Wednesday, March 12, 2014

AGANO NA MUNGU(3)













Na Joseph Goliama
HATUA YA SITA YA USHUHUDA HUU NI HII HAPA
Kila mwanadamu anapaswa kujua kuwa Mungu ni msingi wa kila kitu kinachoonekana na kisichoonekana, Ninaposema Mungu ni Msingi wa kiila kitu namaanisha kuwa Mungu ni chanzo cha kila kitu yeye ni asili ya kila kitu na yeye ni mwanzo wa kila kitu yaani Mungu ni kiini cha kila kitu hapa nataka ujue wazi kuwa ninaposema Mungu ni msingi, kiini, asili, mwanzo na chanzo cha kila kitu namaanisha kwamba Uzima, upendo na haki ndio msingi, asili, kiini,mwanzo na chanzo cha uumbaji wote wa Mungu, ninapata matumaini sana pale ninapojua kwa hakika kuwa Mungu niye chanzo cha maisha yangu ya hapa duniani ufahamu huu umenifanya nifanye kila niwezalo kurudi kwenye msingi wangu, kurudi kwenye kiini changu, kurudi kwenye asili yangu, kurudi kwenye mwanzo wangu, kurudi kwenye chanzo changu kwa hakika kurudi kwenye chanzo,asili,kiini,mwanzo na msingi wangu ni kurudi katika maisha ya Uzima maisha ya upendo maisha ya haki na kwa hakika mtu yule ambaye amerudi katika chanzo chake milele Uzima, upendo na haki havitakuwa adimu katika maisha yake kwakuwa ameunganishwa na majibu ya uhitaji wake
Nataka wanadamu wenzangu ambao wanatafuta Uzima wanaotafuta Upendo na wanaotafuta haki wajue wazi kuwa wanamtafuta Mungu na yakwamba naweza kwa neema ya Mungu kuwasaidia kukutana naye kwasababu amenituma kumtambulisha kwa wanadamu ili yeye mwenyewe Mungu akutane nao nakujhitimisha uhitaji wao katika maisha yao


HATUA YA SABA YA USHUHUDA HUU NI HII HAPA
Baada ya kueleza jinsi Mungu alivyojifunua kwangu sasa nataka wanadamu wenzangu muelewe kuwa Mungu alisema nami kuhusu miili yenu aliniambia watu wangu wanakufa kabla ya wakati wao kwa sababu Uzima , nguvu za Uzima na mamlaka ya Uzima imeadimika katika maisha yao, kiukweli maneno ya Mungu yalinichoma sana hasa ukizingatia kuwa Mungu tayari alishaniambia kuwa yeye ni Uzima yeye ni nguvu za Uzima(UPENDO) na yeye ni mamlaka ya Uzima(HAKI), hivyo aliponiambia kuwa wanadamu wanakufa kabla ya wakati wao moja kwa moja niliangalia nakujua wazi kuwa ni kweli hapa duniani wanadamu wengi wanahangaika sana kwa sababu miili yao inahitaji Uzima, nguvu na mamlaka yakufanya kazi ipasavyo, miili au viungo vya wanadamu mara nyingi vinapata magonjwa na magonjwa hayo yamekuwa sababisho la roho za wanadamu kutoka ndani ya miili hiyo
Ukiienda mahospitalini utajua nini naongea hapa hospitali utawakuta wagonjwa wengi sanA na wote wanahitaji Uzima, wanahitaji uzima wa kiungo chao kimoja baadhi kwa mujibu wa maelezo hapo nyuma nataka uelewe wazi kuwa mwanadamu anapohitaji uzima humuitaji Mungu kwakuwa Mungu ni Uzima hapa nataka kukuuliza wewe mwenye pumu wewe mwenye vidonda vya tumbo, wewe mwenye kisukari, wewe mwenye ngiri, wewe mwenye kansa, wewe ,mwenye ugonjwa wa moyo ,wewe mwenye ugonjwa wa mifupa wewe mwenye leukemia, wewe mwenye uonjwa wa kichwa, wewe mwenye ugonjwa wa kifua, wewemwenye ugonjwa wa kiungo chochote cha mwili wako jeeeee unajua kuwa unahitaji Uzima? najeee unajua Uzima ni Mungu?

