Sunday, March 9, 2014

KUWEKA AGANO NA MUNGU









 JOSEPH GOLIAMA

AGANO NA MUNGU
Agano na Mungu ni maafikiano na Mungu, ni makubaliano baina yako na Mungu, ni mapatano na Mungu wako, kufikia agano na Mungu au kuweka agano na Mungu ni lazima kwa kila mwanadamu anayetaka kuingia mbinguni, agano na Mungu ni makubaliana ambayo unapaswa wewe binafsi mwanadamu uyaingie na Mungu wako makubaliano ya kuamua kuyatoa maisha yako kuishi na Mungu na kutembewa na Mungu siku zote za maisha yako ya hapa duniani
Kuweka agano na Mungu kunawezekana endapo tu utamjua Mungu na endapo utayajua maisha anayoyaishi Mungu wako, kuweka agano na Mungu ni sawa na kuweka agano la ndoa na mume wako au mke wako mnayetaka kuoana, kwanza kabla ya kuingia agano la ndoa ni lazima kila mmoja amjue mwenzi wake kumjua mwenzi wako kunakupa fulsa ya kujua kama atakuwa msaada kwako katika maisha ya ndoa pili unapaswa kujua maisha ambayo mwenzi wako anayaishi hii itakupa kujua kama maisha yake yanaendana nawewe au maisha yake yatakua sababu ya ndoa yenu kuwa na matatizo na kuvunjika...ndivyo ilivyo katika maisha kama unataka kuweka agano na Mungu kwanza unapaswa kujua Mungu ninani pili utapaswa kuyajua maisha ya Mungu anayoyaishi, baada ya kuyajua mambo hayo mawili ndipo sasa waweza kuweka makubaliana na Mungu ya kuishi nayeye na kutembea naye hapa duniani kwasababu mnakua mmejuana
SOMA USHUDA HUU JINSI MUNGU ALIVYONITOKEA MIMI NAKUJITAMBULISHA KWANGU NAMIMI NIKAMJUA
Ndugu wanadamu wenzangu napenda kuwashuhudia jinsi nilivyokutana na Mungu na maisha yangu kubadilika ilikuwa mwaka 2007 mwezi wa saba nikiwa naishi tegeta siku hiyo ilikuwa yapata kama saa saba mchana, nikiwa chumbani ghafla nilijisikia kama moyoni nimetenda dhambi ambayo ilikuwa ikinisuta nikaanza kuomba rehema za Mungu niliomba kwakuwa nilijisikia hatia sana, wakati ninaomba nilianza kutembea huku na huku mpaka nikafika sebuleni, nikiwa sebuleni huku nikiomba nikahisi kama moshi unatokea na kujaa pale sebuleni, hali ile ilinishangaza sana nikahisi kama kuna mtu pengine amekoka moto ndio maana dirishani moshi unapenya, hivyo nikaamua kukatiza maombi na kutoka nje ,nilizunguka nyumba yote niliyokuwepo kuona kama kuna mtu amewasha moto katika ile nyumba, hata hivyo sikuona moto wala dalili za moto nikaamua kurudi ndani nilipofungua mlango huku nikiendela kuomba nikaona ule moshi ndio kwanza unazidi nakuongezeka sana, kwakweli niliingiwa na uwoga sana, wakati natafakari hali hiyo gafla nikakumbuka mafundisho aliyonifundisha mchungaji mmoja jina nalihifadhi aliyeniambia habari za alama zinazoonyesha uwepo wa Mungu naye alinitajia kuwa Wingu, Moto,Njiwa, Malaika, Moshi na alama nyingi nimezisahau kuwa ni alama zinazoonyesha uwepo wa Mungu na yakwamba Mungu ameonekana akijifunua kupitia alama hizo mara kwa mara alipokuwa anawatokea wanadamu kwa kwakuwa yeye hana umbo. Mara baada ya kukumbuka jambo hilo nilipiga magoti chini na kusujudu ,nilipokuwa nasujudu gafla nilisikia sauti ikiniambia usiogope mara Nne iliongea maneno hayo, usiogope...usiogope...usiogope...usiogope nimimi Mungu nimekuja kujifunua kwako ili unijue nataka unitambulishe katika kizazi chako ilisema sauti ile
Nikiwa nimesujudu pale chini hofu ilinitawala nisijue lakusema nikiwa sielewi niseme nini ile sauti ikaniambia tena nimekuja kujitambulisha kwako kama nilivyokuahidi ndipo sasa nilijua kuwa Mungu anaongea nami akaniambia yafuatayo
Mwanangu mimi Mungu ndiye yule ambaye ninyi wanadamu kote duniani katika mataifa yote mnanitafuta kwasababu mnanihitaji, akarudia tena mara ya pili akaniambia Mwanangu mimi Mungu ndiye yule ambaye ninyi wanadamu kote duniani katika mataifa mbalimbali mnanitafuta kwasababu mnanihitaji aliponiambia kwa mara ya pili nikajiuliza hivi hapa duniani katika mataifa yote sisi wanadamu tunatafuta nini? wakati najiuliza swali hilo akaniambia tena akasema mwanangu mimi Mungu ndiye yule ambaye ninyi wanadamu kote duniani katika mataifa mbalimbali mnanitafuta sana kwasababu mnanihitaji sana mnanitafuta kwa kuzunguka huko na huko duniani kunitafuta,mnanitafuta kwa kupanda ndege, kwakupanda meli kwakupanda magari kwakupanda treni kwakupanda wanyama kwakutembea kwa miguu na kwa njia nyingine nyingi kwasababu mnanihitaji sana. Baada ya Mungu kuniambia maneno hayo