Monday, November 25, 2013

HATIMAYE FAMILIA YA DONNIE McCLURKIN YAMPUMZISHA BABA YAO

Donnie McClurkin mkono wa kuume akiwa na marehemu baba yake katikati pamoja na ndugu yao wakifurahia jambo.

Hatimaye familia ya gwiji la muziki wa injili Donnie McClurkin wamepumzisha mwili wa baba yao siku ya jumamosi katika mazishi ambayo yalihudhuriwa na familia pamoja na watu wa karibu wa familia hiyo, mazishi hayo yamefanyika huko Manhattan jijini New York ambapo awali yalitanguliwa na ibada ambayo pia ilishirikisha ndugu hao na marafiki zao wa karibu.


Donnie akiwa na watoto wake wawili Michelle na Matthew pamoja na ndugu wa familia hiyo ambao baada ya mazishi walikwenda kwenye moja ya mgahawa na kupata chakula pamoja ikiwa pamoja na kumaliza siku nzima wakiwa pamoja kama familia. Ni takribani miezi 10 sasa tangu mwanamziki huyo kufiwa na mama yake ambapo wiki moja iliyopita ndipo alipokufa baba yake mzazi ambaye katika maelezo yake Donnie amesema alikuwa mtu wake wa karibu sana na rafiki kipenzi.


Baba na watoto wake mara baada ya ibada ya mazishi.

Baba mdogo na shangazi zake Donnie wakiwa katika picha ya pamoja.

Michelle na Matthew watoto wa Donnie wakiwa katika picha ya pamoja.


Dada yake na Donnie mchungaji Andrea akiwa amembeba mmoja wa watoto kutoka familia yao baada ya ibada ya mazishi.

Familia picha za pamoja.

Picha inayoonyesha jeneza na Donnie akiwa mbele wakati wa mazishi, familia haijaachilia picha kamili za makaburini.

Familia ya McClurkin wakipata chakula cha pamoja baada ya mazishi.SOURCE: GOSPEL KITAA BLOG

No comments:

Post a Comment