Monday, March 10, 2014

KUWEKA AGANO NA MUNGU (2)







Na Joseph Goliama
 HATUA YA TATU YA USHUHUDA HUU SOMA HAPA
Wakati nawaza sana kuhusu Mungu ni Upendo nilijiona gafla nipo maeneo ya chuo kikuu cha Dar es salaam baadae nikapelekwa katika vyuo vingine na nikatembezwa shule za sekondari Dar na mwisho nikajiona nipo mahakama ya kisutu na mahakama ya mwanzo kariakoo nikiwa katika hali hiyo huku kwa wakati mmoja najihisi ninaona kuwa nipo katika maeneohayo yote nikasikia swali kutoka kwa Mungu akiniuliza Mwanangu kote duniani katika maeneo kama haya watu huenda kutafuta nini? ndipo nikawa nawaza chakujibu wakati nataka kutamka cha kujibu ghafla nikasikia nanong'onezwa niseme kwamba watu huenda katika maeneo hayo yote kutafuta Haki, nami nikamwambia Mungu nikasema katika maeneo kama hayo duniani kote watu huenda kutafuta haki, nikamwambia kule chuo kikuu, mashuleni na vyuoni watu huenda kutafuta haki yakuwa na elimu ili wawe na maisha bora, nakule mahakamani nikamwabia Mungu kuwa watu huenda kutafuta haki zao za aina mbalimbali, ndipo Mungu akaniambia Mwanangu kumbuka siku zote za maisha yako mimi Mungu ni Haki, aliponiambia kuwa yeye Mungu ni haki niliingia katika mawazo mengi sana nikawaza kumbe wanadamu tunapotafuta haki ndani ya maisha yetu ndani ya ndoa ndani ya familia ndani ya ukoo ndani ya kabila ndani ya chama ndani ya Taifa ndani ya huduma ndani ya shirika ndani ya taasisi ndani ya bara ndani ya EAC ndani ya Umoja wa mataifa na katika kila eneo la maisha kumbe tunamtafuta Mungu pasipokujua ,kwakweli niliwaza sana tena sana kwa jinsi Mungu alivyojifunua kwangu siku ile hata hivyo wakati nawaza hayo Mungu akaniambia Mwanangu pamoja nakwamba Mimi Mungu ni uzima ni upendo nani haki lakini sina umbo ,akaniambia sina umbo ndio maana niliwaambia wana wa Israel wasinifananishe na kitu chochote kilicho juu mbinguni kilicho chini ya dunia au kilicho majini chini ya dunia kwakuwa mimi sifanani na chochote. Mungu akaniambia kwakuwa sifanani nachochote ndio maana hata uzima huwezi ukaufanananisha na chochote kwakuwa hauonekani pia akaniambia kuwa kwakuwa hafanani na chochote ndio maana hata upendo haufanani na chochote japo upo na pia akaniambia kuwa kwakuwa hafanani na chochote ndio maaana hata haki huwezi kuifananisha na chochote. Ndipo Mungu akaendelea kuniambia kuwa kwakuwa hana Umbo ndio maana aliishi ndani ya Kristo Yesu na kumtumia Kristo Yesu kujifunua hapa duniani, akaniambia watu wote waliomfuata Yesu hawakumfuata kwasababu ya sura yake au kwasababu ya umbo lake au kwasababu ya taifa lake au kwasababu ya mavazi yake au kwasababu ya rangi yake au kwasababu ya chochote alichokuwa nacho au alivyoonekana , Mungu akaniambia wazi Kuwa waliomfuata Yesu walimfuata kwasababu alikuwa na yeye Mungu yaani Yesu alikuwa na Uzima alikuwa na Upendo alikuwa na Haki yaani Yesu hapa duniani alikuwa na Mungu Baba yake wa Mbinguni
Ndipo kwa mara ya kwanza nilijua wazi kuwa Uzima,upendo na haki aliishi ndani ya Yesu Kristo naye Uzima ,upendo na haki ndiye Mungu wetu wa milele.
Baada ya Mungu kuniambia maneno hayo ndipo akasema..................

