mt, namaanisha wasiokuwa na vipawa na karama za Roho mt hawapo katika sabato, bado wanahangaika na kushika sabato. Ikumbukwe kuwa sabato ni lazima. Kwa hali hii, ni afadhali ya msabato anayeshika siku kuliko mlokole asiyekuwa rohoni ingawa wote wawili wameingia chaka - MATH 7:16

- Wasabato wote ambao hawana Roho Mt, na karama na vipawa, hawapo katika sabato na hawastahili kuitwa wasabato, mbaya zaidi wanamhuzunisha Roho Mt EFESO 4:30. Chochote kinachofanyika kanisa lolote bila Roho Mt ni kumdharau Roho Mt.YOHANA 15:5

F) UTAMJUAJE MSABATO HALISI ?

- Kila mwanadamu anaejali maisha ni lazima awe msabato(sio mjumamosi). Kumjua msabato halisi ni rahisi sana, anatoa unabii, anafanya miujiza na uponyaji na ishara,anapambanua roho, anatafsiri na kunena kwa lugha, anafichua mambo ya siri(hekima, maarifa), ana imani ya yasiyowezekana, anaona maono, anaisikia sauti ya Mungu, anaweza kufukuza mapepo, anafufua wafu. Nk MDO 1:8, 10:38, 1KORIN 12:8, ISAYA 11:2-3

- Acha kutumia nguvu za kimwili, badala yake pumzika mwilini harafu fanya kazi ya nguvu rohoni, sabato ni kupumzika mwilini na kufanya kazi nzito rohoni EFESO 6:12. Wafuatao ni watu ambao wamejaribu kuonyesha maisha ya kisabato ;- TB JOSHUA, EUBERT ANGEL, PASTOR CHRISS, BENNY HINNY, IDAHOSA, MAKANDIWA, BOATENG, KAKOBE, GWAJIMA, MALISA, KULOLA, COVENANT,KATHRINE, ORAL ROBERT, YONG CHO, OYEDEPO, n.k. Hawa jamaa ndio wasabato na kila mkristo alitakiwa awe kama mmojawapo wa hawa ndugu.- MDO 8:29,39, 7:55

- Kwakifupi msabato halisi ni yule anaeishi maisha ya kiroho na kimwili kama ya Yesu au zaidi ya Yesu. Yesu ni mfano wa mtu anayetaka kuwa Msabato. Yesu hakuna alichokuwa anabuni katika huduma yake, mambo yote alielekezwa, naye alikuwa muaminifu kutekeleza. Hiyo ndio sabato, alisikia , alitii, alifanya, hii ndiyo sabato.- YOHANA 14:10b

G. ITAKUWAJE NISIPOINGIA SABATO ?

- Kabla sijajibu swali labda niseme kwamba anayefaidika hasa na sabato ni mwanadamu, kutokuingia sabato hakutakuzuia kwenda mbinguni, kwahiyo mbinguni utaingia hata kama haujaingia sabato hapa Duniani.

-Usipoingia sabato utaishi maisha ya misuri, utakula kwa jasho, ardhi itakuwa imelaaniwa kwako,utatawaliwa, tama yako itakuwa kwa mwingine, shambani kwako miba itamea, lakini mbinguni utaingia. Uchaguzi ni wako MWANZO 3:16-18, utakuwa kama mwana mpotevu LUKA 15:15-19

- Ipo sabato kuu naya milele inakuja, lakini kipindi hiki tumeruhusiwa kuonja utamu wa sabato inayokuja ya milele LUKA 11:2, utakuwa mjinga usipoonja, lakini ukishindwa, subiri ile inayokuja, lakini kubali kuishi hapa Duniani kwa Jasho. Usiwaseme vibaya walio elewa sabato LUKA 11:20-22, MATHAYO 6:9d, UFUNUO 21:1-2


3.HITIMISHO

- Kuwa msabato ni lazima, kama unataka kuwa msabato tekeleza mambo haya mawili kikamili;- a) Amini Injili kwa usahihi, b) Jazwa Roho Mt kikamilifu.

- Haya mambo mawili yamewashinda wasabato na walokole wengi. Mpaka sasa wachawi na waganga ndio wanao furahia sabato, sio wakristo. Mchawi kuingia rohoni ni rahisi lakini mlokole kasheshe, hii ni kuonyesha wachawi ndio wasabato wazuri.

………..Remember…………THE BEST HAS COMES………………

1 comment:

  1. MBONA HAPO KWENYE G, sehemu ya kwanza haujaweka aya umeweka maneno matupu? HAPO NAPO WEKA AYA inayo elezea hicho ulichoWEKA

    ReplyDelete