Saturday, December 28, 2013

Ufufuo wa Theo Nez

Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu 

Nafasi ya Pili 
www.DivineRevelations.info/Swahili 
Theo Nez alikulia katika taifa wa Wanavajo karibu na pembe 4 za USA. 
Bado anaishi katika eneo hilo. Mwaka 1995 alinunua kitabu cha Mary 
Baxter “Ufunuo wa kuhusu Kuzimu” akifikiri ataishi tena miaka 30 ijayo 
hivyo angeweza kuwa na muda mzuri kurekebisha na Mungu. Akakiweka 
kandolakini, miezi sita baadae alipokuwa akifanya Meth nyumbani kwake 
alikufa kwa sababu ya kutumia nyingi (over dose). Yesu Kristo mwenyewe akamchukua Theo 
kwa mkono wake na akampeleka katika shimo lake la Kuzimu. Kwa masaa mawili alimsihi Yesu 
asimpeleke pale….. Lakini Yesu hakuweza kubadili kitu. Mpaka pale aliposikia mke wake, 
muamini, akimuombea….Yesu akamueleza kuwa atakwenda kujibu maombi yake kwa sababu 
alisimama katika neon na hakurudi nyuma… Yesu akampeleka Mbinguni na kwa masaa mawili 
alimuonyesha mambo yajayo na akamuamuru awaambie wengine kwamba tunaishi katika 
nyakati za mwisho naya kwamba Bwana amekaribia kurudi. Ujumbe wake ni kuwa hatuwezi 
kuwatumikia mabwana wawili. 
Hello Kaka na dada zangu wapendwa. Jina langu ni Theo nez na ninnaishi Farmington New 
Mexico. Leo ningependa kushiriki nanyi ushuhuda wangu, Jinsi Mungu alivyofanya kitu cha 
ajabu sana, Kwangu mimi na kwa familia yangu. Alileta Wokovu wake katika nyumba yetu. 
Mwaka 1995, Nilikuwa ni mtu wa asili. Nilikunywa na kutumia madawa, sikujali kitu 
chochote.Siku moja, Nilitumia zaidi kupindukia kwa haraka na moyo wangu ukasimama. Nikafa 
kwa masaa. Kile nachotaka kuwaeleza, kitawafanya mfikiri mara mbili kwa habari ya maisha na 
kifo. Moyo wangu uliposimama, kelele za ulimwengu zikatoweka kabisa na giza kuu likaja 
kwangu. Nikaona mapepo matatu yakitoka kwenye moyo wangu, yakienda nje ya dirisha huku 
yakicheka. Nilipotoka kwenye Mwili wangu, Niligeuka nyuma nikamuona Yesu alikuwa 
amesimama nyuma yangu. Nywele zake zilikuwa ni dhahabu yenye weupe; Alikuwa amevalia 
vazi jeupe lenye mshipi wa dhahabu. Viatu vyake vilikuwa ni sandosi za dhahabu, na alisogea na 
akaongea kwa sauti ya upole.Viatu sandosi za dhahabu. Viatu vyake vilikuwa ni sandosi za 
dhahabu, na alisogea na akaongea kwa sauti tulivu. Kulikuwa na mwanga uliomzunguka na 
Roho yangu ikawa imekwisha mtambua. Nilitembea mpaka kwake na kumuuliza; Yesu ulikuwa 
wapi, nilikuwa nikikutafuta. na akaongea kwa upole na kusema; sikuwahi kukuacha, nimekuwa 
pembeni yako siku zote. Nilikuwa nikisubiri wewe utubu na kufanya kusudi la Baba. 
Unafahamu, nilikuwa nimeitwa kuhubiri miaka michache iliyopita. Nikasema, Nitakwenda,lakini 
nilikimbia. Nikasema siwezi kufanya, Bado ni kijana sana. Mungu anapokuita na kuingilia 
maisha yako huna uchaguzi mwingine lakini inakupasa useme ndiyo Bwana. Kisha 
nikamwambia Yesu, nilifikiri ningeishi miaka mingine thelathini. Njoo, imekupasa kuona mengi. 
Alinishika mkono wangu na tukaanza kutembea kuelekea chini kwenye njia. Ilikuwa ni giza na Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu 

