Tuesday, May 27, 2014

HALI YA MWIMBAJI WA INJILI NCHINI SI NZURI, YUPO CHUMBA CHA UPASUAJI SASA, MAOMBI YAKO MUHIMU

Maombi yako yanahitajika ili Mungu amponye mwimbaji wa muziki wa injili nchini Debora John Saidi ambaye hali yake inaelezwa kwamba si nzuri nasasa yuko chumba cha upasuaji hospitali ya Mwananyamala kuondolewa uvimbe mkubwa tumboni ambao umesababisha alie kwa maumivu makali.

Upasuaji wa kutoa uvimbe huo ulitarajiwa kufanyika kesho, lakini kutokana na maumivu pamoja na kilio kutoka kwa mwimbaji huyo imebidi kupelekwa chumba cha upasuaji mchana huu. Ambapo mchana wa leo baadhi ya waimbaji wenzake akiwemo Joshua Makondeko, Tumaini Njole walifika hospitalini hapo kumjulia hali. Mdau wa GK popote ulipo, sema neno la uponyaji kwaajili ya Debora

Debora akilishwa kabla ya kupelekwa chumba cha upasuaji.
Mungu akuponye Debora.



Joshua Makondeko akimnywesha maji Debora.

No comments:

Post a Comment