Monday, January 13, 2014

Gwajima avamiwa usiku, anusurika kuuawa


Na Jelard Lucas

ILITOKEA lakini haikuandikwa kwa sababu haikudakwa!

 Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lenye makazi yake

 kwenye Viwanja vya Tanganyika Perkas, Kawe jijini Dar,

 Josephat Gwajima alinusurika kuuawa mara tatu kufuatia 

kuvamiwa na majambazi watatu mwishoni mwa mwaka jana.
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.

Akizungumza na Risasi Jumamosi hivi karibuni, Gwajima

 alisema tukio hilo lilijiri nyumbani kwake, Mbezi Beach jijini

 Dar ambapo siku ya kwanza, majambazi hao waliingia 

nyumbani kwake saa nne usiku wakiwa wameficha sura na 

kumkuta yeye sebuleni ambapo walimuuliza, ‘Gwajima yuko

 wapi?’

“Ni kweli nilinusurika kifo na majambazi, walinivamia mara

 tatu nyumbani. Zilikuwa siku mbaya maishani mwangu.

 Siku ya kwanza walikuja na bunduki huku wameficha sura, 

walinikuta sebuleni, wakaniuliza alipo Gwajima, niliwajibu

 ametoka, wakaondoka wakisema watarudi kesho yake.

“Nilijua ni utani, lakini kweli siku iliyofuata saa nne usiku 

walikuja tena, wakanikuta ndiyo naingia nyumbani, 

wakaniambia niko chini ya ulinzi, nilimuomba Mungu aokoe

 maisha yangu kwani nilipatwa na mshtuko, wakahoji; 

‘Gwajuma yuko wapi?’ Kabla sijajibu mmoja akasema; ‘huyu

 bwana mdogo ndiye tuliyemkuta jana,’ wakaondoka.

“Sikuwa na wazo la kuripoti polisi ila nilimwamini Mungu 

aliye hai. Siku ya tatu walipitia juu ya paa kwa kung’oa vigae

 na kushukia chumbani wakiwa na bunduki.

“Mimi nilikuwa kitandani na mke wangu, wakauliza tena

 Gwajima yuko wapi? Nikawajibu bado hajarudi, wakasema;

 ‘haka (Gwajima) ndiyo kale kale ka bwana mdogo ka jana.’

“Mungu mkubwa, kwa nje zilisikika kelele za mbwa kisha 

wakatoweka ghafla, niliona ni siku za majaribu kwangu,

 nilimwomba Mungu atupilie mbali majaribu yale, baada ya

 siku kadhaa niliamua kuhama kwenye nyumba ile.

“Ila nakumbuka ile siku ya mwisho walisema tunamtaka

 Gwajima kwa sababu anajifanya kufufua misukule kisha 

anataja majina yetu.

“Ndipo nilijua kumbe kisa ni kufufua misukule. Najua umbo

 langu ndiyo mkombozi wa yote kwani waliponiona walijua

 Gwajima hawezi kuwa na umbo dogo kama mimi nilivyo,”

 alisema Gwajima.

Katika mahojiano marefu na gazeti hili, mchungaji huyo 

alisema kuwa mpango wa kumuua uliofanywa na mtu

 ambaye aliwahi kutajwa jina na binti msukule aliyemfufua

 kanisani kwake. Alisema mtu huyo aliyetajwa na msukule

 ni  mtumishi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (jina 

hakumtaja).

No comments:

Post a Comment