Yesu mwenyewe ndiye alikuwa mwanga. Mara nikaanza kuona pepo wametuzunguka. 
Walikuwa wakijaribu kunirarua, lakini nikamshikilia Yesu mkononi kama mtoto mdogo. 
Alikuwa ni kinga yangu na akaanza kuongea nami. Akasema, unajua Baba anahasira nawe. Ni 
kwa sababu nilikuwa na cheza na kanisa na kukimbia kama Yona. Biblia inasema Yona aliitwa 
kuhubiri lakini alimkimbia Mungu. Nimefanya hivi kwa muda wa miaka mingi. Sasa imenishika 
mimi pia. Nilifahamu kuwa nilikuwa nimekufa katika dhambi zangu, na nilikuwa nimekwisha 
chelewa. Tulipoendelea mbele, Yesu akaongea mambo mengi na nikamuuliza maswali mengi. 
Tukasima mahali fulani na yesu akaniambia, angalia mbele. Niliweza kuona aina fulani ya 
mwanga kwa mbali. Yesu akaniuliza; Unafikiri hiyo ni nini? Nikasema, Bwana hiyo inaonekana 
kama kuzimu, Labda ni miali ya moto wa kuzimu. Hakika, tuliposogelea karibu, tukafika juu ya 
bonde. Bonde lilikuwa kama maili mbili kwa kina na maili tatu kwa upana 
Chini niliweza kuona miali ya moto, kila kitu kilikuwa ni orenji nyekundu, Nikaanza 
kutetemeka, Nikaanza kuogopa. Nilifahamu kuwa nitawenda kuishia mahali pale.Yesu 
akaniambia niangalie chini. Sikuweza hata kuangalia chini, nilianza kulia huku nikimkimbilia 
Yesu nyuma. Nikaanza kutubu, na kuliakwa Bwana ili anisamehe. Nitahubiri sasa, nipe nafasi 
moja ya mwisho. Nililia kama mtoto mdogo. 
Tuliendelea mpaka tukafika chini kabisa kwenye shimo la kuzimu. Nilona vitu vingi ambavyo 
maneno hayawezi kusimulia. Sehemu ile ilijaa roho za watu, na mapepo yalikuwa kila eneo. 
Biblia inasema Isaya 5:14 Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake 
bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, 
hushuka na kuingia humo. 
Kulikuwa na Roho za watu zikiwaka katika miali ya moto. Vilio na 
kelele zilikuwa kila sehemu. Hakukuwa na tumaini, hakukuwa na 
tumaini kwa roho zilizopotea. Kwa nini ? Kwa sababu walimkataa 
Yesu. Wengine walisubiri muda mrefu. Wengi walifanya mdhaa na 
wakamkimbia Mungu. Kumkimbia Mungu kutakufanya uingie 
Kuzimu. Ukishaingia mule huwezi kutoka. Tafadhali, ningependa 
uinue mikono yako na kumwambia Bwana; Usiruhusu hili kutokea 
kwangu. Tulipoendelea kutembea, Niliona mamia ya elfu ya mashimo. 
Nilikuwa nikilia na kuomboleza tulipokuja kwenye shimo moja 
ambalo ni tupu. lilikuwa na moto uliokuwa ukitoka ndani yake. Yesu 
akaniambia; Hili ndilo shimo ambalo shetani amekuchimbia. Kisha nikaanza kupiga mayowe, 
nikilia, Bwana sitaki kwenda pale. Nililia na kutubu, NikimuombaYesu anipe nafasi moja 
nyingine tena. Nililia kama Yona alipokuwa kwenye tumbo la Kuzimu. 
Katika Kitabu cha Luka 16, tunasoma kwa habari ya Lazaro na Tajiri mmoja. Tajiri alikuwa na 
kila kitu. 20 Kulikuwa pia na maskini mmoja jina lake Lazaro, aliyekuwa amejaa vidonda na 
alikuwa analazwa mlangoni pa nyumba ya huyo tajiri. 21 Lazaro alitamani kula makombo 
yaliyoanguka kutoka meza ya tajiri; na zaidi ya hayo, mbwa walikuwa wanakuja na kulamba 
vidonda vyake! 22 Ikatokea kwamba huyo maskini akafa, malaika wakamchukua, wakamweka Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu 