HATUA YA NANE YA USHUHUDA HUU HII HAPA ISOME
Baada ya kukujulisha kuwa Mungu ni Uzima ni Upendo nani Haki, na baada ya kukujulisha kuwa Mungu hana umbo ndio maana hata Uzima hauna umbo hata upendo hauna umbo hata haki haina umbo na baada ya kukujulisha kuwa duniani kote wanadamu wanahitaji Uzima, Upendo na haki nayakwamba wanadamu tunamtafuta Mungu bila kujua kuwa tunamtafuta pale tunapotafuta Uzima, upendo na haki , na baada ya kukusaidia kujua wazi kuwa hata Yesu mwenyewe aliishi na Mungu kwakuwa aliishi na Uzima na Upendo na haki, na kwakuwa Yesu aliishi na Mungu ndio maana maisha yake yote aliishi maisha ya kumfunua Mungu baba yake kwakufunua Uzima, upendo na haki kwa wale wote waliokuwa wanatafuta Uzima, upendo na haki na kwakuwa Yesu aliishi na kutembea na Mungu baba yake ndio maana alifunua asili ya Mungu ya wokovu, utakatifu na ushindi. kwa ukweli huo huo nataka ujue kwa hakika kuwa Mungu wetu yeye ni Uzima yeye ni Upendo yeye ni haki, Mungu huyu ninayemzungumzia anataka kujifunua kwako yeye mwenyewe anataka kujifunua kwako ili wewe ujue wazi kuwa yeye ndiye Uzima wako yeye ndiye Upendo wako yeye ndiye haki yako, kwa hakika ili Mungu ajifunue kwako unapaswa wewe kwanza kumjua yeye, kumjua Mungu ni kujua mawazo yake ni kujua mtazamo wake ni kujua maneno ya kinywa chake ni kujua matendo yake ni kujua mwonekano wake ni kujua mahusiano yake ni kujua maamuzi yake ni kujua misimamo yake, kuyajua haya ni kujua maisha ya Mungu, maisha ya Mungu ni maisha ya Uzima ni maisha ya upendo nani maisha ya haki, maisha ya Mungu ndio yanayomfanya tumuite Mwokozi, mtakatifu na Mshindi, maisha ya Mungu ndio yanayotufanya wanadamu tumjuao, tuweze kuishi maisha ya kumtegemea, kumpenda na kumuamini, maisha ya Mungu yenye sehemu hizo nane nilizozitaja yanamfanya Mungu kuwa adui mkubwa wa shetani, Mungu ni adui wa shetani maana yake adui wa mauti adui wa uovu ni adui wa yasiyo ya haki. Mwanadamu anayetaka kukutana na Mungu yaani kukutana na Uzima kukutana na Upendo na kukutana na haki lazima akubali kuyatoa maisha yake ili ndani yake Mungu(Uzima, upendo,haki)aishi na pia akubali Mungu kuutumia mwili wake kujifunua kwake na kwa wanadamu wengine
Jiulize maswali haya
1. Uko tayari Mungu aishi nawewe? yaana uko tayari Uzima, upendo na haki viwe maisha yako ya kila siku kila wakati?
2. Uko tayari Mungu atumie mwili wako kujifunua kwako na pia autumie mwili wako kujifunua kwa wengine? kwanini Mungu anataka aafikiane (akubaliane nawewe,aweke agano nawewe, apatane nawewe) nawewe kuishi nawewe mwanadamu na kutembea nawewe mwanadamu hapa duniani? jibu ni rahisi yeye Mungu hana Umbo yeye hana mwili kama sisi wanadamu , hivyo ili aishi na kutembea hapa duniani ni lazima akubaliane apatane,aweke agano afikie mapatano nawewe mwanadamu anayetaka kuishi nawewe na kutembea nawewe, ndio maana tunasema Mungu wetu ni Mungu wa maagano
Jee! uko tayari kukubaliana na Mungu aishi ndani yako kama alivyoishi ndani ya Yesu Kristo? na jee! uko tayari kutembea na Mungu hapa duniani kama alivyotembea na Yesu Kristo? kama Utakubali kuishi na kutembea na Mungu nakuhakikishia Uzima, upendo na haki havitakuwa adimu siku zote za maisha yako
Kumbuka katika MUNGU NI MMOJA PART HII YA 8 , tumejifunza maisha ya Mungu wetu yale maeneo nane na yakwamba Mungu anataka kuishi na kila mwanadamu na kutembea na kila mwanadamu ili Uzima, upendo nahaki visiwe adimu hapa duniani.

