Monday, December 9, 2013

MAONO YA HUDUMA YA EFATHA


Photo: APOSTLE N PROPHET MWINGIRA
mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat  Mwingira. 

Huduma ya Efatha ni maono aliyopewa Mtumishi wa Mungu, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira ambayo ndani yake kuna kusudi la Kiungu. Neno Efatha linapatikana katika kitabu cha Marko 7:34, maana yake FUNGUKA.

Ili kufanikisha kusudi hilo, MUNGU alimpa Mtume na Nabii vipengele 10 vya kutekeleza ambavyo kwa pamoja ndivyo vinavyoumba Huduma ya Efatha.

1. Kuikomboa Tanzania ili iweze kusimama mbele za kiti cha hukumu na kupokea baraka za MUNGU.
2. Kuliandaa kanisa la YESU KRISTO kwa ajili ya kunyakuliwa lisilo na mawaa wala makunyazi.
3. Kufanya Kanisa la YESU KRISTO liwe na Mamlaka.
4. Kudhihirisha uweza katika KRISTO YESU, kwa Ishara, Miujiza, Uponyaji na Ukombozi wa Roho, Nafsi na Mwili.
5. Kuwafanya watakatifu wawe na umoja.
6. Kumzalia BWANA matunda yaani kuwaleta watu kwa YESU.
7. Kupokea vipawa vya MUNGU kama mahitaji yetu, ROHO MTAKATIFU, lugha mpya na kuvigawa.
8. Kusimamia kazi ya MUNGU na kuruhusu maongozi ya ROHO MTAKATIFU yaweze kutenda kazi.
9. Kuhakikisha kuwa malango ya kuzimu yananyamazishwa.
10. Kuwa tayari wakati unaofaa na usiofaa kuhubiri NENO la MUNGU.

No comments:

Post a Comment