karibu na Abrahamu. Na yule tajiri pia akafa, akazikwa. 23 Huyo tajiri, alikuwa na mateso 
makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu 
naye. 24 Basi, akaita kwa sauti: Baba Abrahamu, nionee huruma; umtume Lazaro angalau 
achovye ncha ya kidole chake katika maji, auburudishe ulimi wangu, maana ninateseka mno 
katika moto huu. 25 Lakini Abrahamu akamjibu: Kumbuka mwanangu, kwamba ulipokea mema 
yako katika maisha, naye Lazaro akapokea mabaya. Sasa lakini, yeye anatulizwa, nawe 
unateswa. 26 Licha ya hayo, kati yetu na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wanaotaka kuja 
kwenu kutoka huku wasiweze, wala wanaotaka kutoka kwenu kuja kwetu wasiweze. 27 Huyo 
aliyekuwa tajiri akasema: Basi baba, nakuomba umtume aende nyumbani kwa baba yangu, 
28 maana ninao ndugu watano, ili awaonye wasije wakaja huku kwenye mateso. 29 Lakini 
Abrahamu akamwambia: Ndugu zako wanao Mose na manabii; waache wawasikilize hao. 
30 Lakini yeye akasema: Sivyo baba Abrahamu, ila kama mtu atafufuka kutoka wafu na 
kuwaendea, watatubu. 31 Naye Abrahamu akasema: Kama hawawasikilizi Mose na manabii, 
hawatajali hata kama mtu angefufuka kutoka wafu." 
Oh Watu , tafadhali mnisikilize,hii ni halisi,weka mambo yako sawa na Mungu vile uwezavyo 
.Tulipotoka nje, tulisimama katika eneo lenye ukiwa. Yesu akasema;sikia. Na nikaanza kusikia 
mwanamke akisali niliweza kusikia sauti yake vizuri wakati akiomba alisema; Bwana mrudishe 
tena! Mpe tena nafasi nyingine. Bwana ana watoto wawili wa kiume wa kuwalea. Yeye ndiye 
pekee niliyenaye. Usimchukue Bwana! 
Unaamini maombi ya imani yanaweza kuamisha chochote? Biblia inasema, chochote 
mnachohitaji mkiomba , amini umekwisha pokea,na hakika mtapokea. Mwanamke huyu 
akaendelea kuomba. Yesu akaniuliza, Unafikiri huyo ni nani? Nikamwambia huyo ni mke 
wangu. Bwana akasema, unasikia hicho,nina watoto wawili wa kuwalea. Nikaanza kumshika 
Bwana kwenye mabega, siwezi kufa sasa, familia yangubado inanihitaji. Nikaanza kutoa sababu 
mbalimbali, lakini hakukuwa na jibu. Nikaanza kulia tena. 

Mke wangu aliendelea kuomba. Kulikuwa na kipindi cha kusubiri ambacho kilikuwa kama 
masaa na mwisho Mungu Baba akajibu hili, Akaongea na sauti yake ilikuwa kama Maji mengi. 
Akasema Mwanangu; nakwenda kukupa tena nafasi nyingine kwa sababu ya maombi na imani 
ya mke wako,nitakuhifadhi. Nikikurudisha, nitakwenda kukutumia. 
Hapo nikaanza kusema kwa viapo,Bwana nitahubiri. Nitafanya chochote, Nitawaeleza watu 
kuhusu sehemu hii, Nikasema Bwana ,Nitakusaidia kuokoa roho . 
Kisha tukatembea kuelekea kwenye chumba chenye kioo kikubwa kama Televisheni. 
Nilionyeshwa wakati wangu uliopita,wa sasa na utakaokuja. Nikaweza kuona ,maisha yangu 
kuanzia mtoto mpaka nilipokuwa mkubwa. Yesu alinipa ufunuo, maono. Alinionyesha mambo 
mengi sana ambayo ni lazima yatokee. Akasema, kweli tunaishi katika nyakati za mwisho. 
Nenda na uwaeleze watu. waambie watembee katika njia sahihi na watubu. Waeleze waache 
kucheza na mimi na waanze kushika amri zangu. 
 Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu 

Akanionyesha jinsi watu wanavyojificha nyuma ya Biblia, wanayaficha matendo yao,na 
wanaishi katika dhambi. Mungu anasikia na kuona kila kitu. Akasema watu hawa 
wanamuheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nae. Oh jinsi wanavyopenda 
kufundisha amri kwa watu, lakini wanaziacha amri za Mungu. 

Akasema , usogope,Mimi ni alpha na omega, wa kwanza na wa mwisho, Unachokisikia ni haki. 
Akasema; yeye aliye na sikio, na sikie kile Roho anasema kwa kanisa. Akanipa mistari mitatu,Ta
hadhari. Wa kwanza ni Kumbukumbu la torati 6:15. (15 kwani Bwana, Mungu wako, aliye 
katikati yako ni Mungu mwenye wivu;) isije ikawaka juu yako hasira ya Bwana, Mungu wako, 
akakuangamiza kutoka juu ya uso wa nchi. 