HATUA YA TISA YA USHUHUDA HUU HII HAPA ISOME
Baada ya kujifunza katika hatua za awali za kumjua Mungu wetu kisha kuyajua maisha anayoishi Mungu wetu sasa tujifunze ni kwa namna gani mwanadamu bila kujali dini yake, kabila lake, rangi yake, Taifa lake, jinsia yake ,rika lake, asili yake, ukoo wake au bila kujali chochote awezavyo kuweka makubaliano na Mungu, mapatano na Mungu,maafikiano na Mungu,agano na Mungu la kuishi na Mungu na Kutembea na Mungu hapa duniani na milele mbinguni
Tukumbuke kuwa Mungu hana umbo wala mwili, yeye ni Mungu wa wote wenye mwili, yeye ni Uzima yeye ni Upendo yeye ni haki, Mungu hana mwili ndio maana akikaribishwa na mwenye mwili kwake ni rahisi kuingia ndani ya mwenye mwili na kufanya makao ndani yake, hufanya makao kwa kuishi ndani ya mwenye mwili na kwa kawaida akiishi ndani ya mwanadamu humsaidia mwanadamu huyo kila anapohitaji Uzima, upendo na haki kwakuwa yeye mwenyewe ndiye jibu la uhitaji wa mwanadamu, huwezi ukaishi na Mungu uzima ukawa adimu au upendo ukawa adimu au haki ikawa adimu kwako, ukiishi na Mungu unaishi na utoshelevu wako, yeye anakuwa maji kwa kiu yako anakuwa chakula kwa njaa yako, utajiona huitaji kitu kwakuwa yeye ni kila kitu kwako. kuishi na Mungu ni sawa na mwanamke anayeishi na mwanaume wake mwenye kila kitu anachokihitaji hakika mwanamke huyo huishi na utoshelevu wake wote na hujiona kila anachokihitaji ni mume wake tuu na hatahitaji mwingine zaidi ya mume wake, hali hiyo ndio inayompata mwanadamu anayeishi na Mungu na kutembea na Mungu hapa duniani hatahitaji chochote zaidi ya Mungu, maisha yangu yamebadilika sana baada ya kukutana na Mungu wangu hivi sassa moyo wangu unahitaji kuishi na Mungu na kutembea na Mungu tuu kwani najua kama ntaishi naye na kutembea naye basi atanisaidia mimi na wanadamu wenzangu kupitia mimi
Kuingia agano na Mungu ndio njia pekee yakuingia katika maisha ya Uzima ya upendo na ya haki yaani maisha ya Mungu ndani yetu, agano na Mungu unapaswa kuliweka kwa kukubali yafuatayo
1. Kumkubali Mungu maishani mwako kwa kukubali Uzima, upendo na haki kuwa maisha yako ya hapa duniani na milele mbinguni
2. Kukubali maisha ya Mungu kuwa maisha yako ya hapa duniani na milele mbinguni
3. Kukubali kuyajenga maisha yako ya hapa duniani kwa kumtumikia Mungu yaani kutumikia Uzima,upendo na haki kwa kuyafuata maisha ya Mungu yaani kwakufuata mawazo yake,mtazamo wake,maneno ya kinywa chake,matendo yake,mwonekani wake,mahusiano yake,maamuzi yake na misimamo yake
Kama utaamua kukubaliana na Mungu maisha hayo kuyaishi ndipo utakuwa umefanyika kiumbe kipya na kimsingi ndio kuzaliwa mara ya pili, ndio kuanza maisha mapya na Mungu ndio kuingia katika ufalme wa Mungu ndipo kuanzia hapo Mungu atakuwa mfalme wako atakuwa Mungu wako yaani atakuwa uzima wako atakuwa Upendo wako atakuwa haki yako. nasisitiza kabisa kuingia katika agano na Mungu kunakupa sauti ya Mungu na mwelekeo wa Mungu maishani mwako, kama hauisiki sauti ya Mungu wala hauoni mwelekeo wa MUNGU MAISHANI MWAKO USIJIULIZE,sababu ni hii hauna makubaliana yoyote na Mungu, hauna mapatano yoyote na Mungu hauna maafikiano yoyote na Mungu, kama utaweka mapatano na Mungu,kama utaafikiana na Mungu maisha yako yatapata sauti ya kuisikiliza na yatapata mwelekeo wa kuufuata nawe utakuwa na amani na Mungu. unajua kwanini wanadamu wengi wanaogopa kifo ?wanaogopa kifo kwasababu hawana agano na Mungu,hawana maafikiano yoyote na Mungu na maisha yao wanaishi kama wamekuja duniani kwa bahati mbaya. lakini nakushauri wewe mfanye Mungu kuwa maisha yako ya hapa duniani ili ukienda mbinguni uishi naye na kutembea naye milele
Mungu ni Mungu wa agano sisi ni warithi wa agano jipya tunapaswa kuishi katika agano letu ambalo linatutaka tuishi na Mungu na kutembea na Mungu hapa duniani na milele mbinguni. weka agano na Mungu sasa,kubali kuishi naye na kutembea naye hapa duniani na milele mbinguni. ukiweka agano na Mungu unakuwa umejikabidhi maisha yako kwa Mungu naye atawajibika kukutunza,kukulinda na kukutetea siku zote za maisha yako wewe na yeye hapa duniani mpaka atakapoamua urudi nyumbani ukakae nae milele

