Tuesday, July 11, 2017

SOMO#3. KAINI, HABILI NA SETHI

SOMO#3. KAINI, HABILI NA SETHI

Andiko Kuu-Mwanzo sura yote ya  4
11.   KAINI, HABILI NA SETHI (Kabla ya Yesu)
1.       Adam na Hawa
·         Adam na Hawa walifukuzwa Bustanini (Maskani) kwasababu ya Dhambi, lakini Mungu aliwafanyia Upatanisho ingawa haukuwa mkamilifu kwasababu UTHAMANI WA MWANADAMU SIO SAWA NAWA MNYAMA, ndio maana mahusiano yao yaliendelea NJE ya Bustani (Maskani).
·         Adamu na kizazi chake chote kilishaingiwa na Kasoro, walikuwa na Sura ambili – Ya Mungu na Shetani, kwahiyo kila anaezaliwa kwa asili ni lazima afanye maamuzi ya KUCHAGUA, ama Mungu au Shetani.
2.       Kaini na Habili – Mwanzo 4:1-7
·         Adam na Hawa walipata watoto-Kaini na Habili wakiwa na Asili ya wazazi wao
·         Kaini alikuwa mtoto wa kwanza, mkulima, Mungu alimkataa yeye na Sadaka yake. Lakini Mungu alimtakabali Habili na Sadaka yake, alikuwa mtoto wa pili, mchunga kondoo. Swali- Kwanini Mungu amtakabali Habili na asimtakabali Kaini?
·         Sadaka waliyotakiwa kutoa ilikuwa ni sadaka ya UPATANISHO/KUFUNIKA DHAMBI/KUSITIRI DHAMBI, sasa sadaka yenye hii sifa ni sadaka yenye DAMU. Kaini alitoa sadaka nzuri lakini haikuwa na Damu kwani kinachofanya upatanisho ni Damu
·         Kaini alijibunia njia yake ya kufanya upatanisho kama Baba yake na Mama yake hii inaonyesha hakumuamini Mungu, lakini Habili alifuata njia ya Mungu ya KUUA KONDOO ili kufanya upatanisho, hii inaonyesha alimuamini Mungu na akahesaiwa HAKI kwa hii IMANI yake.
·         Mwanzo 4:8-18. Kaini muasi akamuua mwenye Haki Habili, akalaaniwa TENA kama wazazi wake na AKAFUKUZWA kwenye uwepo wa Bwana akaenda kuendeleza kizazi KIASI, na wakati huo hakukua NA kizazi cha haki kwani Habili alishakufa.
3.       SethiMwanzo 4:25-26
·         Vizazi viwili toka kwa Adam- cha haki kilishauawa lakini cha UASI kilizidi kuchanua, Dunia nzima ilijawa na kizazi hiki cha Kaini cha Uasi, hakukua na aliyekuwa AKIMCHA Mungu mpaka MTOTO WA KIUME alipozaliwa – SETHI.
·         Baada ya Adam kumpata Sethi akasema “ Mungu ameniwekea uzao…..’ Maneno haya yanaonyesha huyu mtoto wa kiume ni utimilizo mdogo wa ahadi aliyoitoa Mungu wakati anamlaani Hawa-Mwanzo 3:15.
·         Huyu mtoto wa kiume Sethi akaanza kutengeneza kizazi cha haki kwani walikuwa wakiliitia jina la Bwana. Adam alidhani kizazi hiki cha haki kingedumu milele, baada ya vizazi kumi vya haki, haki ikaanza kupotea kwani wengi walivutwa na kizazi cha uasi cha Kaini.
·         Unabii wa kuzaliwa mtoto wa kiume, mkombozi-Hakua Sulemani - 1Nyakati 22:9-10, bali ni Imanueli - Isaya 7:14,9:6

.   2.   AGANO JIPYA (Wakati wa Yesu)
1.       Unabii wa kuja Mtoto Yesu
·         Mungu aliwa ahidi Adam na Hawa kuhusu UZAO wa Mwanamke – kwamba Bikra angepata mtoto wa kiume ambaye ndie angelikuwa mkombozi. Hawa alipomzaa Sethi alidhani kuwa Sethi alikuwa ndio Utimilizo kamili wa ahadi ya Mungu.
·         Nabii Isaya anaona uhitaji wa mtoto wa kiume mwingine ambaye sio Sethi – Isaya 7:14-16. Sethi hakufaa kwa sababu alikuwa na asili ya uasi ndani yake ingawa kwa nje alifanya vizuri ukilinganisha na kaka yake Habili. Isaya 9:6-7.
·         Luka 2:10-14. Huu ndio utimilizo wa Ahadi aliyomuahidi Hawa, ingawa wao walidhani ni Sethi. Mtoto huyu wa Kiume Yesu ndiye MWOKOZI, mbingu zilifurahi, malaika walishuka , mji ulitaharuki lakini wakati wa Sethi hakukua na chochote.
2.       YESU
·         Kuna laana iliyotakiwa kuwapata Waisraeli kwa kumwaga Damu za Haki, lakini ili mtu AEPE hiyo laana alitakiwa kumuamini Yesu asitiriwe- Mathayo 23:34-36.
·         Yohana 3:16- Mungu alimtoa mwanawe ili aanze upya uzao wa Haki, waliokuwa wakimwamini yesu walipewa uwezo wa kuwa uzao mteule, watoto wa Mungu kwa njia ya Imani juu ya Yesu – Yohana 1:12-13,
·         1Yohana 2:22-23,3:1-2

        3. NYAKATI ZETU (Baada ya Yesu)
1.       Damu ya Yesu Yanena Mema- Ebrania 12:24-Tuliona Damu ya Habili ilikuwa ikinena mbele za Mungu, lakini haikuwa inanena mema bali mabaya, ingawa Habili alikuwa mwenye haki lakini alipouawa bila hatia alidai kisasi lakini Yesu hakufanya hivyo, alisema “Baba uwasamehe…’ Luka 23:34. Baadae tutaona mambo 7 ambayo Damu ya Yesu inayanena.
2.       Vizazi viwili – uzao mteule na Wana wa Uasi- 1Yohana 3:10-12, Yuda 1:11- wana wa ibilisi, lakini 1Petro 2:8-10 ni wana wa mungu. Wale watoto wawili wa Adamu ni Unabii mpaka nyakati hizi, kwamba kuna watu wa aina mbili tu haijalishi tunajidanganyaje – aidha ni wa Kaini au Habili ama wa Shetani au wa yesu, hakuna katikati.
3.       Imani juu ya YesuGalatia 3:26- Leo hii mimi na wewe twaweza kuwa Wana kwa kumuamini Yesu tu. Mungu atakuhesabia Haki kama Habili alivyohesabiwa haki kwa njia ya Imani tu- Waebrania 11:4

   4.     HITIMISHO
CHUKUA HATUA- Leo hii unaweza kuwa mwenye Haki kama Habili kwa njia ya Upatanisho ambayo Mungu aliianzisha kwa njia ya Damu ya Yesu, Mungu anakupenda hivyo ameamua akusitiri kwasababu anakupenda – 1Petro 4:8. Lakini pia Leo hii unaweza UKACHAGUA kuwa MUASI kama Kaini kwa kujibunia njia zako za kumpendeza Mungu bila Damu-Waebrania 9:22

BY
APOSTLE  ELIYA
THE EPANGELIA CHURCH
MAKULU-DODOMA

0753 011 774

No comments:

Post a Comment