Mstari wa pili katika Luka 16:13. Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili; 
kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au ataambatana na mmoja na 
kumdharau mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali. 

Msitari wa tatu katika kitabu cha Ufunuo 3:3 Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi 
ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua 
saa nitakayokuja kwako. 
Kaka na dada, Hatujui ni siku gani tutaonndoka katika ulimwengu huu, hatujui kesho imebeba 
nini ,kwa hivyo ninaomba kwamba uweke mambo yako sawa na Mungu wakati bado unaweza. 

Baada ya hili Yesu akanichukua mpaka mbinguni 
na tukatembea katika malango haya ya dhahabu 
katika mtaa wa dhahabu. Nikaona watu wengi wa 
kila taifa na walikuwa wamesimama mbele ya kiti 
kile cha enzi, wamevalia mavazi meupe, Baadhi 
yao ni watu niliowafahamu, wachungaji na 
manabii wa kwenye biblia. kila kitu kilikuwa ni 
kizuri,kila mtu alikuwa ni mwenye 
furaha;ungeweza kuona upendo wao kwenye sura 
zao. Nilianza kuhisi furaha na amani.Nilipokuwa 
nikitembeatembea, sikutaka tena kurudi. Yesu 
akanifunulia saa kubwa. Mkono wa saa ulikuwa 
umekaribia kufikia kamili kwenye 12,wakati 
unakimbia haraka,wakati wa kwenda sasa. 
Nikasema Bwana, sitapenda kwenda, nataka 
nibaki. Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu 

Lakini ilinipasa kurudi. Tulipokuwa tukirudi niliona dunia kama kampira kadogo kama ule wa 
golf. Alinileta tena kwenye chumba changumwili wangu ulipokuwa umelala. Alisogelea mahali 
ambapo moyo wangu ulikuwepo. Nyama iliyozungukza moyo wanguilifunguka. Yesu 
akachukua moyo wangu wa kale nje, na akautupa katika ziwa la moto, Kisha akanipa moyo 
mpya, na mwanga ukaja juu yake. Nilisimama pale nikiagalia na kutafakari,wow; hata ngozi na 
mifupa inasikia Yesu. 


Baadae nilitafuta katika biblia yangu na nikakuta Ezekieil sura 36 :26-27, Nililia kama mtoto 
mdogo kwa sababu ilikuwa imeandikwa, Pale Biblia inasema hivi: 26 Nami nitawapa ninyi 
moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya 
mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama. 27 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na 
kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda. 

Baada ya Yesu kurejesha roho yangu kwenye mwili wangu, lakini moyo wangu mpya haukuwa 
unafanya kazi bado.Nilimuona mke wangu ameshika mikono yangu anaomba. Muda nikaona 
chumba changu kimezungukwa na maelfu ya malaika, walikuwa wakisifu na kuimba kwa 
nyimbo nzuri ambazo sikuwahi kuzisikia. Muziki tu wenyewe ulikuwa ni waajabu sana,Malaika 
mmoja akatokeza kwa nje na akatamka, akisema; Damu ya Yesu inakuja. Na malaika wote 
wakaanza kusifu na kuabudu. Kisha Damu ya Yesu ikaja tulipo,na kunisafisha mimi kuanzia 
kichwani mpaka kwenye vidole vyangu vya miguu ikasafisha dhambi zangu zote. Pombe na 
madawa vikatoka nje ya mwili. Nikahisi kama maji ya moto. Nilipojiangalia, ule weusi wote wa 
mwili wangu ukaondoka. Nilikuwa mweupe na msafi. 
Baadae malaika Yule Yule akatoka nje tena na akasema; Roho Mtakatifu anakuja.Malaika 
wakaanza kuimba na kuabudu tena. Holy spirit akaja kwetu tulipo na kutujaza. Roho yangu 
ikaanza kuruka tena juu na chini. Kisha nikampata Roho Mtakatifu. Roho ya Bwana ilikuwa na 
moto kama umeme; ilikuwa kama moto unaowaka kwenye mifupa yangu. 

Malaika walikuwa bado wakiimba na kusifu Yesu aliposema; Mwanangu, nenda kawaambie 
watu nilicho kushuhudia wewe. Akaugusa moyo wangu mpya kwa vidole vyake na ukaanza 
kufanya kazi. Ndipo kidogo kidogo macho yangu yakaanza kufunguka. Nikagundua mwili 
wangu umekuwa wa baridi, ilikuwa ni vigumu kidogo kuongea. Nikamuuliza mke wangu 
kilichotokea. Akaniangalia na kuniambia; Uko sawa? Kisha akaanza kulia. 