HATUA YA KUMI YA USHUHUDA HUU HII HAPA ISOME
Ikiwa utaamua kuweka agano na Mungu ikiwa utapatana naye kuishi naye na kutembea naye hapa duniani na milele mbinguni baada ya kifo chako cha mwili, basi unakuwa tayari umeanza maisha mapya, maisha haya nayafananisha na maisha ya wawili waliooana na sasa wanaanza maisha ya ndoa yao, cha kwanza kinachopaswa kufanyika baada ya kuingia Agano na Mungu ni kujua kwa upande wako unapaswa kuishije katika agano lako na Mungu, hapa jiulize unapaswa utumikiaje mawazo ya Mungu?unapaswa utumikiaje mtazamo wa Mungu?unapaswa utumikiaje maneno ya kinywa cha Mungu?unapaswa utumikiaje matendo ya Mungu?unapaswa utumikiaje mwonekano wa Mungu?unapaswa utumikiaje mahusiano ya Mungu?unapaswa utumikiaje maamuzi ya Mungu?unapsawa utumikiaje misimamo ya Mungu......hapa nataka ujue wazi kuwa unakuwa wakati umewadia wa wewe kufa ili Mungu aishi ndani ya mwili wako kupitia wewe, hapa unapaswa kufa yaani mawazo yako yanapaswa kufa,mtazamo wako unapaswa kufa, maneno ya kinywa chako yanapaswa kufa, matendo yako yanapaswa kufa, mwonekano wako unapaswa kufa,mahusiano yako yanapaswa kufa,maamuzi yako yanapaswa kufa na misimamo yako inapaswa kufa na kama maisha yako hayo yakifa yanafufuka maisha ya Mungu ndani yako, maisah ya Mungu maana yake mawazo ya Mungu,mtazamo wa Mungu,maneno ya kinywa cha Mungu,matendo ya Mungu,mwonekano wa Mungu,maamuzi ya Mungu na misimamo ya Mungu kwa misingi hiyo nataka ifike wazi wewe usiiishi bali Mungu aishi ndani yako ndani ya mwili wako.
Kumruhusu Mungu aishi ndani yako ni hatua ya kwanza kabisa ya ukombozi wa mwili wako mwanadamu, Mungu anapoishi ndani ya mwili wako anaua nafsi yako anaua self yako anaua uwewe(your self)anaua yale maeneo yako nane niliyoyataja hapo juu, anapoua self yako wakati huo huo yeye anachipua ndani yako,yaani maeneo yake yale nane yanaanzan kuchipua ndani ya moyo wako