HATUA YA NNE YA USHUHUDA HUU HII HAPA ISOME
Baada ya Mungu kujifunua kwangu nakunithibitishia kwamba yeye ni Uzima ni Upendo nani Haki ndipo akaniambia kama nilivyoishi na Yesu Kristo na kutembea na Yesu Kristo hapa duniani Pia nimekuchagua wewe nataka kuishi nawewe na kutembea nawewe hapa duniani kama nilivyoishi na kutembea na Yesu Kristo, maneno haya hayakuwa rahisi kwangu kwani nilikuwa kijana mdogo kwa umri nasikuwa najitambua kama ninavyojitambua hivi leo, na kwakweli maisha yangu yalikuwa njia panda kwa mambo mengi wakati huo , nikiwa pale chini hofu ilikuwa kubwa sana moyoni mwangu lakini amani ilikuwa kubwa zaidi hivyo niliendelea kumsikiliza Mwisho Mungu akasema namimi akaniambia ninakutuma kwenda duniani katika kizazi chako kwenda kunitambulisha ili wanadamu wanijue mimi Mungu wa pekee wa kweli niliyemtuma Yesu Kristo na manabii na mitume wengine
Kwakweli
Kwakweli utukufu wa Mungu niliokutana nao siku ile sijawahi kukutana nao maisha yangu yote hakika Mungu ana nguvu na mamlaka yake ni ya milele, baada ya utukufu wa Mungu yaani uwepo wa Mungu kuniachia nilirudi katika akilia yangu ya kawaida nakujikuta nipo pale pale sebuleni nilipokuwa awali kabla sijaingia katika kukutana na uwepo wa Mungu na utukufu wa ajabua. nilijifunza nini kwa Mungu kujitambulisha kwangu? ninini nilifanya baada ya tukio hilo? Mungu amenituma kufanya nini duniani kuanzia Tanzania

HATUA YA TANO YA USHUHUDA HUU HII HAPA ISOME
Baada ya Mungu kunitokea na kujifunua kwangu ndipo kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilimjua Mungu wa pekee wa kweli nilimjua Mungu kwamba kumbe hana umbo kama wengine wanavyofikiria nilijua Mungu anaweza kuingia ndani ya mwanadamu yeyote amtakaye na kumtumia kukutana na shida za wanadamu wengine, nilijua wazi kuwa Matatizo ya wanadamu ndio ibilisi na majibu ya matatizo ya wanadamu ndio Mungu mwenyewe yani hapa nilijua kwa hakika kuwa wanadamu tunasumbuliwa na shetani yaani shetani ni Mauti, Uovu na yasiyo ya haki na ndipo nilijua wazi jibu la matatizo yaani jibu la shetani duniani ni Mungu yaaani Uzima, upendo na haki kwa hakika nimejua wazi kuwa wanadamu wakimjua Mungu watajua namna ya kumsinda shetani ambaye ni adui wa MUNGU NAni adui yao , kwa hakika mimi binafsi nimejua wazi wanadamu wote wa dini zote makabila yote na mataifa yote sote tunamuhitaji Mungu yaani tunaitaji uzima, upendo na haki na daima tunaishi maisha ya kumtafuta bila kujua kuwa tunamtafuta Mungu. kwa hakika maisha yangu tangu nimjue MUNGU yamebadilika sana hivi sasa ninaishi na Mungu na ninatembea na Mungu kumfunua kwa wanadamu wengine wote wanaomuhitaji katika maisha yao
Katika maisha yangu nimegundua kwa hakika kuwa miili ya wanadamu,ndoa zao, familia zao,ko zao, makabila yao, vyama vyao, mataifa yao, huduma zao, taasisi zao, mashirika yao, vikundi vyao, madhehhebu yao, dini zao, mabara yao na umoja wa mataifa vyote vinahitaji Uzima , upendo na haki, na ndivyo ambavyo wanadamu katika maeneo hayo ya maisha wanavipigania na kuvitafuta daima, pia niligundua kitu kimoja nacho ni kwamba popote palipo na uzima pana amani, hivyo twaweza kusema wakati mwingine kuwa Mungu ni amani ni upendo nani haki kwakusema hivi nataka ujue wazi kuwa Amani , upendo na haki ndio msingi wa maisha ya mwanadamu katika ndoa ,familia, ukoo nk... ITAENDELEA

No comments:

Post a Comment