Saturday, February 15, 2014

it is well with my soul" / "Salama rohoni mwangu


Horatio Gates Spafford na Anna Spafford

Katika miaka ya 1860 Horatio aliishi na mke wake

 Anna Chicago,Marekani. Spafford alikuwa

 mwanasheria mkubwa aliyewekeza zaidi kwenye 

majengo (real estates). Maisha yalianza kubadilika

 mwaka 1870 ambapo mtoto wao pekee wa kiume

 alifariki kwa ugonjwa wa nimonia, Mda mfupi baadae

 janga la moto mkubwa wa Chicago uliteketeza 

sehemu kubwa sana ya mali zake.

Wakiwa na matumaini ya kupunguza maumivu

 waliyopata kutokana na matatizo yote,


Mwaka 1873 Spafford na mkewe walikubaliana

 kwenda Uingereza ambapo rafiki yake alikuwa ana

 hubiri injili.

Katika maandalizi ya mwisho kazi zilimbana Horatio, 

Akawaambia mke wake na watoto wake wakike 

wanne watangulie akiahidi kuwafuata haraka.

Ndipo jambo lisiloweza kufikirika likatokea, Boti 

aliyopanda mke wake na watoto wake ikapata ajali 

na watoto wake wote wanne walizama na kupoteza

 maisha, Mke wake pekee alipona nae baada ya

 kufika ufukweni akamuandikia note spaffors ikisema 

"Saved Alone, What shall I do?" yaani "Nimeokolewa

 peke yangu, Nitafanya nini?"


Horatio akiwa njiani kwenda kumfariji mke wake,

 akipita eneo ambalo watoto wake walizama na

 kupoteza maisha ndipo aliandika mashairi ya wimbo

 uliopata umaarufu sana mpaka miaka hii,

Wimbo unaitwa "it is well with my soul" / "Salama

 rohoni mwangu"

Haya hapa mashairi yake


When peace, like a river, attendeth my way,

When sorrows like sea billows roll;

Whatever my lot, Thou hast taught me to say,

It is well, it is well with my soul.

(Refrain:) It is well (it is well),

with my soul (with my soul),

It is well, it is well with my soul.

Though Satan should buffet, though trials should

 come,

Let this blest assurance control,

That Christ hath regarded my helpless estate,

And hath shed His own blood for my soul.

(Refrain)

My sin, oh the bliss of this glorious thought!

My sin, not in part but the whole,

Is nailed to His cross, and I bear it no more,

Praise the Lord, praise the Lord, O my soul!

(Refrain)

For me, be it Christ, be it Christ hence to live:

If Jordan above me shall roll,

No pain shall be mine, for in death as in life

Thou wilt whisper Thy peace to my soul.

(Refrain)

And Lord haste the day, when my faith shall be sight,

The clouds be rolled back as a scroll;

The trump shall resound, and the Lord shall descend,

Even so, it is well with my soul.

(Refrain)

Baadae Anna alibarikiwa na watoto watatu, Mmoja

 wa kiume ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka

 minne, na wakike wawili. Na baada ya mda walienda

 kuishi Israel na familia yake wakaanzisha kundi la

 kusaidia masikini huko Israel. 




Binafsi Siku ya leo wimbo huu umekua ukijirudia

 ndani yangu kila ninapotafakari matendo makuu

 ambayo Mungu amenifanyia hasa kwa kipindi hiki

 ambacho nimezungukwa na mambo mengi, siwezi

 kuwaza lolote Mungu ni muweza wa yote.

Chanzo: Injili Tanzania Blog

No comments:

Post a Comment