Kuishi na Mungu ni kufanya nini? kuishi na Mungu ni kwa namna gani? kuishi na Mungu ni kwakumtafakari yeye Mungu,,kama unataka kuishi na Mungu lazima,lazima,lazima,lazima,lazima,lazima,lazima uishi naye katika mawazo yako kwa kumuwaza yeye wakati wote,unapomtafakari Mungu most of your time unamruhusu aumbike ndani ya moyo wako, Mungu huumbika ndani ya moyo wa mwanadamu pale mwanadamu anapochukua muda wake masaa yake kumtafakari, kumtafakari Mungu ni kufanya nini? Nikuchukua muda kutafakari,kuwaza kufikiria sana 1. mawazo yake, 2. mtazamo wake, 3. maneno ya kinywa chake,4. matendo yake,5. mwonekano wake,6. mahusiano yake,7. maamuzi yake na 8. misimamo yake kama utachukua muda kwanza kuyajua maisha hayo ya Mungu kisha ukaamua kuchukua muda wako mwingi kama sio wote wakukaa hapa duniani kuwaza hayo,matokeo yake utaanza kuyasahau maisha yako ya kibinadamu na kujikuta unabadilika na watu watakaokuwa jirani nawe wataanza kuona mabadiliko ya maisha yako sana tena sana.
Kuishi na Mungu ni ukombozi wa mwili wako unakuwa umempata wa kukusaidia dhidi ya mauti ,nguvu zake na mamlaka zake, unakuwa umejitenga na wanadamu wanaokufa bila Mungu kutaka, inaniuma sana kujua wazi kuwa wapo wanadamu maisha ya miili yao yamekatiliwa na ajari, silaha,magonjwa,sumu,wanyama wakali,wanadamu wenzao,hali za hewa,mabadiliko ya maumbile ya dunia nk inaniuma sana kuona hayo yanatokea huku Mungu akitangazwa bila mabadiliko yoyote.
Kuishi na Mungu kunamnyima nafasi shetani kuteka nyara mawazo yako nakuishi ndani yako, shetani ambae ndiye matatizo yetu wanadamu anapigana vita vikubwa na Mungu wakigombea mawazo ya wanadamu , Mungu na Shetani wote wanagombea kumiliki mawazo ya wanadamu na kuyatumia kuishi ndani ya mwili wa mwanadamu. SHETANI NA MUNGU WANAPIGANIA KILA MMOJA KUMILIKI MAWAZO YA MWANADAMU, MWANADAMU ANAYEKUBALI MAWAZO YAKE KUTEKWA NYARA NA KUTUMIWA NA SHETANI DAIMA HATMA YA MAISHA YAKE INAKUWA MIKONONI MWA SHETANI NA UUMBAJI WA MUNGU.

..................................................MWISHO........................................

No comments:

Post a Comment