nilijiuliza sana juu ya maneno hayo nikawa najiuliza hivi sisi wanadamu tunatumia vyombo vya usafiri na miguui tunazunguka huku na huko tunatafuta nini kote duniani? wakati najiuliza maswali hayo gafla nilijikuta nipo hospitali ya muhimbile kisha nikajiona nipo hospitali ya mwananyamala na kisha nikajiona nipo hospitali ya mikocheni mbele yangu niliwaona wagonjwa wakila kiungo wamelazwa mawodini na wengine wako nje ya hospitali, hali ilikuwa mbaya sana kwasababu hospitali karibu zote niliona zimefulika wagonjwa niliwatambua wagonjwa wa kansa wa matumbo wa ngozi wa nywele wa masikio, wa macho karibu kila mgonjwa alisumbiliwa na kiungo kimoja ua kadhaa, nikiwa kwa huzuni na fadhaa nikiwaona wale wagonjwa kafla nilisikia sauti ya Mungu ikiniuliza maneo yafuatayo 'bila shaka watu hao wametoka sehemu mbalimbali za dunia hii na wamekuja kwa kutumia njia mbalimbali wanatafuta nini mahali hapo? ni swali ambalo kwakweli lilinipa kuwaza sana wakati najiandaa kulijibu nikasikia sauti ya ndani kama inaniong'oneza ikiniambia sema wamekuja kutafuta Uzima wa viungo vya miili yao name bila ajizi nikasema MUNGU WATU HAWA wanahitaji uzima katika miili yao ndio maana wapo hospitali nikaonyesha nikasema mtazame yule anatafuta uzima wa jicho yule uzima wa miguu yule uzima wa tumbo yule uzima wa damu yule uzima wa mifupa yake yule uzima wa kiuno yule uzima wa matiti yule uzima wa shingo yule uzima wa meno yule uzima wa goti yule uzima wa ..........nilitaja kila kiungo kilichokuwa kinahitaji uzima baada yakumaliza kumuambia Mungu hitaji la watu niliokuwa nawaona ndipo Mungu akasema name akaniambia Mwanangu usisahau siku zote za maisha yako kwamba Mimi Mungu wako ni Uzima
Neno hilo lilinipa mshangao sana nikajiuliza moyoni inamaana wanadamu wanapotafuta uzima kumbe wanamtafuta Mungu bila kujua?kumbe Mungu ni Uzima ufunuo huu mara ya kwanza ulinipa kujua wazi kuwa Mungu ni Uzima unapohitaji Uzima katika mwili wako kumbe unamuhitaji Uzima yaani unamuhitaji Mungu
HATUA YA PILI YA USHUHUDA HUU NI HII ISOME
Nikiwa katika dimbwi zito la kutafakari kuhusu Mungu ni Uzima na jinsi wanadamu tunavyotumia ghalama kubwa kutafuta uzima ,kumbe hatujui kuwa tunamtafuta Mungu ndipo nikajiona nipo mbele za umati wa watu wengi sana, watu wale niliowaona walikuwa wengi na idadi yao sikuweza kabisa kuijua na walikuwa katika makundi matatu, kundi la kulia kwangu walikuwa ni watoto niliowatambua kuwa ni yatima na katikati niliwaona wakina mama ambao niliwatambua kuwa ni wajane na kushoto niliwaona wadada ambao kimsingi nilijua kuwa ni makahaba, huku nikiwaangalia watu hawa wote kwa makini nilisikia sauti ya Mungu ikisema name na kuniuliza ikisema, 'bila shaka watu hawa wapo kote duniani katika maisha yao wanatafuta nini? swali hili lilikuwa gumu kwangu kulijibu mara moja wakati nawaza nijibu nini nikasikia sauti ndani ya moyo wangu ikininong'oneza tena ikisema sema wanatafuta Upendo maishani mwao, nami bila ajizi nikasema Mungu wangu hawa watu katika maisha yao wanatafuta upendo nikamwambia waangalie wale watoto yatima wazazi wao wamefariki wanatafuta mtu atakayewahudumia kama wazazi wao walivyokuwa wanafanya, wanahitaji mtu anayeweza kuwajali na kuwathamini ili waendelee kushi kama watoto wengine, tena nikamwambia wale kina mama wajane nao wamefiwa na waume zao wanahitaji mtu wakuweza kuwahudumia kuwaonyesha upendo kama waume zao walivyokuwa wanawahudumia kwa kuwaonyesha upendo na nikamwambia na wale wanadada makahaba nao pia wanahitaji upendo maishani mwao wanahitaji kuendesha maisha yao wanahitaji kuishi hivyo wanahitaji kuhudumiwa ili waache maisha yao machafu kimsingi nilimwambia Mungu kuwa makundi yote matatu yanahitaji upendo, kujaliwa ,kuthaminiwa .ndipo Mungu akasema namimi nakuniambia 'mwanangu kumbuka siku zote za maisha yako kuwa mimi Mungu ni UPENDO, aliponiambia kuwa yeye Mungu ni Upendo ghafla niliingia katika dimbwi zito sana la mawazo nikawa nawaza kumbe wanadamu tunapotafuta upendo kumbe tunamtafuta Mungu pasipokujua kuwa tunamtafuta Mungu kuanzia pale nikawa nawaza mambo mengi sana tena nikawa nawaza maisha yangu nilipotoka na pale nilipo, wakati nawaza haya gafla nikajiona nipo... ITAENDELEA KESHO USIKOSE MWENDELEZO HUU WA MAKALA ITAKAYO BADILISHA MAISHA YAKO.

No comments:

Post a Comment