Kulikuwa bado kuna maumivu kwenye kifua changu chote, nikaona kama ninaopresheni. 
Nilikuwa mdhaifu na kiu; Kitu cha kwanza kuuliza ilikuwa ni maji. Kisha fahamu zangu Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu 

zikaanza kunirudia na nikakumbuka kilichonitokea. Kisha nikaanguka kwa Magoti na kuomba 
kwa muda wa masaa matatu mpaka jua likachomoka. 
Kutoka siku hiyo maisha yangu yamekuwa tofauti. Nilikuwa muasi, Lakini Mungu akanishusha 
kwa magoti , nikaanza kulia kama mtoto mdogo, nikiomba rehema. Nilikuwa nikifikiri, nikienda 
kuzimu, haitajalisha. Lakini sikuwa najua ni kiasi gani kuzimu ni chungu mpaka pale Bwana 
aliponifunulia. Sasa namshukuru Bwana kila siku kwa maisha ambayo amenirejeshea, familia, na 
huduma aliyonipa. 
Kaka na dada ,Ninaomba kwamba msichezee kanisa na kuwa na mabwana wawili, Kwa sababu 
huwezi ukacheza na Mungu. Ni kitu cha kutisha kama nini kuangukia katika mikono ya Mungu 
aliyehai. Hivyo usidanganyike,Mungu hadhiakiwi. Biblia inasema;Apandacho mtu, ndicho 
atakachovuna, Yeye apandaye uovu, atavuna huo. Ndiyo Mungu ni Mungu wa upendo; amejaa 
huruma na rehema. ni Mungu wa nafasi ya pili, lakini ni Mungu wa hukumu .Biblia inasema 
Yeye ni moto ulao.hivyo imetupasa tujiandae, kwa sababu hujui ni lini utakwenda kufa, Bilblia 
inasema katika waebrania 9:27, kama inavyoamriwa kwa wanadamu kufa mara moja, lakini 
baada ya hili ni Hukumu. 

Siku inakuja ambayo sote tutasimama mbele zake Mungu, na vitabu vyetu vitafunguliwa. Utakw
enda kuwa pale. Kila Mtu ambaye anasikiliza ushuhuda huu atakwenda kuwa pale. Hiyo itakuwa 
ni mwito ambao huwezi kukosa. Hii inaweza kuwa ni mwito wako wa mwisho, usiasi mbele zak
e Mungu. Tafakari kwa makini kuhusu hili, Itaenda kuwa peponi au kuzimu. Unaweza usipate na
fasi nyingine kama mimi; Ni kwa neema ya Mungu tu. 
Niko hapa leo ilikushiriki nanyi ushuhuda huu, ningependa unyanyue mikono yako na uongee na
Bwana, Mshukuru Yeye kwa kuwatahadharisha, Mshukuru Yeye kwa maisha haya ya thamani. 
Kama ungependa kuokoka, unahitaji sala hii, Ngoja niombe sala hii pamoja nawe hivi sasa. 

Bwana Yesu ,nisamehe. Ninakupokea wewe kama Bwana Mwokozi wangu. Njoo moyoni mwan
gu na maishani mwangu. Nipe Uzima wa milele, ili niweze kuishi nawe milele. Nipe maisha ya a
mani na furaha. Aksante Bwana. Katika Jina la Yesu, Amen. 




 Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu 

Kama ukipenda kuniandikia anuani yangu ni: 

Last living days Ministries 
P.O. Box 3701 
Farmington, NM 87499 
USA 
Unachokisikia kwenye ushuhuda huu ni simulizi ya kweli. Mimi ni
 Mtu wa India Mnavajo.Ninaishi Four Corners. Nina rasimisha kan
da hii kwa Wamarekani wenyeji wote Marekani nzima. 
Ninatoa Ruhusa kunakili ushuhuda huu. 




Ndugu aliyefasiri ufunuo huu ni Peter Kahale ni kijana aliyeokoka na anampenda Yesu na 
mwenye shauku ya kuhubiri injili ya Yesu Kristo. 
Simu ya Mkononi: +255-769-610460, +255-653-610460. 
Barua Pepe: kahalepeter@gmail.com 

No comments:

Post a Comment